Posts

Showing posts from February, 2024

DK .TINDWA AMWAGA SIMU JANJA CCM MKURANGA

Image
   Mjumbe wa kamati ya Uchumi ya Jumuiya ya Wazazi Taifa ambaye ni mjumbe wa kamati ya Siasa ya Mkoa wa Pwani Dk. Chakou Tindwa(kushoto)akimkabidhi mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Pwani Mwinshehe Mlao(Kulia) simu 26 zenye thamani ya Sh.milioni 6.5 Kwa ajili ya kusajilia wanachama kieletroniki. Na Gustafu Haule,Pwani MJUMBE wa Kamati  ya Uchumi ya Jumuiya ya Wazazi Taifa Dk.Chakou Tindwa ameendelea na jitihada za kukiimarisha Chama Cha Mapinduzi(CCM) ambapo kwa sasa ameipiga tafu CCM kwa kutoa simu janja 26 zenye thamani ya Sh.milioni 6.5 zitakazotumika kusajili wanachama waliopo Wilayani Mkuranga. Dk.Chakou ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Pwani mbali na kusaidia simu hizo lakini pia  amekabidhi kadi za CCM 12,500 kwa ajili ya kuwagawia wanachama waliopo Wilayani humo. Hatua ya Dk Chakou kutoa simu na kadi hizo ni sehemu ya utekelezaji wa aadi zake alizozitoa kwa kamati ya Siasa ya Wilayani Mkuranga siku chache zilizopita. Akikabidhi simu na kadi hizo kwa...

RC PWANI AHAMASISHA KUPELEKA WATOTO KUPATA CHANJO YA SURUA NA RUBELLA.

Image
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge (katikati) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kampeni ya chanjo ya Surua na Rubella iliyoanza kufanyika Februari 15 mwaka huu ,Kushoto ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani Benedicto Ngaiza na Kulia ni mratibu wa mpango wa chanjo  Taifa kutoka Wizara ya afya Geogina Ngaiza. Na Gustafu Haule,Pwani MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge,amesema kuwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano 174,298 wamelengwa kufikiwa kwa ajili ya kupata chanjo ya Surua - Rubella inayotolewa katika maeneo mbalimbali. Kunenge, amesema kuwa kampeni ya chanjo hiyo tayari imeanza Februari 15 mwaka huu na itamalizika Februari 18 na kwamba kwa Mkoa wa Pwani chanjo hiyo inapatikana katika ngazi ya vituo vya huduma ya afya,ngazi ya kaya kupitia huduma ya mKoba  pamoja na maeneo mengine yaliyoainiashwa. Kunenge,ametoa kauli hiyo Februari 16 mwaka huu wakati akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano maalum wa kuhamasisha kampeni ya masuala ya chanjo ya Surua n...

UCHAPAKAZI WA LOWASSA HAUWEZI KUBISHANIWA; NCHIMBI

Image
Na Mwandishi wetu. Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Balozi Emmanuel Nchimbi, amesema watu wanaweza kupishana katika maelezo ya kumwelezea Hayati Edward Ngoyai Lowassa katika mambo mbalimbali, lakini jambo moja ambalo haliwezi kubishaniwa ni jinsi alivyokuwa mchakapakazi wa kweli, katika nafasi zake zote alizowahi kuwa nazo, katika kuwatumikia Watanzania wote.  Dkt. Balozi Nchimbi amesema kupitia uhodari wake wa kuchapa kazi katika kutimiza wajibu wake kwa nchi, Hayati Lowassa alikuwa kiongozi mwenye uthubutu na uwezo wa kufanya maamuzi magumu kwa ajili ya kutafuta ufanisi na kupata matokeo chanya ya haraka kwa ajili ya maendeleo ya watu.  Dkt. Balozi Nchimbi amesema hayo Februari 16, 2024 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, baada ya kufika kuwapatia pole wafiwa, kusaini kitabu cha maombolezo na kutoa heshima za mwisho, nyumbani kwa Hayati Lowassa, katika Kijiji cha Ngarash, wilayani Monduli Mkoa wa Arusha, akiongeza kuwa kutokana na sifa za kiuongozi al...

BAADHI YA ASASI CHANZO CHA KUKWAMISHA UFANISI WA PROGRAM YA MALEZI.MAKUZI NA MAENDELEO YA AWALI YA MTOTO

Image
        Ni kwa kuwakwepa maafisa maendeleo ya jamii        Baadhi zaanza kuchukuliwa hatua. Serikali yaonya    Julieth Ngarabali, Pwani. Moja ya wadau wakubwa katika utekelezaji wa program jumuishi ya Taifa ya malezi,makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto ni maafisa ustawi wa jamii ambao hufanya kazi kwa niaba ya Serikali katika kusimamia utekelezaji wa Pogram hii ambayo Serikali imetoa maelekezo ya utekelezaji wake kusambaa maeneo yote nchini ifikapo mwezi wa nne mwaka huu. Katika mkutano wa mwaka uliofanyika mwezi Disemba mwaka 2023 na kuwakutanisha wadau wote kutoka Serikalini, asasi za kiraia pamoja na waandishi wa habari,msukumo mkubwa ulikuwa kutengeneza muunganiko wa pamoja kati ya wadau muhimun ili elimu juu ya malezi,makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto kuanzia umri wa miaka 0-8 iweze kuifikia jamii na kuelewa huku kilio kikubwa kikitajwa kwa baadhi ya wadau kutoshiriki kikamilifu ama kukwepa kufuata taratibu kama zilivyoa...

