Posts

Showing posts from January, 2024

WASICHANA TUMBI SEKONDARI WAMPA HESHIMA RAIS SAMIA

Image
Esther Kilamwegula msichana pekee aliyepata daraja la kwanza alama ya nane kutoka shule ya Sekondari Tumbi  Kibaha Na. Gustafu Haule,Pwani WANAFUNZI wakike 34 waliofanya mtihani wa kumaliza kidato cha nne mwaka 2023 katika Shule ya Sekondari ya Wananchi Tumbi iliyopo Halmashauri ya Mji Kibaha wamempa  heshima Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuonyesha maajabu makubwa ya ufaulu. Maajabu hayo yametokea kwa mara ya kwanza katika Shule ya Kata Sekondari  Tumbi kwa kuhakikisha wanafunzi wote wakike waliofanya mtihani  huo kufaulu kwa kiwango cha juu jambo ambalo limepelekea Shule hiyo kufanya vizuri kwa Mkoa wa Pwani.   Ufaulu wa wanafunzi hao wa kike ni heshima kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Makamu wa  Rais Dkt.Philipo Mpango ambaye mwaka jana alitoa motisha ya  Sh.milioni 50 Kwa walimu wa Shule hiyo baada ya kupokea ripoti ya matokeo mazuri ya ufaulu shuleni hapo.   Mkuu wa Shule ya Sekondari ya ...

MARUFUKU GARI LA WAGONJWA KUGEUZWA DALADALA KIBAHA

Image
Na Julieth Mkireri,  Kibaha. MBUNGE wa Jimbo la Kibaha Vijijini Michael Mwakamo,amepiga marufuku tabia ya kutumia magari ya wagonjwa kama daladala la kubebea watendaji kuwapeleka kazini na kuwarudisha makwao na badala yake magari hayo yafanyekazi iliyokusudiwa.   Mwakamo,ametoa tahadhari hiyo wakati akikabidhi gari la kubebea wagonjwa kwa mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Kibaha Vijijini ikiwa ni kwa ajili ya  matumizi katika hospitali ya Wilaya iliyopo Mamlaka ya Mji mdogo wa Mlandizi.   Mwakamo amesema ili gari hilo liweze kudumu kwa muda mrefu linatakiwa kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa ambayo ni kubebea wagonjwa pamoja na dharula nyingine zinazohusiana na masuala ya hospitali. "Gari hili linakuja kuondoa kikwazo cha uhaba wa magari kilichokuwepo awali, natoa angalizo lisitumike kama daladala ya kubebea watendaji wanapoenda kazini, pandeni daladala, bajaji sio kupanda kwenye hili gari, mkifanya hivyo tatizo litarudi tena," amesisitiza. Mwakamo,pam...

AWESO AKEMEA MATUMIZI MABAYA FEDHA ZA MAJI

Image
Aonya, vipo vya kuchezea ukishiba chezea kidefu au kitambi chako sio fedha za miradi ya maji      Waziri wa maji Juma Aweso  akizungumza na wananchi (hawapo pichani )Kata ya Chumbi Wilayani Rufiji Mkoani Pwani. Na. Julieth Ngarabali. Rufiji   Waziri wa Maji Juma Aweso  amezindua skimu ya maji inayohudumia zaidi wananchi 8,000 katika kata ya Chumbi Wilayani Rufiji na kuielekeza jumuia ya watumiaji huduma hiyo kuhakikisha pesa walizokubaliana zinakusanywa na kupelekwa benki kwenye akaunti .    Aweso ametoa maelekezo hayo wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Chumbi Rufiji Mkoani Pwani  na kusisitiza kuwa vipo vya kuchezea na sio pesa za miradi ya maji   ‘’ Tunajua mmeweka pesa ambayo mmekubaliana unapotaka kuchota maji lazima uchangie ,niwasihi jumuia iayosimamia hili fedha inapokusanywa ipelekwe benki kwenye akaunti  na nataka niwaambie vipo vya kuchezea ukishiba chezea kidefu chako au kitambi chako sio fedha za miradi...

