Posts

Showing posts from December, 2024

IJUE SIRI YA JOSEPHINE MAENDAENDA KUCHAGULIWA MARA TATU KITONGOJI CHA JANGA.

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani UNAPOTAKA kuwataja wenyeviti wa Vitongoji Wanawake waliopo katika Halmashauri ya Kibaha Vijijini hutakosa kumtaja Josephine Maendaenda  mwenyekiti wa Kitongoji cha Janga kilichopo Kata ya Janga. Maendaenda ameshinda katika uchaguzi wa Serikali ya Mitaa,Vijiji na Vitongoji uliofanyika Novemba 27 mwaka huu kwa kupata kura 2066 ushindi  ambao unamfanya kuwa mwenyekiti wa Kitongoji cha Janga kwa awamu ya tatu mfululizo. Ushindi wa Maendaenda kwa Kitongoji hicho sio wa bahati mbaya bali nikusudio jema kwa Wananchi wake kutokana na umahiri wa kiuongozi katika vipindi viwili vya nyuma alivyowai kuongoza. Maendaenda ambaye pia ni mama mjasiriamali mwenye watoto wanne amekuwa na uzoefu mkubwa wa kiuongozi na hivyo kuwafanya Wananchi wake wafurahie kumchagua katika kila uchaguzi unapowadia. Maendaenda katika uchaguzi wake  hakuwa na mpinzani ambapo  wakati wa uchaguzi, mpiga kura alikuwa na chaguo la kutiki Ndio au Hapana jambo ambalo pia liliwapa wepe...

SERIKALI YA RAIS SAMIA YANADI FURSA ZA UWEKEZAJI FALME ZA KIARABU.

Image
Na Gustaphu Haule, Tanzania  #KAZIINAONGEA Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, inaendelea na mkakati wake wa kufungua fursa za Uwekezaji ambapo imeikaribisha Saudi Arabia kuwekeza nchini katika fursa mbalimbali zikiwemo Utalii, Kilimo, Madini, Uendelezaji wa miundombinu pamoja na Uchumi wa Buluu. Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu  Nchemba, ametoa mwaliko huo alipokutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Wizara ya Uchumi na Mipango wa Saudi Arabia mhandisi Ammar Naqadi,  Nchemba amekutana na Mhandisi Naqadi katika mkutano wa Jukwaa la Biashara na Uwekezaji lililoandaliwa na Ubalozi wa Tanzania kwa kushirikiana na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) na Shirika la Kuendeleza Uwekezaji Zanzibar (ZIPA), lililofanyika hivi karibuni Mjini Riyadh nchini Saudi Arabia. Dkt. Nchemba amebainisha kuwa, Tanzania inaendelea na mradi wa ujenzi wa Reli ya kisasa (SGR) ambapo imeshakamilika kipande kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma na ujenzi unaendelea ...

SERIKALI YA RAIS SAMIA YAFANIKIWA UWEKEZAJI DP WORD DAR ES SALAAM.

Image
Na Gustaphu Haule, Tanzania  *●Yawekeza Sh.Bilioni 214.425 katika miezi mitano* #KAZIINAONGEA Kwa mujibu wa mkataba kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, chini ya Uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na  Kampuni ya DP World (DPW),  inapaswa kuwekeza Dola za Marekani Milioni 250 sawa na Shilingi Bilioni 675 katika kipindi cha miaka mitano. Katika kipindi cha miezi mitano tangu kuanza uwekezaji kwa kampuni hiyo, tayari wameshawekeza Shilingi  Bilioni 214.425 ambayo ni asilimia 31,  kwa ajili ya manunuzi ya mitambo ya kisasa, ukarabati wa mitambo iliyokuwa ya TPA, na usanifu na usimikaji wa mfumo wa TEHAMA wa kisasa wa uendeshaji wa Bandari.  Katika taarifa iliyotolewa na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, alipotembelea Bandari ya Dar es Salaam amesema kuwa, tangu Kampuni ya DP World ianze uendeshaji wa shughuli za Bandari mwezi Aprili 2024, mafanikio mbalimbali yamepatikana. Msemaji wa Serikali GERSON MSIGWA Ameyataja mafanikio hayo n...

