RATIBA RASMI MAZISHI YA HAYATI LOWASSA KUTOLEWA JUMANNE


Na Mwandishi wetu.

Ratiba rasmi ya mazishi  ya Waziri Mkuu mstaafu  Edward Lowassa yanatarajiwa kutolewa Februari 13/2024 .

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Februari 11 na  msemaji binafsi wa Lowassa , Aboubakar Liongo  nyumbani kwa marehemu Masaki  jijini Dar esalam ni kwamba  ratiba hiyo itahusisha pia taratibu zote za kiserikali.

“Taarifa zaidi kuhusiana na tukio zima la mazishi zitatolewa baadae’’ amesema.

Hata hivyo mwili wa Lowassa unatarajiwa kuzikwa  Februari 17/2024 katia kijiji cha  Ngarash Wilayani Monduli  mkoani Arusha .

Lowassa amefarikia dunia Februari 10/2024 saa nane mchana jijini Dare salaam ambapo alikua akipatiwa matibabu katika taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)

Taarifa za kifo chake ilitolewa jana na makamu wa Rais, Dk. Philip Mpango.

Lowassa ambaye hadi anafariki dunia alikua na umri wa miaka 70 alikua akipatiwa matibabu JKCI ya magonjwa ya kujikunja utumbo,shinikizo la damu pamoja na matatizo ya mapafu.

“ Hayati Lowassa alikua akipatiwa matibabu JKCI tangu tarehe 14/1/2022 na baadae alipelekwa Afrika kusini kwa matibabu zaidi na baadae kurejea nchini “ amesema Dk. Mpango alipokua akitangaza tukio la msiba huo.

Ameogeza kuwa akiwa nchini Afrika kusini , Lowassa alitembelewa na Waziri Mkuu Kassim Mjaliwa Desemba 28/2022 na kuwasilisha salamu za Rais, Samia Suluhu Hassan,

 

 







Club News Editor Julieth Ngarabali

Comments

Popular posts from this blog

RC PWANI AONGOZA WAKAZI PWANI KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA

BARAZA LA MADIWANI KIBAHA MJINI LAMPONGEZA MKURUGENZI WAKE KWA KAZI NZURI ANAYOIFANYA SAMBAMBA NA KUONGEZA MAPATO.

RAIS SAMIA ATANGAZA KIBAHA MJINI KUWA MANISAPAA,MBUNGE KOKA AFURAHIA ASEMA KIBAHA ITANG'AA