SERIKALI YATOA MATREKTA KWA WAKULIMA KIBAHA

Image
Na Gustafu Haule,Pwani MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge, amesema Mkoa  umeanza kutimiza adhma ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt.Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha Tanzania inakuwa nchi inayoweza kuilisha dunia. Kunenge, ameyasema hayo Januari 26/2024 wakati akikabidhi matrekta matatu kwa mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John yaliyotolewa na serikali kwa ajili ya wakulima wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha wanaofanya kilimo cha pamoja. Amesema,Mkoa umeweka utaratibu wa kuhakikisha mabadiliko ya haraka yanaonekana na kuunga adhma ya Rais ya kulisha nchi jirani na dunia ambapo ameonyesha nia ya dhati kwa kuweka mazingira mazuri ikiwa ni pamoja na kuweka wataalamu, vitendea kazi na vifaa vingine vya kilimo. Aidha,Kunenge ameipongeza Wilaya ya Kibaha kwa kutenga eneo lenye ukubwa wa hekari 1,650 kwa ajili ya kilimo cha pamoja  cha mazao ya kilimo biashara na kuunganisha kilimo na viwanda kwa ajili ya kutoa ajira.  "Kilimo kiungane na uchumi wa buluu ku...

YANAYOENDELEA KIKAO CHA MAKATIBU WAKUU WA VYA VYA SIASA

Image
  Shule ya uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere (MJNLS)  Kibaha Pwani Makatibu wakuu wa vyama sita marafiki vya Ukombozi kusini mwa Afrika, wakisaini katiba ya usimamizi na uendeshaji wa shule ya uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere (MJNLS), eneo la kwa Mfipa, Kibaha, mkoani Pwani, Tanzania.  Kuanzia katikati kwenda kulia ni  Dk. Emmanuel John Nchimbi, Katibu Mkuu wa CCM (Tanzania), Prof. Marcelina Chijoriga, Mkuu wa Shule ya MJNLS, Francisco Mucanheia, mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Chama cha FRELIMO (Msumbiji) na Fikile Mbalula na Katibu Mkuu wa ANC (Afrika Kusini)  Obert Moses Mpofu, Katibu Mkuu wa Chama cha ZANU- PF (Zimbabwe),Sophia Shaningwa Katibu Mkuu wa Chama cha SWAPO (Namibia) na  Manuel Domingos Augusto, mwakilishi wa Katibu Mkuu wa MPLA (Angola).  Makatibu wakuu wa vyama sita marafiki vya ukombozi kusini mwa Afrika, wakionesha nakala ya Katiba ya usimamizi na uendeshaji wa shule ya uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere (MJNLS), baada ya kutia saini, h...

DK.NCHIMBI ATETA NA VYAMA VYA SIASA VYA UKOMBOZI

Image
Asema CCM itashinda kwa kishindo uchaguzi Serikali za Mitaa 2024 na uchaguzi Mkuu 2025 Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),Dkt. Emmanuel Nchimbi akizungumza wakati wa kufungua kikao cha kazi cha Makatibu Wakuu wa Vyama Sita rafiki vya Ukombozi Kusini mwa Afrika. Makatibu Wakuu hao ambao wamekutana Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere (MJNLS), iliyopo Kibaha, mkoani Pwani, leo Alhamis Januari 25, 2024, kujadili masuala mbalimbali, ni kutoka vyama vya SWAPO (Namibia), ZANU-PF (Zimbabwe), ANC (Afrika Kusini), MPLA (Angola) na FRELIMO (Msumbiji). Mwandishi  wetu Kibaha. Katibu mkuu wa chama cha Mapinduzi Taifa Balozi Dkt.  Emanuel Nchimbi   amewahakikishia Makatibu Wakuu wa Vyama Sita vya Ukombozi wa Nchi za Kusini mwa Afrika kwamba chama cha  Mapinduzi  kina uhakika wa  kushinda kwa kishindo katika changuzi za mwaka huu na mwaka kesho, kwa maana ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu mwaka 2025.  Dkt. Nchimbi ametoa kauli hiyo...

