Posts

Showing posts from June, 2026

MIAKA 30 YA TRA: TEKNOLOJIA NA HUDUMA BORA ZAIMARISHA UHUSIANO NA WALIPA KODI MKOA WA PWANI

Image
Na Charles Kusaga, Pwani Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika maadhimisho ya miaka 30 tangu kuanzishwa kwake tarehe 01 Julai 1996, imedhihirisha ukuaji wa huduma bora na teknolojia huku ikijivunia hatua kubwa iliyofikiwa katika kuimarisha mahusiano mema na ushirikiano thabiti na walipa kodi mkoa wa Pwani. Akizungumza na wadau mbalimbali wa kodi mkoani hapa katika ufunguzi wa kongamano la maadhimisho ya miaka 30 ya TRA kwa mkoa wa Pwani Menejea wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Ndugu Peter Eliona alizungumzia mafanikio ya Mamlaka ya Mapato nchini.  Kwa mkoa wa Pwani alieleza kuwa katika kipindi hiki cha miongo mitatu, TRA Mkoa wa Pwani imeshuhudia mabadiliko makubwa kutoka katika mifumo ya kizamani ya ukusanyaji mapato na kuingia katika ulimwengu wa kidigitali. Mabadiliko haya ya kiteknolojia yamekuwa nguzo kuu katika kurahisisha utoaji wa huduma na kuondoa urasimu uliokuwa ukiwapa changamoto wafanyabiashara na wananchi mkoani humo. Pia huduma bora, Elimu kwa wateja na ushirikia...

RC MJINI MAGHARIBI AIKARIBISHA HALMASHAURI YA MBEYA KATIKA FURSA ZA UWEKEZAJI ZANZIBAR

Image
Na Mwandishi Wetu,Zanzibar Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Zanzibar, Mhe. Moh’d Ali Abdallah, ameushukuru uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kwa kufanya ziara katika Mkoa huo, akieleza kuwa hatua hiyo inafungua fursa mpya za ushirikiano wa kiuchumi kati ya pande hizo mbili. Akizungumza na viongozi hao, Mhe. Abdallah alisema Mkoa wa Mjini Magharibi uko tayari kuimarisha mahusiano ya kibiashara na Mkoa wa Mbeya, hasa katika sekta ya mazao ya kilimo. "Hii kwetu ni fursa ya kufanya biashara na Mkoa wa Mbeya. Kama mlivyopita katika masoko yetu mmeona viazi na mchele kutoka Mbeya. Karibuni muwekeze Zanzibar, tutawapa eneo maalumu na tutaandika wazi kuwa bidhaa hizo zinatoka Mbeya ili wanaohitaji mazao hayo wajue mahali pa kuyapata kwa bei ya jumla," alisema Mhe. Abdallah. Aliongeza kuwa uwekezaji huo utasaidia kuongeza upatikanaji wa mazao kutoka Mbeya katika masoko ya Mjini Magharibi huku ukiwanufaisha wakulima na wafanyabiashara wa pande zote mbili kupitia masoko ya uhakik...