WASICHANA TUMBI SEKONDARI WAMPA HESHIMA RAIS SAMIA





Esther Kilamwegula msichana pekee aliyepata daraja la kwanza alama ya nane kutoka shule ya Sekondari Tumbi  Kibaha

Na. Gustafu Haule,Pwani

WANAFUNZI wakike 34 waliofanya mtihani wa kumaliza kidato cha nne mwaka 2023 katika Shule ya Sekondari ya Wananchi Tumbi iliyopo Halmashauri ya Mji Kibaha wamempa  heshima Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuonyesha maajabu makubwa ya ufaulu.

Maajabu hayo yametokea kwa mara ya kwanza katika Shule ya Kata Sekondari  Tumbi kwa kuhakikisha wanafunzi wote wakike waliofanya mtihani  huo kufaulu kwa kiwango cha juu jambo ambalo limepelekea Shule hiyo kufanya vizuri kwa Mkoa wa Pwani. 

Ufaulu wa wanafunzi hao wa kike ni heshima kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Makamu wa  Rais Dkt.Philipo Mpango ambaye mwaka jana alitoa motisha ya  Sh.milioni 50 Kwa walimu wa Shule hiyo baada ya kupokea ripoti ya matokeo mazuri ya ufaulu shuleni hapo.

 Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Tumbi Fidelis Haule,akizungumza na waandishi wa habari shuleni hapo jana amesema kuwa Shule yake inajivunia kuona wanafunzi wote wakike waliosoma shuleni hapo wamefaulu kwa kiwango cha juu jambo ambalo kwake ni faraja.



Haule ,amesema kuwa katika wanafunzi hao 34 waliopata daraja la kwanza (Division One 14) huku mmoja wao  anayejulikana kwa jina la Esther Kilamwegula akiwa na pointi nane wakati  waliopata daraja la pili (Division Two 16 )daraja la tatu (Division Three 3) na daraja la nne (Division Four 1).

 "Ufaulu wa wanafunzi wa kike katika Shule yetu imefikia asilimia 99 kwakuwa wote wamepata ufaulu wa juu na sisi kama Shule tunajivunia kuwa na matokeo haya ambayo yameleta heshima kwa mama yetu Rais Samia Suluhu Hassan,"amesema Haule

 Amesema kuwa,siri ya wanafunzi hao kufaulu imetokana na nidhamu nzuri inayotekelezwa  na walimu pamoja na wanafunzi wa kike ,motisha kwa walimu ,utambuzi kwa wanafunzi wanaofanya vizuri na hata kuweka malengo katika ufundishaji.

 "Sisi hapa shuleni kwetu tuna utaratibu wa kila mwaka wa kutoa pongezi kwa walimu wanaofanya vizuri katika masomo yao na huwa tunawapa vyeti lakini kwa wanafunzi wanaofanya vizuri pia tunawapa vyeti mbele ya wenzao ili kuwapa moyo wa kusoma kwa bidii,"amesema Haule

 Haule,ameishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwani imetoa fedha nyingi kwa ajili ya kukarabati miundombinu ya Shule ikiwemo kujenga maabara,kuboresha madarasa, kuongeza viti na vifaa vya ufundishaji na kikubwa walichopanga na kulipa fadhila kwa Rais kwa kuhakikisha kila mwanafunzi wakike anafaulu vizuri

 Mkuu wa Shule ya Sekondari Tumbi Fidelis Haule akimkabidhi zawadi mwanafunzi Esther Kilamwegula baada ya kufanya vizuri katika matokeo ya kidato cha nne ya mwaka 2023.

"Rais mama Samia ametuletea kila kitu,yaani majengo mazuri,walimu wakutosha kwahiyo tunakila sababu ya kumshukuru na ndio maana tukasema lazima tuhakikishe tunalipa fadhila na tumefanikiwa kwani wasichana wote wamefaulu tena kwa kiwango cha juu,",amesema Haule 

Mkuu huyo amesema mikakati ya Shule yake ni kuongeza juhudi na maarifa katika ufundishaji ili kuhakikisha wanafunzi wanaomaliza kidato cha nne wanakuwa na matokeo mazuri zaidi na kwamba wanachohitaji ni kuona wanafunzi wakike wanazidi kuwa vinara katika ufaulu ili kuendelea kuunga mkono jitihada za Rais Samia katika kuboresha mazingira ya elimu hapa nchini. 

Kufuatia matokeo hayo mapema jana  Haule  ametoa zawadi ya pesa kwa mwanafunzi wakike aliyefanya vizuri katika mtihani huo Esther Kilamwegula huku akiwataka wanafunzi wa kidato cha nne wanaotarajia kufanya mitihani yao mwaka huu kuongeza jitihada katika masomo ili waweze kufaulu vizuri zaidi. 

Kwa upande wake Esther Kilamwegula ambaye kinara wa matokeo ya kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Tumbi ,amesema kuwa watu wanafikiri sio rahisi kwa Shule za Kata kufaulisha kwa alama za juu lakini kwa Shule ya Sekondari Tumbi imewezekana.



Mkuu huyo amesema kuwa mikakati ya Shule yake ni kuongeza juhudi na maarifa katika ufundishaji ili kuhakikisha wanafunzi wanaomaliza kidato cha nne wanakuwa na matokeo mazuri zaidi.

Hatahivyo,kufuatia matokeo hayo Haule ametoa zawadi ya pesa kwa wanafunzi watatu waliofanya vizuri wakiwemo wawili waliopata daraja la kwanza alama ya Saba (7) na mmoja aliyepata daraja la kwanza alama ya nane(8).

Kwa upande wao baadhi ya wanafunzi waliofanya vizuri katika mtihani wa kidato cha nne mwaka 2023 kutoka Shule hiyo akiwemo Esther Kilamwegula na Omary Ramadhani wamesema nidhanu na bidii ya masomo ndio kitu pekee kilichofanya wafaulu vizuri.

MWISHO 




Club News Editor Julieth Ngarabali

Comments

Popular posts from this blog

RC PWANI AONGOZA WAKAZI PWANI KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA

BARAZA LA MADIWANI KIBAHA MJINI LAMPONGEZA MKURUGENZI WAKE KWA KAZI NZURI ANAYOIFANYA SAMBAMBA NA KUONGEZA MAPATO.

RAIS SAMIA ATANGAZA KIBAHA MJINI KUWA MANISAPAA,MBUNGE KOKA AFURAHIA ASEMA KIBAHA ITANG'AA