MKOA WA PWANI WATATHMINI MALEZI YA AWALI YA MTOTO: ZAIDI YA VITUO 400 VYA DCCA VIMESAJILIWA
Na Julieth Ngarabali, PWANI. Mkoa wa Pwani umefanya tathmini ya utekelezaji wa Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM) kwa kipindi cha Januari hadi Juni 2026, kinacholenga kuimarisha ustawi na huduma kwa watoto wenye umri wa miaka 0 mpaka 8. Kwenye tathmini hiyo pamoja na mambo mbalimbali yaliyowasilishwa imeelezwa jumla ya vituo 858 vya kulelea watoto wadogo mchana (DCC) vimeainishwa, ambapo vituo 477 tayari vimesajiliwa na vinahudumia watoto 19,478—sawa na asilimia 56 ya vituo vyote vilivyotambuliwa kimkoa. Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji, Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Lidya Mafole amesema pia kuna vituo saba vya malezi ya jamii (Community ECD) vilivyoanzishwa na shirika la BRAC tangu mwaka 2025 ambavyo mchakato wa usajili wake unaendelea. Bi. Lidya Mafole Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mafole amebainisha kuwa katika kipindi hicho, vikao vya tathmini vimefanyika ...