TRA MKOA WA PWANI YATOA ELIMU YA MABADILIKO YA SHERIA ZA KODI 2026


Na. Charles Kusaga, Kibaha - PWANI

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)  imeendesha semina ya elimu kuhusu mabadiliko ya sheria za kodi kwa mwaka 2026, iliyowakutanisha wafanyabiashara, wahasibu, watoa huduma za kodi na wadau mbalimbali katika Ukumbi wa Destiny, Kibaha Mkoa wa PWANI


Lengo la semina hiyo lilikuwa kuwajengea walipakodi uelewa wa mabadiliko ya sheria za kodi, taratibu za ulipaji kodi pamoja na umuhimu wa kuzingatia sheria za kodi ili kuongeza uwajibikaji na kuchangia maendeleo ya taifa.



Washiriki walipata fursa ya kuuliza maswali na kupata ufafanuzi  kuhusu changamoto mbalimbali zinazowakabili walipakodi, huku wakihimizwa kuendelea kufuata sheria na kutumia huduma za kidijitali zinazotolewa na mamlaka hiyo.


TRA imeendelea kusisitiza kuwa elimu ya mlipakodi ni nyenzo muhimu katika kuongeza uelewa wa wananchi, kuboresha hiari ya ulipaji kodi na kuimarisha ushirikiano kati ya mamlaka na walipakodi.



Club News Editor

Comments

Popular posts from this blog

MWENYEKITI KITONGOJI CHA KWAKIBOSHA MAPINGA AWAPIGA MSASA VIJANA 500 KULINDA AMANI YA TAIFA.

WIZARA YA AFYA YASEMA:UGONJWA WA SIKOSELI SIO WA KUROGWA, YAHAMASISHA JAMII KWENDA KUPIMA VINASABA

TAKUKURU PWANI YAOKOA ZAIDI YA SH. MILIONI 385 ZA KIJIJI CHA MSUFINI MKURANGA.