DK, TINDWA AKUSANYA MIL 10.8 UJENZI OFISI YA CCM MKURAGA

Image
Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Pwani Dr.Chakou Tindwa (kulia ) akikabidhi fedha taslimu Sh.milioni tano kwa mmoja wa viongozi wa Kata ya Shungubweni kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya CCM ya Kata hiyo. Ni katika harambee ya kuchangia ujenzi wa ofisi ya Kata CCM Shungubweni Na Gustafu Haule,Pwani MJUMBE wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Pwani Dr.Chakou Tindwa,ameendesha harambee ya kuchangia ujenzi wa ofisi ya CCM Kata ya Shungubweni iliyopo Wilayani Mkuranga na kufanikiwa kukusanya Sh.milioni 10.8. Dr .Tindwa ameendesha harambee hiyo Februari 11 mwaka huu kwa kushirikiana na viongozi mbalimbali wa Halmashauri Kuu ya CCM Kata ya Shungubweni,huku ikihudhuriwa na viongozi wa Chama na Jumuiya kutoka Wilaya na Mkoa. Kuwepo kwa Dr.Tindwa katika harambee hiyo kulitoa hamasa  kwa WanaCCM na viongozi wengine kujitokeza na kumuunga mkono Dr.Tindwa ili kuhakikisha malengo ya ujenzi wa ofisi hiyo yanatimia Dr.Tindwa mbali na kuendesha harambe hiyo lakini nae alichangia fedha taslimu Sh. milioni 5 na ...

KIPANDE CHA VUMBI CHA BARABARA CHASABABISHA AJALI MSAFARA WA MAKONDA

Image
  Magari zaidi ya 10 yagongana wakati msafara wa Makonda ukirejea Dar esalaam kujumuika na wananchi katika maombolezo ya kifo cha Lowassa Na.Mwandishi wetu, Mtwara  Zaidi ya magari 10 yaliyokua kwenye msafara wa Katibu wa itikadi, uenezi na mafunzo wa chama cha Mapinduzi CCM Taifa , Paul Makonda yamegongana leo katika kijiji cha Sululu Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara. Ajali hiyo imetoka leo Februari 11 majira ya saa nane mchana katika eneo hilo wakati msafara huo ukitokea Mkoani Ruvuma kuelekea Dar salaam. Kwa mujibu wa taarifa za awali kutoka kwa wakazi wa eneo hilo wamesema ajali hiyo imetokana na vumbi na mwendo mkasi wa magari hayo ya msafara ambapo ilipofika kijijini hapo kwenye kipande cha barabara ya vumbi moja ya gari ilipunguza mwendo kutokana na vumbi kubwa na zito kwenye kipande cha barabara hali ambayo  inaaminika ilisababisha mengine yaliyokua nyuma kugongana na kuparamiana kwa nyuma. “ mimi na mdogo wangu tulikua tunasubiri kumuona Paul Makonda tumpun...

RATIBA RASMI MAZISHI YA HAYATI LOWASSA KUTOLEWA JUMANNE

Image
Na Mwandishi wetu. Ratiba rasmi ya mazishi  ya Waziri Mkuu mstaafu  Edward Lowassa yanatarajiwa kutolewa Februari 13/2024 . Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Februari 11 na  msemaji binafsi wa Lowassa , Aboubakar Liongo  nyumbani kwa marehemu Masaki  jijini Dar esalam ni kwamba  ratiba hiyo itahusisha pia taratibu zote za kiserikali. “Taarifa zaidi kuhusiana na tukio zima la mazishi zitatolewa baadae’’ amesema. Hata hivyo mwili wa Lowassa unatarajiwa kuzikwa  Februari 17/2024 katia kijiji cha  Ngarash Wilayani Monduli  mkoani Arusha . Lowassa amefarikia dunia Februari 10/2024 saa nane mchana jijini Dare salaam ambapo alikua akipatiwa matibabu katika taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Taarifa za kifo chake ilitolewa jana na makamu wa Rais, Dk. Philip Mpango. Lowassa ambaye hadi anafariki dunia alikua na umri wa miaka 70 alikua akipatiwa matibabu JKCI ya magonjwa ya kujikunja utumbo,shinikizo la damu pamoja na matatizo y...

