MIAKA 30 YA TRA: TEKNOLOJIA NA HUDUMA BORA ZAIMARISHA UHUSIANO NA WALIPA KODI MKOA WA PWANI
Na Charles Kusaga, Pwani Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika maadhimisho ya miaka 30 tangu kuanzishwa kwake tarehe 01 Julai 1996, imedhihirisha ukuaji wa huduma bora na teknolojia huku ikijivunia hatua kubwa iliyofikiwa katika kuimarisha mahusiano mema na ushirikiano thabiti na walipa kodi mkoa wa Pwani. Akizungumza na wadau mbalimbali wa kodi mkoani hapa katika ufunguzi wa kongamano la maadhimisho ya miaka 30 ya TRA kwa mkoa wa Pwani Menejea wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Ndugu Peter Eliona alizungumzia mafanikio ya Mamlaka ya Mapato nchini. Kwa mkoa wa Pwani alieleza kuwa katika kipindi hiki cha miongo mitatu, TRA Mkoa wa Pwani imeshuhudia mabadiliko makubwa kutoka katika mifumo ya kizamani ya ukusanyaji mapato na kuingia katika ulimwengu wa kidigitali. Mabadiliko haya ya kiteknolojia yamekuwa nguzo kuu katika kurahisisha utoaji wa huduma na kuondoa urasimu uliokuwa ukiwapa changamoto wafanyabiashara na wananchi mkoani humo. Pia huduma bora, Elimu kwa wateja na ushirikia...