Posts

RC MJINI MAGHARIBI AIKARIBISHA HALMASHAURI YA MBEYA KATIKA FURSA ZA UWEKEZAJI ZANZIBAR

Image
Na Mwandishi Wetu,Zanzibar Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Zanzibar, Mhe. Moh’d Ali Abdallah, ameushukuru uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kwa kufanya ziara katika Mkoa huo, akieleza kuwa hatua hiyo inafungua fursa mpya za ushirikiano wa kiuchumi kati ya pande hizo mbili. Akizungumza na viongozi hao, Mhe. Abdallah alisema Mkoa wa Mjini Magharibi uko tayari kuimarisha mahusiano ya kibiashara na Mkoa wa Mbeya, hasa katika sekta ya mazao ya kilimo. "Hii kwetu ni fursa ya kufanya biashara na Mkoa wa Mbeya. Kama mlivyopita katika masoko yetu mmeona viazi na mchele kutoka Mbeya. Karibuni muwekeze Zanzibar, tutawapa eneo maalumu na tutaandika wazi kuwa bidhaa hizo zinatoka Mbeya ili wanaohitaji mazao hayo wajue mahali pa kuyapata kwa bei ya jumla," alisema Mhe. Abdallah. Aliongeza kuwa uwekezaji huo utasaidia kuongeza upatikanaji wa mazao kutoka Mbeya katika masoko ya Mjini Magharibi huku ukiwanufaisha wakulima na wafanyabiashara wa pande zote mbili kupitia masoko ya uhakik...

RC PWANI ATAKA MRADI WA IPOSA UTOE MATOKEO CHANYA KWA VIJANA

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  MKUU wa Mkoa wa Pwani  Abubakar Kunenge, ameielekeza Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima kuhakikisha programu ya Mpango wa IPOSA  inakuwa na matokeo chanya kwa kuwajengea vijana uwezo wa kujiajiri na kuajirika. IPOSA ni Mpango ulioandaliwa na Taasisi ya Elimu ya Watu wazima wa elimu changamani kwa Vijana walio nje ya Shule.  Kunenge ametoa maelekezo hayo wakati akifunga mafunzo ya walimu wa programu hiyo yaliyofanyika Oktoba 2,2025 katika  ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha. Mkuu wa mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge akizungumza na wasimamizi wa mradi wa IPOSA katika mkutano uliofanyika Oktoba 2,2025 katika ukumbi mdogo wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha. Alisema kuwa  elimu inayotolewa kupitia IPOSA haipaswi kubaki kwenye vyeti pekee, bali iwe chachu ya mabadiliko katika maisha ya vijana ambao wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya ajira. “Mradi huu wa IPOSA lazima uwe na matokeo ya kweli, vijana wanapaswa kufundish...

TISEZA YAKARIBISHA WAWEKEZAJI KWALA YATENGA EKARI 100 KWA AJILI YA UWEKEZAJI

Image
  Na Gustaphu Haule, Pwani  MAMLAKA ya Uwekezaji na Maeneo Maalumu ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) imesema imetenga ekari 100 katika eneo la Kwala katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani kwa ajili ya ujenzi wa viwanda. Kaimu Meneja Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma kutoka TISEZA Adelina Rushekya ametoa kauli hiyo Septemba 30,2025 wakati akizungumza na Waandishi wa habari katika mkutano maalum uliofanyika eneo la Kwala. Kaimu meneja Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma kutoka TISEZA Adelina Rushekya akizungumza na Waandishi wa habari katika eneo la Kwala. Rushekya amesema kuwa maeneo ya Kwala yana vivutio vinavyotakiwa kwa ajili ya uwekezaji huku akisema fursa za uwekezaji zipo vizuri katika kila sekta. Rushekya amesema mwekezaji atakayekuwa tayari kuwekeza katika eneo hilo atapatiwa ekari moja na pia anatakiwa kuwa na mtaji wa dola za Kimarekani milioni tano kwa wazawa na kwa raia wa kigeni anatakiwa kuwa na dola milion kumi. Aidha Rushekya amesema kuwa  mwekezaji at...

CCM MKOA WA PWANI YASISITIZA UTULIVU KWA WAGOMBEA UBUNGE NA UDIWANI.