TRA PWANI YAFURAHIA MAONESHO YA VIWANDA YASEMA YAMEKUWA NA MAFANIKIO,YAWAOMBA WALIPAKODI KUDAI NA KUTOA RISITI PINDI WANAPOUZA NA KUNUNUA BIDHAA

Image
  Na Gustaphu Haule,Pwani MENEJA wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)  Mkoa wa Pwani Masawa Masatu amesema maonesho  ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji yaliyofanyika Mjini Kibaha yamekuwa na mafanikio makubwa pamoja na kutoa fursa kwa walipa kodi wengi kupata elimu. Masatu ameyasema hayo Desemba 20 mwaka huu wakati akizungumza na Waandishi wa Habari waliotembelea katika banda  la TRA kwa ajili ya kujionea shughuli zilizokuwa zikifanywa na TRA katika maonesho hayo . Masatu ,amesema kuwa TRA ambao ni moja ya wadhamini wa maonesho hayo waliona kushiriki maonesho hayo ni fursa kwa walipakodi kupata huduma sambamba na elimu ambayo itawasaidia katika kusimamia biashara zao. Amesema kuwa, huduma zilizokuwa zikitolewa katika maonesho hayo ni zile zile ambazo zilikuwa zinapatikana ofisini ambapo miongoni mwa huduma hizo ni kusajili TN namba, kutoa huduma ya namba za kulipia (Control Number), kurekebisha taarifa mbalimbali za walipakodi pamoja na kutoa elimu ya Kodi. "Huduma zote...

STAMICO YAWASHAURI WATANZANIA KUTUMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA , YASEMA INAOKOA GHARAMA

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani SHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limewashauri Watanzania kutumia Nishati SAfi ya Kupikia  inayotengenezwa na Shirika hilo kwakuwa Nishati hiyo inasaidia kutunza mazingira pamoja na kuokoa gharama za maisha . Afisa Masoko wa STAMICO  Hope Mahokola,ametoa ushauri Desemba 20 wakati akizungumza na waandishi habari katika maonesho ya Viwanda Biashara na Uwekezaji yanayofanyika katika viwanja vya stendi ya zamani Mailimoja Kibaha Mkoani Pwani. Mahokola, amesema kuwa Nishati Safi  ya kupikia inayotengenezwa na Shirika hilo inatokana na mabaki ya  Makaa ya Mawe ambayo ni rafiki kwa mazingira hivyo ni vyema  jamii ikatumia Nishati hiyo. Amesema kuwa,ajenda ya Nishati Safi ya kupikia ni ajenda ya Rais kwakuwa malengo yake ni kuifanya nchi hiwe salama katika kuondokana na adha ya uharibifu wa mazingira unaotokana na kukata kuni na mkaa. Afisa Masoko wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Fatuma Msumi (kushoto)akitoa elimu ya matumizi ya Nishati...

KAMPUNI YA DOWERCARE TECHNOLOGY YAGAWA TAULO ZA KIKE ZAIDI YA 20,000 KWA WANAFUNZI NCHINI

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani KAMPUNI ya Dowercare Teknology ya Kibaha Mkoani Pwani imefanikiwa kuifikia jamii kwa kugawa bure taulo za kike  zaidi ya 20,000 kwa wanafunzi wa Shule mbalimbali hapa nchini. Kampuni hiyo ambayo ni wazalishaji wa bidhaa mbalimbal ikiwemo pampanzi (pampers) vifutio vya watoto (Baby Wipes), Taulo za kike, sabuni za miche na zile za unga ikiwemo Doff ni miongoni mwa kampuni ambazo zimekuwa zikizalisha bidhaa zenye ubora hapa nchini. Afisa Masoko wa kampuni hiyo Lucia Msami, amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maonesho ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji yanayofanyika katika viwanja vya stendi ya zamani Mailimoja Kibaha Mkoani Pwani. Afisa Masoko wa kampuni ya Dowercare Technology Lucia Msami akiwa katika maonesho ya Viwanda Biashara na Uwekezaji katika viwanja vya stendi ya zamani Mailimoja Kibaha Pwani. Amesema kuwa,kampuni yake imekuwa ikigusa jamii hususani watoto wa kike kwa kugawa taulo bure mashuleni na kwamba kwa mwaka 2023/2024 w...

