Posts

Showing posts from February, 2025

WAKILI MKOLWE-WANAFUNZI TOENI TAARIFA ZA UKATILI WA KINGONO ,ASEMA KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA YA MAMA SAMIA IMEKUJA KUWAKOMBOA

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  MRATIBU wa Kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia ( Mama Samia Legal Aid Campaign) katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Vijijini Egidy Mkolwe, amewataka wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kilangalanga kuhakikisha wanatoa taarifa zinazoashiria ukatili wa Kingono. Mkolwe ambaye pia ni Wakili wa Serikali kutoka ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali ametoa wito huo wakati alipotembelea shuleni hapo akiambatana na timu ya wataalam mbalimbali katika utekelezaji wa kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia iliyoanza kufanyika leo Februari 25 katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Pwani. Mratibu wa Kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia katika Halmashauri ya Kibaha Vijijini Egidy Mkolwe alitoa elimu kuhusu masuala ya ukatili wa Kingono kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kilangalanga ikiwa ni sehemu ya kampeni hiyo iliyoanza Februari 25 mwaka huu  Mkolwe, amewaambia wanafunzi hao kuwa zipo tabia na vitendo viovu vinavyoashiria ukatili wa Kingono ambavyo hu...

RC PWANI AZINDUA KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA YA MAMA SAMIA, SHEKHE WA MKOA AOMBA VYETI VYA NDOA YA KIISLAMU VITAMBULIKE KISHERIA.

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani SHEKHE Mkuu wa Mkoa wa Pwani Hamis Mtupa ameiomba Serikali kuvitambua kisheria vyeti vya ndoa vinavyotolewa na dini ya kiislamu ili kuondoa usumbufu uliopo sasa. Mtupa amewasilisha ombi hilo Februari 24 Mjini Kibaha wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya msaada wa Kisheria ya mama Samia (Mama Samia Legal Aid Campaign) uliofanyika katika viwanja vya stendi ya zamani Mailimoja Kibaha Pwani. Akizungumza katika hafla hiyo Mtupa amesema wamekuwa wakitoa hati halali za ndoa lakini waumini wa dini hiyo wakizipeleka Serikalini wanaambiwa hazitambuliki na hivyo kuleta usumbufu katika jamii. " Tunaomba Serikali ifanyie maboresho vyeti vinavyotolewa kwa wanandoa wa kiislamu, wakivipeleka Serikalini wanaambiwa vinatakiwa vya ndoa za Serikali wakati hawakufungia ndoa zao huko,naomba hili liangaliwe," amesema Akizindua kampeni hiyo Mkuu wa Mkoa wa Pwani  Abubakar Kunenge amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kupata Msaada wa Kisheria wa migogoro mbalimbali hu...

DOGO MABROUK AONGOZA SAMIA MARATHON KIBAHA VIJIJINI, ATOA UJUMBE KWA WANANCHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA MWISHONI MWAKA HUU

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  MAKAMU mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa Dogo Mabrouk ameongoza mbio za Samia Marathon iliyofanyika leo Februari 22,2025 katika viwanja vya Shule ya Msingi Mtongani Mlandizi Kibaha Vijijini. Mabrouk, ameongoza mbio hizo akimwakilisha Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambaye ndiye alipaswa kuwa mgeni rasmi katika kuongoza mbio hizo. Makamu mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa Dogo Mabrouk akizungumza na Wananchi, viongozi wa chama na Serikali pamoja na WanaCCM kiujumla katika mkutano uliofanyika viwanja vya Shule ya Msingi Mtongani Mlandizi Kibaha Vijijini sehemu ambayo ilifanyika Samia Marathon chini ya maandalizi ya Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Pwani. Mabrouk, katika mbio hizo aliongozana na viongozi wa chama na Serikali akiwemo Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Hamoud Jumaa ( MNEC) ambaye ni mkazi wa Mji wa Mlandizi, mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Pwani,Mwishehe Mlao,Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kun...

