AWESO AKEMEA MATUMIZI MABAYA FEDHA ZA MAJI

  • Aonya, vipo vya kuchezea ukishiba chezea kidefu au kitambi chako sio fedha za miradi ya maji  

  
Waziri wa maji Juma Aweso akizungumza na wananchi (hawapo pichani )Kata ya Chumbi Wilayani Rufiji Mkoani Pwani.

Na. Julieth Ngarabali. Rufiji

 Waziri wa Maji Juma Aweso  amezindua skimu ya maji inayohudumia zaidi wananchi 8,000 katika kata ya Chumbi Wilayani Rufiji na kuielekeza jumuia ya watumiaji huduma hiyo kuhakikisha pesa walizokubaliana zinakusanywa na kupelekwa benki kwenye akaunti . 

 Aweso ametoa maelekezo hayo wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Chumbi Rufiji Mkoani Pwani  na kusisitiza kuwa vipo vya kuchezea na sio pesa za miradi ya maji 

‘’ Tunajua mmeweka pesa ambayo mmekubaliana unapotaka kuchota maji lazima uchangie ,niwasihi jumuia iayosimamia hili fedha inapokusanywa ipelekwe benki kwenye akaunti  na nataka niwaambie vipo vya kuchezea ukishiba chezea kidefu chako au kitambi chako sio fedha za miradi ya maji tutashughulikiana’’ amesema  na kuongeza 

‘’Watu wametesema kwa muda mrefu sana wakitafuta hii huduma ya maji ambayo leo hii imepatikana  hapa Chumbi kwa iyo tunapojenga mradi wa maji maana yake lazima wananchi  wafurahie matunda na kazi nzuri inayofanywa na Mbunge, Rais, madiwani na wenyeviti hivyo niwasihi sana kuulinda na kuutunza kwa faida ya vizazi vya sasa na vijavyo’’ ameongeza

 Akijibu ombi maalumu  lililotolewa na Kaimu mkuu wa Wilaya ya Rufiji ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Mkuranga Hadija Nasri ya uhitaji ya huduma ya maji katika kitongoji cha Nyakipande Aweso amemuagiza Meneja wa wakala wa maji safi na mazingira vijijini (RUWASA ) Pwani  Beatrice Kasimbazi kuhakisha wanapeleka huduma hiyo kwenye eneo hilo

Awali Mkuu wa Mkoa Abubakar Kunenge  akitoa salamu amemshukuru Rais  Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya  kwani mradi huu ni matokeo ya jitihada zake.

“’ Maji ni uhai  na pia maji ni ibada huu  mradi ni kielelezo cha miradi  mingi inayotelezwa na Rais katika Mkoa wa Pwani na  Nchi nzima kwa hiyo niamshukuru sana kwa niaba ya watu wa Rufiji na Pwani kiujumla”’ amesema Kunenge

 Naye Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi  (CCM ) Wilaya Rufiji Kaswakala Mbonde  amesema kuwa wao chama wanafuraha kuwa utekeleaji skimu hiyo ni utekelezaji  Ilani ya  uchaguzi  ya chama hicho Ibara ya 97 na kuwapongeza  wananchi waliopisha chanzo cha maji ili mradi huo utekelezeke.

Baadhi ya wananchi  wa Chumbi wamesema wamefarijika kupata huduma hiyo kwa sababu awali walikua wanatembea umbali mrefu wa zaidi ya kilomita nne kufaya maji kwenye mabwaya ambayo hata hivyo hayakua salama kwa afya zao  

Aidha mwa mujibu wa taarifa ya RUWASA Rufiji ni kwamba ujenzi wa mradi huo wa maji umegharimu sh. 722.3 milioni fedha za mfuko wa maji ( NWF)  chini ya usimamizi wa wakala wa maji safi na mazingira vijijini na kwamba umekwishaanza kutoa huduma kwa jamii  katika vijiji vitatu vya Chumbi A,B na C

Taarifa hiyo imeeleza kuwa  mradi huo uliibuliwa na wananchi wenyewe mwaka 2020  na kuanzishwa kwa lengo la kusogeza na kungezeka kiwango cha upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama na ya kutosheleza kwa jamii wa kata ya Chumbi hivyo kusaidia kupunguza magonjwa yanayosababishwa na ukosefu wa maji safi na salama

Lengo jingine ni kuwapunguzia adha ya kufuata maji  kwa umbali mrefu na kusababisha kutumia muda mwingi kutafuta maji hali ambayo inapelekea  pia kushindwa kujishughulisha na shughuli zinguine za kiuchumi.

Wananchi wa  vijiji vitatu vya Chumbi A,B na C Wilayani Rufiji Mkoani Pwani wakiwa kwenye mkutano wa uzinduzi wa mradi wao mkubwa wa maji safi Kijiji humo 



 

 

 





Club News Editor

Comments

Popular posts from this blog

RC PWANI AONGOZA WAKAZI PWANI KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA

BARAZA LA MADIWANI KIBAHA MJINI LAMPONGEZA MKURUGENZI WAKE KWA KAZI NZURI ANAYOIFANYA SAMBAMBA NA KUONGEZA MAPATO.

RAIS SAMIA ATANGAZA KIBAHA MJINI KUWA MANISAPAA,MBUNGE KOKA AFURAHIA ASEMA KIBAHA ITANG'AA