HIKI NDICHO KILICHOMUUA EDWARD LOWASSA
· Lowassa
amefariki baada ya kuugua magonjwa ya kujikunja utumbo, matatizo ya mapafu na
shinikizo la damu.
Na mwandishi wetu.
Makamu wa Rais wa Tanzania Dk. Philip Mpango ametangaza kifo cha Waziri Mkuu wa zamani
Edward Lowassa aliyefariki leo saa nane mchana katika taasisi ya Moyo ya Jakaya
Kikwete (JKCI) Dar esalam Februari 10 , 2024
Makamu wa Rais ametoa tarifa hiyo kwa niaba ya
Rais Samia Suluhu Hassan kupitia
Televisheni ya shirika la utangazaji la Taifa (TBC) ambapo pia ametangaza maradhi yaliyokua yanamsumbua na kumsababishia kifo.
Kupitia taarifa hiyo, amesema Lowassa amefariki
baada ya kuugua magonjwa ya kujikunja utumbo , matatizo ya mapafu pamoja na shinikizo la damu ,
Amebainisha kuwa hayati Ed
“kutokana na kifo hicho Rais Samia ametoa pole
kwa ndugu, jamaa na marafiki na pia
ametangaza siku tano za maombelezo ambapo bendera zitapepea nusu mlingoti
kuanzia Februari 10 ,2024 na kwamba
taarifa zaidi kuhusu msiba huu zitaendelea kutolewa na Serikali.
Hayati Edward Lowassa amezaliwa Agosti 26,1953 katika kijiji cha Ngarash Monduli na kwamba katika familia ya mzee Ngoyai Lowassa yeye ndiye alikua mtoto mkubwa wa kiume.
Comments
Post a Comment