Posts

TRA MKOA WA PWANI YATOA ELIMU YA MABADILIKO YA SHERIA ZA KODI 2026

Image
Na. Charles Kusaga, Kibaha - PWANI Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)  imeendesha semina ya elimu kuhusu mabadiliko ya sheria za kodi kwa mwaka 2026, iliyowakutanisha wafanyabiashara, wahasibu, watoa huduma za kodi na wadau mbalimbali katika Ukumbi wa Destiny, Kibaha Mkoa wa PWANI Lengo la semina hiyo lilikuwa kuwajengea walipakodi uelewa wa mabadiliko ya sheria za kodi, taratibu za ulipaji kodi pamoja na umuhimu wa kuzingatia sheria za kodi ili kuongeza uwajibikaji na kuchangia maendeleo ya taifa. Washiriki walipata fursa ya kuuliza maswali na kupata ufafanuzi  kuhusu changamoto mbalimbali zinazowakabili walipakodi, huku wakihimizwa kuendelea kufuata sheria na kutumia huduma za kidijitali zinazotolewa na mamlaka hiyo. TRA imeendelea kusisitiza kuwa elimu ya mlipakodi ni nyenzo muhimu katika kuongeza uelewa wa wananchi, kuboresha hiari ya ulipaji kodi na kuimarisha ushirikiano kati ya mamlaka na walipakodi. Club News Editor

MIAKA 30 YA TRA: TEKNOLOJIA NA HUDUMA BORA ZAIMARISHA UHUSIANO NA WALIPA KODI MKOA WA PWANI

Image
Na Charles Kusaga, Pwani Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika maadhimisho ya miaka 30 tangu kuanzishwa kwake tarehe 01 Julai 1996, imedhihirisha ukuaji wa huduma bora na teknolojia huku ikijivunia hatua kubwa iliyofikiwa katika kuimarisha mahusiano mema na ushirikiano thabiti na walipa kodi mkoa wa Pwani. Akizungumza na wadau mbalimbali wa kodi mkoani hapa katika ufunguzi wa kongamano la maadhimisho ya miaka 30 ya TRA kwa mkoa wa Pwani Menejea wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Ndugu Peter Eliona alizungumzia mafanikio ya Mamlaka ya Mapato nchini.  Kwa mkoa wa Pwani alieleza kuwa katika kipindi hiki cha miongo mitatu, TRA Mkoa wa Pwani imeshuhudia mabadiliko makubwa kutoka katika mifumo ya kizamani ya ukusanyaji mapato na kuingia katika ulimwengu wa kidigitali. Mabadiliko haya ya kiteknolojia yamekuwa nguzo kuu katika kurahisisha utoaji wa huduma na kuondoa urasimu uliokuwa ukiwapa changamoto wafanyabiashara na wananchi mkoani humo. Pia huduma bora, Elimu kwa wateja na ushirikia...

RC MJINI MAGHARIBI AIKARIBISHA HALMASHAURI YA MBEYA KATIKA FURSA ZA UWEKEZAJI ZANZIBAR

Image
Na Mwandishi Wetu,Zanzibar Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Zanzibar, Mhe. Moh’d Ali Abdallah, ameushukuru uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kwa kufanya ziara katika Mkoa huo, akieleza kuwa hatua hiyo inafungua fursa mpya za ushirikiano wa kiuchumi kati ya pande hizo mbili. Akizungumza na viongozi hao, Mhe. Abdallah alisema Mkoa wa Mjini Magharibi uko tayari kuimarisha mahusiano ya kibiashara na Mkoa wa Mbeya, hasa katika sekta ya mazao ya kilimo. "Hii kwetu ni fursa ya kufanya biashara na Mkoa wa Mbeya. Kama mlivyopita katika masoko yetu mmeona viazi na mchele kutoka Mbeya. Karibuni muwekeze Zanzibar, tutawapa eneo maalumu na tutaandika wazi kuwa bidhaa hizo zinatoka Mbeya ili wanaohitaji mazao hayo wajue mahali pa kuyapata kwa bei ya jumla," alisema Mhe. Abdallah. Aliongeza kuwa uwekezaji huo utasaidia kuongeza upatikanaji wa mazao kutoka Mbeya katika masoko ya Mjini Magharibi huku ukiwanufaisha wakulima na wafanyabiashara wa pande zote mbili kupitia masoko ya uhakik...

