KIPANDE CHA VUMBI CHA BARABARA CHASABABISHA AJALI MSAFARA WA MAKONDA



  •  Magari zaidi ya 10 yagongana wakati msafara wa Makonda ukirejea Dar esalaam kujumuika na wananchi katika maombolezo ya kifo cha Lowassa

Na.Mwandishi wetu, Mtwara

 Zaidi ya magari 10 yaliyokua kwenye msafara wa Katibu wa itikadi, uenezi na mafunzo wa chama cha Mapinduzi CCM Taifa , Paul Makonda yamegongana leo katika kijiji cha Sululu Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara.

Ajali hiyo imetoka leo Februari 11 majira ya saa nane mchana katika eneo hilo wakati msafara huo ukitokea Mkoani Ruvuma kuelekea Dar salaam.

Kwa mujibu wa taarifa za awali kutoka kwa wakazi wa eneo hilo wamesema ajali hiyo imetokana na vumbi na mwendo mkasi wa magari hayo ya msafara ambapo ilipofika kijijini hapo kwenye kipande cha barabara ya vumbi moja ya gari ilipunguza mwendo kutokana na vumbi kubwa na zito kwenye kipande cha barabara hali ambayo  inaaminika ilisababisha mengine yaliyokua nyuma kugongana na kuparamiana kwa nyuma.

“ mimi na mdogo wangu tulikua tunasubiri kumuona Paul Makonda tumpungie mkono lakini kutokana na vumbi la barabarani eneo tulipokuwa tulishindwa hivyo tukakaa pembeni kabisa na ghafla baada ya magari kupita tukasikia kishindo cha magari kugongana na baada ya dakika kadhaa tukabaini ni yale ya msafara”’ amesema Bakari Musa

Kamanda wa Polisi Mkoani  humo Nicodemus Katembo alipopigiwa simu amesema anafatilia tukio hilo na atatoa taarifa baadae.

Msafara huo wa Makonda ulikua unarejea jijini Dar esalaam ukitokea Songea baada ya mapema leo asubuhi kutangaza  chama hicho kusitisha ziara ya kiongozi huo katika mikoa ya Mtwara na Lindi iliyokua imebaki katia ya 20 iliyolengwa na ziara hiyo.

Sababu kuu ya kusitishwa kwa ziara hiyo  leo ni kutokana na kifo cha Waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa iliyotokea Februari 10 ambapo CCM inaungana na waTanzania katia maombolezo



 

 











Club News Editor Julieh Ngarabali

Comments

Popular posts from this blog

RC PWANI AONGOZA WAKAZI PWANI KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA

BARAZA LA MADIWANI KIBAHA MJINI LAMPONGEZA MKURUGENZI WAKE KWA KAZI NZURI ANAYOIFANYA SAMBAMBA NA KUONGEZA MAPATO.

RAIS SAMIA ATANGAZA KIBAHA MJINI KUWA MANISAPAA,MBUNGE KOKA AFURAHIA ASEMA KIBAHA ITANG'AA