NOTI BANDIA ZA ZAIDI YA MIL.13 ZADAKWA PWANI

    Noti za pesa  bandia zilizokamatwa Pwani 
  • Baadhi zilishaingia kwenye mzunguko wa matumizi Msata  
Mwandishi wetu.

Pwani.WATU wanne wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Pwani  kwa tuhuma za kukutwa na noti za  pesa bandia za thamani ya zaidi ya sh. 13  milioni pamoja na mtambo  wa kutengeneza pesa hizo.

Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani Pius  Lutumo amesema  kukamatwa kwa watu hao  waliokutwa na pesa  sh.1,550,000 milioni  kulitokana na baadhi yao kutiliwa shaka baada ya kufanya malipo ya kukodisha chumba kwenye moja ya nyumba ya kulala wageni   huko Masata Mkoani humo.

Amewataja watuhumiwa hao ni Mbaraka Fundi (48)Zena Naringa (42)wakazi wa Buza Jijini Daresalaam wengine  ni  Masumuko Kiyogoma (54) Mkazi wa Goba na Elius  Wandiba (50) mkazi wa kimara Suka Jijini Dar esalaam.

''Kukamatwa kwa watuhumiwa hao kulitokana na taarifa za raia mwema aliyetilia  mashaka  noti ya sh.10,000 aliyopokea kama malipo ya huduma katika nyumba ya kulala wageni  huko Msata na tulipata taarifa hiyo kisha kuwakamata na  baada ya mahijiano tulifanikiwa kuwabaini washirika wenzao waishio huko Daresalaa"amesema Lutumo
       Kamanda wa Polisi Pwani Pius Lutumo akielezea  walivyoakamata  fedha hizo.

 Nakuongeza"Tulipopekua kwenye makazi yao tuliwakuta na pesa za noti bandia sh.12,000,000 na mashine ya kutengenezea pesa bandia pamoja na malighafi zake'amesema

 Lutumo amewataka wakazi Mkoani humo kuchunguza kwa makini pesa wanazopokea kutoka kwa wateja wao kwaajili ya malipo mbalimbali na pindi wanapotilia mashaka wasisite kutoa taarifa kwa vyombo vya sheria ili hatua za uchunguzi zichukuliwe.

Baadhi ya wananchi  Mjini Kibaha wamesema  utambuzi wa noti bandia kwao ni changamoto kwa sababu sio rahisi kutambua machoni kwa haraka na hivyo wameomba Serikali kutoa elimu  zaidi ili iwe rahisi kwao kutambua wanapokuta nazo kwenye maeneo ya biashara




 










Club News Editor, Julieth Ngarabali

Comments

Popular posts from this blog

RC PWANI AONGOZA WAKAZI PWANI KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA

BARAZA LA MADIWANI KIBAHA MJINI LAMPONGEZA MKURUGENZI WAKE KWA KAZI NZURI ANAYOIFANYA SAMBAMBA NA KUONGEZA MAPATO.

RAIS SAMIA ATANGAZA KIBAHA MJINI KUWA MANISAPAA,MBUNGE KOKA AFURAHIA ASEMA KIBAHA ITANG'AA