WAZIRI PROF. KABUDI AKUTANA NA WADAU SEKTA YA HABARI NA UTANGAZAJI

Image
Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam.    * Wizara hii ndiyo inayobeba Taswira na Haiba ya Tanzania na Taswira na Haiba ya Mtanzania   * Sekta ya Habari ni mhimili usio rasmi wa nne wa demokrasia      Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Palamagamba Kabudi amekutana na kufanya mazungumzo na wadau wa sekta ya habari na utangazaji jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere tarehe 18 December 2024. Wadau walioshiriki mkutano huo ni Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Umoja wa Klabu za Waandishi wa HabarI Tanzania (UTPC), Umoja wa Haki ya kupata Taarifa (CoRI), Idara ya Habari Maelezo, Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari, Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari (MOAT), Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Waandishi wa habari na wadau wengine wa Sekta ya Habari na Utangazaji. Mkutano huo ndio wa kwanza tangu Waziri Prof. Kabudi ateuliwe kushika ...

BARAZA LA UUGUZI NA UKUNGA TNMC KUENDESHA MTIHANI WA USAJILI NA LESENI KWA WAHITIMU 5,147 NCHINI, WADANGANYIFU KUFUTIWA MITIHANI.

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani BARAZA la Uuguzi na Ukunga Tanzania (TNMC) limejipanga kuendesha Mtihani wa usajili na leseni kwa wahitimu 5147 utakaofanyika Disemba 20 mwaka huu katika vituo Saba vilivyopo hapa nchini. Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga hapa nchini Agness Mtawa, ametoa taarifa hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi zake zilizopo Kibaha Mkoani Pwani. Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania( TNMC) Agness Mtawa wa kwanza Kulia akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha leo Disemba 18,2024 kuhusu kuelekea katika mtihani wa usajili na leseni kwa Wauguzi na Wakunga pamoja na wataalamu wa dawa za usingizi na ganzi utakaofanyika Disemba 20 mwaka huu. Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania( TNMC) Agness Mtawa wa kwanza Kulia akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha leo Disemba 18,2024 kuhusu kuelekea katika mtihani wa usajili na leseni kwa Wauguzi na Wakunga pamoja na wataalamu wa dawa za usingizi na ganzi ...

WAZIRI JAFO ATAKA WAWEKEZAJI WAZALISHE BIDHAA ZENYE UBORA KUENDANA NA SOKO LA DUNIA

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani WAZIRI wa Viwanda na Biashara Dkt. Selemani Jafo amewataka wawekezaji kuhakikisha wanazalisha bidhaa zenye viwango vya juu ili kuendana na Soko la dunia. Jafo, ametoa wito huo wakati akifungua maonesho ya Nne ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji yanayofanyika viwanja vya stendi ya zamani Kibaha Mailimoja Mkoani Pwani. Amesema kuwa, Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan imeweka mazingira mazuri na wezeshi kwa wawekezaji hivyo ni vyema sasa bidhaa zinazozalishwa ziwe za viwango. "Nawaomba wawekezaji kuzalisha bidhaa zenye ubora ili ziweze kupata Soko la dunia lakini na sisi Watanzania tujitahidi kupenda vyakwetu kwakuwa uwezo wa kuzalisha bidhaa bora tunao,"amesema Jafo Amesema Wizara inakuja na mpango mahususi wa miaka mitano wa kuwakwamua vijana kupitia Kilimo cha matunda utakaonza mwaka 2025 hadi 2030 ambapo utakuwa unasimamia vijana katika Uzalishaji wa matunda ya aina mbalimbali na tayari Soko lipo. Waziri wa Viwanda na ...

BENKI YA CRDB YAHAMASISHA SAMIA BOND, YASEMA NI MKOMBOZI KWA WATANZANIA

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani  BENKI ya CRDB imewahamasisha Wananchi  kuchangamkia fursa ya kufungua akaunti kwa ajili Hatifungani ya Miundombinu ya Samia( Samia Infrastructure Bond) kwakuwa manufaa yake ni makubwa. Meneja Mwandamizi Kitengo cha Serikali kutoka Benki ya CRDB Faraja Kaziulaya, ametoa hamasa hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maonesho ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji yanayofanyika katika viwanja vya stendi ya zamani Mailimoja Mjini Kibaha. Meneja Mwandamizi wa Kitengo cha Serikali kutoka CRDB Faraja Kaziulaya, akizungumza na waandishi wa habari katika maonesho ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji yanayoendelea kufanyika  Kibaha Mkoani Pwani. Maonesho hayo yamefunguliwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt.Selemani Jafo Disemba 17,2024 ambapo wadau mbalimbali wanashiriki ikiwemo Benki ya CRDB. Akizungumzia kuhusu Samia Infrastructure Bond Kaziulaya amesema kuwa mpango huo unafanyika kwa kushirikiana na Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA...