MADEREVA WA POLISI PWANI WATAKIWA KUWA MFANO BARABARANI
Na. Julieth Ngarabali, PWANI. Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Pwani, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Edson Mwakihaba, amewataka madereva wa Jeshi la Polisi mkoani humo kuwa kioo cha jamii na mfano wa kuigwa wanapokuwa barabarani. Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Pwani, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Edson Mwakihaba Mwakihaba ameyasema hayo , Agosti 14, 2026, wakati akifungua mafunzo ya siku moja kwa madereva wa magari ya polisi, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Benjamin Mkapa Polisi Mkoani Pwani. Mafunzo hayo yanalenga kuwakumbusha umuhimu wa kutii sheria za usalama barabarani bila shuruti. Amesisitiza kuwa kuwa askari polisi hakumpi dereva haki ya kuvunja sheria za barabarani. Hivyo, amewataka kuzingatia kanuni zote ikiwemo kuepuka mwendo kasi, kuheshimu taa za kuongozea magari, na kutoa kipaumbele kwenye vivuko vya watembea kwa miguu (zebra crossings). Washiriki wa Mafunzo ya Madereva wa Magari ya Polisi "Ili kufanikiwa katika mapambano dhidi ya ...