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani kimewataka wagombea wa ubunge na udiwani walioongoza katika mchakato wa kura za maoni kuwa watulivu mpaka hapo utaratibu wa chama utakapokamilika.  Aidha, kimewataka wagombea wa ubunge wa vitimaalum walioongoza kuacha kubweteka na badala yake wapite katika maeneo yao kwa ajili ya kumuombea kura mgombea wa Urais wa CCM Dkt . Samia Suluhu Hassan. Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi ( CCM) Mkoa wa Pwani David Mramba ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na Waandishi wa habari Agosti 14,2025 kwenye ofisi za CCM Mkoa zilizopo katika Manispaa ya Kibaha. Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM )Mkoa Pwani David Mramba akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu mchakato wa kujadili majina ya wagombea ubunge na udiwani wa Mkoa wa Pwani ,kikao hicho kimefanyika Agosti 14,2025 katika ofisi za CCM Mkoa zilizopo katika Manispaa ya Kibaha. Mramba, amesema kuongoza katika uchaguzi wa kura za...

WIZARA YA AFYA YASEMA:UGONJWA WA SIKOSELI SIO WA KUROGWA, YAHAMASISHA JAMII KWENDA KUPIMA VINASABA

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  WIZARA ya afya  Kitengo cha Sikoseli imesema kuwa ugonjwa wa Selimundu (Sickle Cell) sio ugonjwa wa kurogwa kama ambavyo jamii inachukulia lakini  ugonjwa huo ni wakurithi kutoka kwa mzazi mmoja kwenda kwa mzazi mwingine. Imesema ili kujiepusha na ugonjwa huo ni vyema kabla ya kuingia katika mahusiano jamii inapaswa kuchukua hatua ya kwenda kupima vinasaba vya ugonjwa na endapo watakuwa salama wanaweza kuoana na hatimaye kujenga familia salama isiyo na ugonjwa huo wa Selimundu (Sickle Cell). Daktari Bingwa wa magonjwa ya damu kutoka katika hospitali ya Amana iliyopo Jijini Dar es Salaam Jamila Makame, ametoa kauli hiyo katika semina ya siku moja kwa  baadhi ya Waandishi wa Mkoa wa Pwani iliyolenga masuala ya ugonjwa wa Selimundu Semina hiyo iliyofanyika Agosti 12, 2025 katika kituo cha afya Mkoani kilichopo Manispaa ya Kibaha iliwajumuisha baadhi ya Waandishi wa habari ambapo Dr.Makame amesema "Sickle Cell" ni ugonjwa wa kurithi ambao chanzo...

RAS PWANI KUANZA ZIARA MANISPAA YA KIBAHA AMSIFU DKT .ROGER'S SHEMWELEKWA KWA UKUSANYAJI MAPATO

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani  KATIBU Tawala wa Mkoa wa Pwani Pili Mnyema, ameanza ziara yake ya kikazi katika Halmashauri za Mkoa wa Pwani kwa kutembelea Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha. Katika ziara hiyo, Mnyema amesisitiza umuhimu wa ubunifu katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ili kuongeza mapato ya Halmashauri pamoja na Mkoa kwa ujumla. Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Pili Mnyema katika kikao na watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha alipofanya ziara ya kuzungumza na watumishi wa Manispaa hiyo Agosti 12, 2025 "Naomba tumuunge mkono mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kubuni vyanzo vipya vya mapato na hii ni miongoni mwa maagizo niliyopatiwa ili kusaidia kuongeza mapato ya Mkoa wetu," amesema  Mnyema. Aidha, amempongeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Kibaha Dkt.Rogers Shemwelekwa kwa kuendelea kubuni na kusimamia miradi mbalimbali yenye tija, ambayo imesababisha ongezeko la mapato ya Manispaa hiyo kila mwaka. ...

MWENEZI CCM PWANI AKOLEZA MOTO USIKU WA COREFA,ASIFU MAANDALIZI YAKE

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani CHAMA Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) kimetoa tuzo kwa wachezaji na wadau mbalimbali waliochangia kwa namna au nyingine katika kuendeleza mchezo wa mpira wa Miguu katika msimu wa mwaka 2024/2025. Hafla hiyo imefanyika Agosti 9, 2025 katika ukumbi wa Maisha Plus uliopo karibu na ofisi ya Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani ambapo mgeni rasmi katika hafla hiyo Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Pwani. Katibu Siasa , Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani David Mramba (Kulia)akitoa tuzo kwa mmoja wa wadau wa michezo waliofanya vizuri katika msimu wa mwaka 2023/2024. Katibu Siasa , Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani David Mramba (Kulia)akitoa tuzo kwa mmoja wa wadau wa michezo waliofanya vizuri katika msimu wa mwaka 2023/2024. Zaidi ya wadau 50 walishiriki hafla hiyo wakiwemo  waamuzi wa mpira wa miguu, wachezaji wa mpira wa miguu ,viongozi wa vyama vya miche...