Makamu wa Rais wa Cuba atembelea Viuadudu Kibaha

Image
Makamu wa Rais wa nchi ya Cuba Salvador Valdes Mesa akizungumza na viongozi mbalimbali wa Serikali katika kiwanda cha kuzalisha viuadudu wa mazalia ya Mbu kilichopo Kibaha Mkoani Pwani ziara hiyo alifanya Januari 24 mwaka huu.  Na Gustafu Haule,Pwani MAKAMU wa Rais wa Muungano wa nchi ya Cuba Salvador Valdes Mesa amefanya ziara ya kutembelea na kukagua kiwanda cha Tanzania Biotech Products  Limited (TBPL) kilichopo Kibaha Mkoani Pwani. Kiwanda hicho kimejengwa kwa ushirikiano wa nchi mbili ikiwemo Tanzania na Cuba ambapo kazi yake ni kuzalisha viuadudu wa kutokomeza mazalia ya Mbu pamoja na kutengeneza dawa mbalimbali kwa ajili ya kuua wadudu wanaoshambulia mazao. Kiongozi huyo mkubwa kutoka nchini Cuba amefanya ziara hiyo Januari 24 mwaka huu  akiambatana na viongozi mbalimbali wa Serikali ya Tanzania akiwemo Balozi anayewakilisha Tanzania nchini Cuba Humphrey Pole pole. Viongozi wengine waliokuwepo katika msafara huo ni Waziri wa Viwanda na Biashara Ashatu Kijaji ,Wazir...

RC KUNENGE APIGA KAMBI BAGAMOYO KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI WILAYANI HUMO

Image
Na Gustafu Haule,Pwani MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge,leo Januari 24 amefika Wilayani Bagamoyo kwa ajili ya kusikiliza kero za wananchi hususani migogoro ya ardhi. Katika ziara hiyo Kunenge ameambatana na wataalamu kutoka  ofisini kwake ikiwemo kitengo cha idara ya ardhi na Sheria pamoja kamati ya ulinzi na usalama ya Wilayani Bagamoyo. Mkuu wa Mkoa wa Pwani akiwa na wataalamu kutoka Ofisi yake na Kamati ya Ulinzi na Usalama wilaya ya Bagamoyo katika Mkutano na wananchi wilayani humo Kunenge,amefika Wilayani Bagamoyo ikiwa ni sehemu ya kutekeleza maagizo ya Waziri wa Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ( Tamisemi) Mohamed Mchengerwa aliyoitoa mwishoni mwa wiki iliyopita Wilayani Bagamoyo. Mchengerwa,alitoa maagizo hayo katika ziara ya Katibu wa Itikadi,Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Paul Makonda ambaye alipita Wilayani humo na kupokea changamoto mbalimbali ikiwemo masuala ya Ardhi. Akiwa Wilayani Bagamoyo Kunenge amekutana na wananchi mbalimbal...

MAKONDA AFICHUA SIRI MAANDAMANO CHADEMA

Image
    Katibu wa Itikadi,Uenezi na Mafunzo  chama cha Mapinduzi (CCM)Paul Makonda Na Mwandishi wetu KATIBU wa Itikadi,Uenezi  na Mafunzo wa chama cha Mapinduzi (CCM)Paul Makonda amefichua siri ya maandamano ya chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)  yaliyopangwa kufanyika wiki ijayo kuwa ni njia anayotumia mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe  kukwepa uchaguzi wa ndani. Makonda amebainisha hayo alipokuwa katika ziara yake ya siku moja  Mikoa ya Dar es Salam na Pwani ambapo alitumia nafasi hiyo kuzungumza na wananchi kwa kutatua kero zao mbalimbali zikiwemo za migogoro ya ardhi. “Mimi ninafahamu hii taarifa na nimeitoa kwa mtu wa ndani sana kumbe kuna uchaguzi wa ndani ya chama,Katibu wa chama hicho John  Mnyika ameamua kumbeba Mbowe kwasababu mwenyekiti huyo amegundua hawezi kumshinda Makamu wake Tundu Lissu,” anasema Makonda Amesema   taarifa alizonazo ndani ya chama hicho wanalalamika kwanini Mnyika anaungana na Mbowe kumhujumu Tu...