RC PWANI ATAKA MRADI WA IPOSA UTOE MATOKEO CHANYA KWA VIJANA

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  MKUU wa Mkoa wa Pwani  Abubakar Kunenge, ameielekeza Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima kuhakikisha programu ya Mpango wa IPOSA  inakuwa na matokeo chanya kwa kuwajengea vijana uwezo wa kujiajiri na kuajirika. IPOSA ni Mpango ulioandaliwa na Taasisi ya Elimu ya Watu wazima wa elimu changamani kwa Vijana walio nje ya Shule.  Kunenge ametoa maelekezo hayo wakati akifunga mafunzo ya walimu wa programu hiyo yaliyofanyika Oktoba 2,2025 katika  ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha. Mkuu wa mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge akizungumza na wasimamizi wa mradi wa IPOSA katika mkutano uliofanyika Oktoba 2,2025 katika ukumbi mdogo wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha. Alisema kuwa  elimu inayotolewa kupitia IPOSA haipaswi kubaki kwenye vyeti pekee, bali iwe chachu ya mabadiliko katika maisha ya vijana ambao wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya ajira. “Mradi huu wa IPOSA lazima uwe na matokeo ya kweli, vijana wanapaswa kufundish...

TISEZA YAKARIBISHA WAWEKEZAJI KWALA YATENGA EKARI 100 KWA AJILI YA UWEKEZAJI

Image
  Na Gustaphu Haule, Pwani  MAMLAKA ya Uwekezaji na Maeneo Maalumu ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) imesema imetenga ekari 100 katika eneo la Kwala katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani kwa ajili ya ujenzi wa viwanda. Kaimu Meneja Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma kutoka TISEZA Adelina Rushekya ametoa kauli hiyo Septemba 30,2025 wakati akizungumza na Waandishi wa habari katika mkutano maalum uliofanyika eneo la Kwala. Kaimu meneja Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma kutoka TISEZA Adelina Rushekya akizungumza na Waandishi wa habari katika eneo la Kwala. Rushekya amesema kuwa maeneo ya Kwala yana vivutio vinavyotakiwa kwa ajili ya uwekezaji huku akisema fursa za uwekezaji zipo vizuri katika kila sekta. Rushekya amesema mwekezaji atakayekuwa tayari kuwekeza katika eneo hilo atapatiwa ekari moja na pia anatakiwa kuwa na mtaji wa dola za Kimarekani milioni tano kwa wazawa na kwa raia wa kigeni anatakiwa kuwa na dola milion kumi. Aidha Rushekya amesema kuwa  mwekezaji at...

CCM MKOA WA PWANI YASISITIZA UTULIVU KWA WAGOMBEA UBUNGE NA UDIWANI.

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani kimewataka wagombea wa ubunge na udiwani walioongoza katika mchakato wa kura za maoni kuwa watulivu mpaka hapo utaratibu wa chama utakapokamilika.  Aidha, kimewataka wagombea wa ubunge wa vitimaalum walioongoza kuacha kubweteka na badala yake wapite katika maeneo yao kwa ajili ya kumuombea kura mgombea wa Urais wa CCM Dkt . Samia Suluhu Hassan. Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi ( CCM) Mkoa wa Pwani David Mramba ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na Waandishi wa habari Agosti 14,2025 kwenye ofisi za CCM Mkoa zilizopo katika Manispaa ya Kibaha. Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM )Mkoa Pwani David Mramba akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu mchakato wa kujadili majina ya wagombea ubunge na udiwani wa Mkoa wa Pwani ,kikao hicho kimefanyika Agosti 14,2025 katika ofisi za CCM Mkoa zilizopo katika Manispaa ya Kibaha. Mramba, amesema kuongoza katika uchaguzi wa kura za...

WIZARA YA AFYA YASEMA:UGONJWA WA SIKOSELI SIO WA KUROGWA, YAHAMASISHA JAMII KWENDA KUPIMA VINASABA

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  WIZARA ya afya  Kitengo cha Sikoseli imesema kuwa ugonjwa wa Selimundu (Sickle Cell) sio ugonjwa wa kurogwa kama ambavyo jamii inachukulia lakini  ugonjwa huo ni wakurithi kutoka kwa mzazi mmoja kwenda kwa mzazi mwingine. Imesema ili kujiepusha na ugonjwa huo ni vyema kabla ya kuingia katika mahusiano jamii inapaswa kuchukua hatua ya kwenda kupima vinasaba vya ugonjwa na endapo watakuwa salama wanaweza kuoana na hatimaye kujenga familia salama isiyo na ugonjwa huo wa Selimundu (Sickle Cell). Daktari Bingwa wa magonjwa ya damu kutoka katika hospitali ya Amana iliyopo Jijini Dar es Salaam Jamila Makame, ametoa kauli hiyo katika semina ya siku moja kwa  baadhi ya Waandishi wa Mkoa wa Pwani iliyolenga masuala ya ugonjwa wa Selimundu Semina hiyo iliyofanyika Agosti 12, 2025 katika kituo cha afya Mkoani kilichopo Manispaa ya Kibaha iliwajumuisha baadhi ya Waandishi wa habari ambapo Dr.Makame amesema "Sickle Cell" ni ugonjwa wa kurithi ambao chanzo...