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA KUONGOZA SAMIA MARATHON KIBAHA VIJIJINI, JACKSON KITUKA ASEMA NI MARATHON YA KIHISTORIA KUFANYIKA PWANI

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa anatarajia kuwa mgeni rasmi katika kuongoza  mbio za polepole "Samia Marathon "zitakazofanyika Februari 22 mwaka huu Mlandizi Kibaha Vijijini Mkoa wa Pwani. Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Pwani Josian Kituka, amewaambia Waandishi wa habari leo Februari 20 katika mkutano uliofanyika kwenye ofisi za Chama Cha Mapinduzi (CCM )Mkoa wa Pwani zilizopo Kibaha Mjini. Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani Josian Kituka akizungumza na Waandishi wa habari leo Februari 20 ofisini kwake kuhusu Samia Marathon inayotarajia kufanyika Februari 22 mwaka huu Mlandizi Kibaha Vijijini   Kituka, amesema kuwa maandalizi ya mbio za Samia Marathon yamekamilika huku malengo yake ni kuhamasisha Wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa 2025. Amesema kuwa, wameamua kutumia jina la Samia kwa ajili ya kumpa heshima Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ambaye amefanyakazi kubwa ya maendeleo kat...

WAANDISHI WA HABARI PWANI WAJENGEWA UWEZO KUANDIKA HABARI ZA MALEZI, MAKUZI NA MAENDELEO YA AWALI YA MTOTO

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani BAADHI ya Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Pwani wamepewa mafunzo ya kujengewa uwezo kuhusu kuandika habari za Malezi,Makuzi na Maendeleo ya awali ya mtoto. Mafunzo hayo yametolewa na Shirika lisilokuwa la Kiserikali la Anjita (ANJITA CHILD DEVELOPMENT FOUNDATION)  kwa kushirikiana na Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa Pwani (CRPC)  chini ya ufadhili wa Taasisi ya TECDEN (TANZANIA EARLY CHILDHOOD DEVELOPMENT NETWORK)  yaliyofanyika Februari 12 Mjini Kibaha. Akizungumza wakati akifungua mafunzo hayo Mkuu wa Kitengo cha mawasiliano Serikalini kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani Zablon Bugingo ameishukuru taasisi ya Anjita kwa kuona umuhimu wa kutoa mafunzo hayo kwa Wanahabari. Bugingo, amesema mradi wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya awali ya mtoto ni mradi unaotekelezwa na Serikali kupitia Wizara ya Afya pamoja na Wizara ya Maendeleo ya Jamii lakini unashirikisha Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania(UTPC). Bugingo, amewaomba Waandishi ...

KISHINDO CHA MBUNGE KOKA SEMINA YA WAENEZI KIBAHA MJINI, AMFAGILIA RAIS SAMIA

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  MBUNGE wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka, amewataka makatibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo wa ngazi Matawi na Kata kuhakikisha wanatumia vizuri nafasi zao kuhakikisha Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan anakwenda kushinda Kwa kishindo katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka huu. Aidha, Koka amesema ushindi wa Rais Samia ni wazi kuwa utaambatana na ushindi wa nafasi ya Ubunge katika Jimbo la Kibaha Mjini kwakuwa kazi nzuri za kimaendeleo zimefanyika kwa kiwango kikubwa.  Koka, amesema hayo wakati akifunga semina ya makatibu  hao iliyofanyika katika ukumbi wa Kibaha Shopping Mall ambapo semina hiyo  iliandaliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM)  Kibaha Mjini kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu yao hususani katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu. Makatibu Uenezi Siasa na Mafunzo wakiwa katika Semina ya kujengewa uwezo iliyofanyika Februari 11 katika Ukumbi wa Kibaha Shopping Mall,semina hiyo iliandaliwa na CCM Kiba...

MNEC JUMAA AWAFUNDA MAKATIBU UENEZI KIBAHA MJINI, ATAKA WAENDE KUTANGAZA KAZI ZA RAIS SAMIA

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Taifa  ya  Chama Cha Mapinduzi ( CCM) Hamoud Jumaa(MNEC) amefungua semina ya makatibu wa Itikadi, Uenezi, Siasa na Mafunzo wa Kibaha Mjini na kuwataka waende kufanyakazi ya kutangaza kazi zilizofanywa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan. Jumaa, amefungua mafunzo hayo  Februari 11,2025 katika ukumbi wa Kibaha Shopping Mall uliopo karibu na stendi Kuu ya Mabasi ya Mkoani iliyopo Kibaha Mjini mafunzo ambayo yameandaliwa na CCM Kibaha Mjini. Jumaa, amesema kuwa yapo mambo mengi CCM imetekeleza chini ya Dkt.Samia Suluhu Hassan hivyo lazima kazi hizo zielezwe kwa Wananchi pamoja na wanaCCM wote ambapo kwa kufanya hivyo watakuwa wamemtendea haki Rais Samia. Makatibu Uenezi,Siasa na Mafunzo wa matawi na Kata wa Kibaha Mjini wakishiriki semina iliyofanyika katika viwanja vya Kibaha Shopping Mall Februari 11,2025 ,semina hiyo imeandaliwa na CCM Kibaha Mjini  Amesema kuwa mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi mkuu na  CCM inahitaj...