HIKI NDICHO KILICHOMUUA EDWARD LOWASSA

Image
                Edward Lowassa enzi za uhai wake Makamu wa Rais  Dk. Philip Mpango atangaza  kifo chake kwa niaba ya Rais  Samia Suluhu Hassan  ·       Lowassa amefariki baada ya kuugua magonjwa ya kujikunja utumbo, matatizo ya mapafu na shinikizo la damu.    Na mwandishi wetu. Makamu wa Rais wa Tanzania Dk. Philip Mpango  ametangaza kifo cha Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa aliyefariki leo saa nane mchana katika taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Dar esalam Februari 10 , 2024 Makamu wa Rais ametoa tarifa hiyo kwa niaba ya Rais  Samia Suluhu Hassan kupitia Televisheni ya shirika la utangazaji la Taifa (TBC) ambapo pia  ametangaza maradhi yaliyokua yanamsumbua na kumsababishia kifo. Kupitia taarifa hiyo, amesema Lowassa amefariki baada ya kuugua magonjwa ya kujikunja utumbo , matatizo ya mapafu  pamoja na shinikizo la damu , Amebainisha kuwa hayati Ed war...

DAKTARI BINGWA WA SARATANI ATETA NA VIONGOZI WA DINI PWANI

Image
Dr Chakou Tindwa akizungumza katika kongamano la Jumuiya  ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT) huko Mkuranga  Pwani. Na Gustaphu Haule MJUMBE wa kamati ya Siasa Mkoa wa Pwani Dr. Chakou Tindwa,amewashauri viongozi mbalimbali kuwa waadilifu ili kulinda amani iliyopo kwani kufanya hivyo itakuwa njia sahihi ya kumuenzi Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan anayefanyakazi huku akiwaheshimu wananchi wake. Tindwa ambaye pia ni daktari bingwa wa magonjwa ya saratani hapa nchini na mdau wa maendeleo anayesaidia masuala ya kijamii ametoa ushauri huo  katika kongamano la Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT)lililofanyika Februari 07 Wilayani Mkuranga. Dr.Tindwa, amesema kuwa uadilifu mara nyingi unaambatana na kutii mamlaka iliyopo na kwamba bila kutii mamlaka ni Wazi kuwa hakuna uadilifu jambo ambalo linaweza kusababisha kuvunjika kwa amani. Aidha,katika kongamano hilo ambalo Tindwa alikuwa mgeni rasmi amewasisitiza washiriki hao kuzingatia mambo makuu matatu ikiwemo kuwaheshimu...

TAZAMA YANAYOJIRI CCM TAIFA JIJINI DODOMA

Image
Na. Mwandishi wetu.Dodoma. B aadhi yaWatumishi wa chama cha Mapinduzi (CCM) Makao Makuu, pamoja na jumuiya zake, Umoja wa Wazazi, Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), wakimsikikiza na kufuatilia kwa makini hotuba ya Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, wakati wa kikao na watumishi hao, katika Ukumbi wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), jijini Dodoma, B aadhi ya Watumishi wa chama cha Mapinduzi (CCM) Makao Makuu, pamoja na jumuiya zake, Umoja wa Wazazi, Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), wakimsikikiza na kufuatilia kwa makini hotuba ya Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, wakati wa kikao na watumishi hao, katika Ukumbi wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), jijini Dodoma, KURASA ZA PICHA MBALIMBALI ZA MATUKIO YANAYOENDELEA KWENYE MKUTANO WA JUMUIYA ZA CHAMA CHA MAPINDUZI  HUKO DODOMA  TANZANIA Katibu Mkuu wa chama cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, akizungumza na watumi...

MAGUMU ALIYOPITIA MSICHANA KINARA TUMBI SEKONDARI

Image
  Magumu ya kwenye familia yalimpeleka kusikojulikana lakini shuleni anaonekana Happness Fredy mmoja wa wasichana 34 waliofaulu mtihani wa kidato cha nne 2023 shule ya Sekondari Tumbi . Na Gustaphu Haule FEBRUARI 3 ,2024 nimekutana na msichana Happness Fredy ambaye ndiye kinara wa ufaulu wa  matokeo ya mtihani wa kidato cha nne katika shule ya Sekondari Tumbi . Happness katika matokeo ya mtihani huo amefanikiwa kupata ufaulu wa daraja la kwanza pointi saba matokeo ambayo yameifanya shule ya Sekondari Tumbi kushika nafasi ya pili kimkoa. Katika mazungumzo yetu ya awali Happness ameanza kwa kusema,"Shule za Kata zimekuja kuwakomboa wanafunzi wanaotoka katika familia duni na kwamba wanaobeza shule hizo ni wazi kuwa hawana wanalolijua,"  Happness ambaye ni mtoto wa pili wa mzee Fredy Godfrey anasema bila kuwepo kwa shule za Kata uenda leo hii angekuwa tayari ameshaolewa na kuitwa mama. Happness (18)mkazi wa Mtaa wa  Tanita, Kata ya Kibaha Halmashauri ya Mji Kibaha alicha...