NOTI BANDIA ZA ZAIDI YA MIL.13 ZADAKWA PWANI

Image
    Noti za pesa  bandia zilizokamatwa Pwani  Baadhi zilishaingia kwenye mzunguko wa matumizi Msata     Mwandishi wetu. Pwani.WATU wanne wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Pwani  kwa tuhuma za kukutwa na noti za  pesa bandia za thamani ya zaidi ya sh. 13  milioni pamoja na mtambo  wa kutengeneza pesa hizo. Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani Pius  Lutumo amesema  kukamatwa kwa watu hao  waliokutwa na pesa  sh.1,550,000 milioni  kulitokana na baadhi yao kutiliwa shaka baada ya kufanya malipo ya kukodisha chumba kwenye moja ya nyumba ya kulala wageni   huko Masata Mkoani humo. Amewataja watuhumiwa hao ni Mbaraka Fundi (48)Zena Naringa (42)wakazi wa Buza Jijini Daresalaam wengine  ni  Masumuko Kiyogoma (54) Mkazi wa Goba na Elius  Wandiba (50) mkazi wa kimara Suka Jijini Dar esalaam. ''Kukamatwa kwa watuhumiwa hao kulitokana na taarifa za raia mwema aliyetilia  mashaka  noti ya sh....

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI ATOA MIONGOZO 10 KWA MAWAKILI

Image
   Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dkt.Eliezer Feleshi, akizungumza na mawakili wafawidhi wa Serikali pamoja na viongozi wa ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakati akifungua mafunzo ya siku tano   katika chuo cha Uongozi cha Mwalimu Nyerere Kibaha Mkoani Pwani. Na Gustaphu Haule,Pwani MWANASHERIA Mkuu wa Serikali  Dkt.Eliezer Feleshi,amewafunda mawakili kutoka ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali kwa kuwapa miongozo 10 inayotakiwa kuzingatiwa pindi wanapotekeleza majukumu yao. Dkt.Feleshi ametoa miongozo hiyo leo Januari 17 wakati akifungua mafunzo ya Viongozi  kwa menejimenti ya ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali yanayofanyika katika Chuo Cha Uongozi cha Mwalimu Nyerere kilichopo Kibaha Mkoani Pwani. Dkt Feleshi ametaja miongozo hiyo kuwa ni pamoja na kuhakikisha mawakili wote wa Serikali wanajifunza maarifa na stadi mpya za kazi bila kukoma ili kuendana na ulimwengu unavyobadilika. Amesema,moja ya miongozo hiyo ni kuandaa dondoo na mawasilisho ya kazi na mrejesho wa ka...

Ushoroba wa tembo: Kivutio kipya milima ya Udzungwa

Image
Ni Ushoroba mpya utakaomaliza pia migogoro ya binadamu na tembo Tanzania                    Njia ya chini ya kupita Tembo(underpass )katika shoroba ya Nyerere -Selous- Udzungwa Na Gustaphu Haule, Kilombero “MWAKA 2018 hatutaweza kusahau katika maisha yetu, jinsi tulivyomwona yule jamaa akiuwawa kwa kuchanwa chanwa na Tembo, yaani tulivyoenda kumuona asubuhi daaah!!!! Hakika tukio lile ni moja ya matukio mabaya yaliyowahi kutokea hapa Magombera. “Kifo cha mwanakijiji mwenzetu Bata Limu kilikuwa kikali sana, kwa kweli kilisikitisha kwa sababu yule mtu alichanwa vipande vipande. Hakika kilikuwa kifo cha majonzi makubwa  na ndio kifo cha kwanza tulichowai kukishuhudia. “Leo hii tunapomuona Tembo sisi wanakijiji wa Magombera tunamheshimu na tunakimbia mbali sana kwa kuwa tunajua kuwa Tembo ni mnyama mwenye madhara makubwa endapo utamsogelea.” Haya ni maneno ya Mwenyekiti wa Kijiji cha Magombera, Kata ya Mkura katika Wilaya ya Kilombero m...