TAKUKURU PWANI YAONGEZA NGUVU UCHAGUZI MKUU 2025, YATOA ONYO KWA WATOA RUSHWA

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Pwani imesema kuwa katika kuelekea kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 imejipanga kikamilifu katika kudhibiti vitendo vya rushwa vinavyofanywa na baadhi ya wagombea. Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Pwani Alli Sadiki, ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu vitendo vya rushwa katika uchaguzi na namna ya kukabiliana navyo. Sadiki, ambaye pia alikuwa akieleza utekelezaji wa shughuli zake katika kipindi cha Oktoba na Desemba 2024 amesema kuwa suala la uchaguzi mwaka huu ndio jukumu ambalo wanakwenda kulifanya kwa ueledi mkubwa kwakuwa wanataka kuona viongozi wanapatikana kwa njia halali na haki. Sadiki,  amesema kuwa kwasasa wataendelea kutoa elimu kwa Wananchi kuhusu madhara ya rushwa katika uchaguzi sambamba na kuwafikia wadau wote wanaohusika na uchaguzi ambao ni vyama vya Siasa,Wasimamizi wa Uchaguzi,Wanahabari, Wananchi na Jamii nzima kiujumla. "Takukuru inatambua ...

MBUNGE KOKA, AFUNGA MASHINDANO YA KIBAHA NDONDO CUP, AGAWA ZAWADI KEMKEM,AAHIDI KUONGEZA VIWANJA VYA KISASA.

Image
  Na Gustaphu Haule,Pwani MBUNGE wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka, amefunga fainali za mashindano ya Kibaha Ndondo Cup yaliyokuwa yakifanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi Mailimoja huku akiahidi kuendelea kuboresha michezo kwa kujenga viwanja vya kisasa. Katika fainali hiyo iliyofanyika kati ya timu ya Sheli Fc kutoka Kata ya Mailimoja na timu ya Ungaunga Fc kutoka Kata ya Tangini iliwavutia Wananchi wengi lakini hata hivyo Ungaunga Fc aliibuka kuwa mshindi Kwa kupata bao 1-0. Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka,akitoa zawadi ya Ng'ombe na Mpira Kwa mshindi wa mashindano ya Kibaha Ndondo Cup Ungaunga FC katika fainali  zilizofanyika  katika viwanja vya Shule ya Msingi Mailimoja, mashindano hayo yalikuwa chini CCM Kata ya Mailimoja  Mashindano hayo ambayo yaliandaliwa na Chama Cha Mapinduzi ( CCM) Kata ya Mailimoja yamelenga kuibua vipaji lakini pia kuunga mkono jitihada za Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan katika kuendeleza michezo hapa nchini. Aidha...

TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YAINGIA PWANI,YAANZA KUTOA ELIMU YA UANDIKISHAJI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA.

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi imewakutanisha wadau mbalimbali wa uchaguzi wa Mkoa wa Pwani ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura zoezi ambalo linatarajia kuanza Februari 13 hadi 19 ,2025. Wadau waliokutanishwa na Tume hiyo wametoka katika  makundi mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini,Vyama vya Siasa,Watu wenye ulemavu,Wazee maarufu,Asasi za kiraia,Wawakilishi wa Vijana,Wahariri, Wawakilishi wa Wanawake, Wawakilishi wa Mkoa na kamati ya ulinzi na usalama. Akizungumza wakati akifungua mkutano huo uliofanyika Februari 01, 2025 Mjini Kibaha makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Mbarouk Mbarouk, amesema kuwa lengo la mkutano huo ni kuanza maandalizi ya uboreshaji wa daftari la kudumu la  wapiga kura Mkoani Pwani. Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Mbarouk Mbarouk akifungua mkutano wa wadau kuhusu zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga kura linalota...