Posts

Showing posts from April, 2024

MWENGE WA UHURU KUZINDUA MIRADI 126 YENYE THAMANI YA TRILIONI 8•5 PWANI

Image
Na Gustafu Haule, Pwani  MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge,amesema kuwa mbio za mwenge wa Uhuru zilizoanza leo Mkoani humu zinatarajia kufikia  miradi 126 yenye thamani zaidi ya Trilioni 8.5. Kunenge,ametoa taarifa hiyo leo Aprili 29 wakati akipokea Mwenge huo kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa  Morogoro Adam Malima ambapo makabidhiano yake yalifanyika katika viwanja vya Jeshi la Magereza Bwawani katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze. Katika taarifa yake Kunenge amesema kuwa Mwenge wa Uhuru ukiwa Mkoani Pwani utapita katika Wilaya Saba na Halmashauri Tisa  huku jumla ya miradi 126 itapitiwa ambapo kati ya hiyo miradi 18 itawekewa mawe ya msingi, miradi 22 itazinduliwa na miradi 86 itakaguliwa. Kunenge,amesema kuwa fedha za utekelezaji wa miradi hiyo imetoka sehemu mbalimbali ikiwemo Serikali Kuu, Halmashauri za Wilaya ,wadau na nguvu za Wananchi. Aidha , Kunenge ametumia nafasi hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan ambaye ndi...

MBARONI KWA KUMDHALILISHA NA KUMTISHIA PINGU WAZIRI NA MBUNGE MSTAAFU.

Image
  Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani Pius Lutumo. Diwani Mstaafu na Askari Mgambo wakamatwa na Polisi Bagamoyo Wapata dhamana, kufikishwa Mahakamani wakati wowote   Na Mwandishi wetu Bagamoyo Jeshi la Polisi mkoani Pwani limemkamata Diwani mstaafu wa kata ya Kiromo Bagamoyo Hassani Usinga maarufu Wembe pamoja na askari mgambo Abdala Mgeni kwa tuhuma ya kumshambulia kwa maneno makali ,kumdhalilisha na kumtishia kumfunga pingu kama muhalifu Waziri na Mbunge mstaafu jimbo la Bagamoyo Dk. Shukuru Kawambwa  hali iliyopelekea taharuki kubwa kwa jamii ndani na nje ya Wilaya hiyo. Watuhumiwa hao wanadaiwa kutenda kosa  hilo Aprili 24 saa nane mchana na kuonekana kupitia kwenye clip ya video iliyosambaa  kwenye mitandao ya kijamii Aprili 25 ikimuonyesha Waziri na Mbunge mstaafu Dk. Shukuru Kawambwa na mtu mwingine aitwaye Cathbert Madondola wakishambuliwa kwa maneno makali,vitisho, dharau na kutishiwa kufungwa pingu na Diwani huyo mstaafu akiwa na askari mgambo huyo. ...

TFS WACHANGIA MILIONI 20 WAHANGA WA MAFURIKO KIBITI NA RUFIJI

Image
Na Gustafu Haule,Pwani WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) imetoa kiasi cha Sh.milioni 20 kwa ajili ya kusaidia kutatua Changamoto za wahanga wa mafuriko yaliyotokea katika Wilaya ya Kibiti na Rufiji  Mkoani Pwani. Mfano wa hundi ya fedha hizo imekabidhiwa leo na meneja mahusiano wa TFS  nchini Johary Kachwamba kwa mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge katika hafla iliyofanyika ofisi za Mkuu huyo zilizopo Mjini Kibaha. Kachwamba,amesema kuwa TFS kupitia Kamishna wake Silayo Dos Santos imeguswa na janga hilo la mafuriko ndio maana imeona kuna kila sababu ya kuunga mkono Serikali kwa kusaidia wahanga wa Wilaya hizo. Amesema kuwa,TFS kwa eneo la Rufiji wanamisitu na kwamba wanaRufiji ni wahifadhi wenzao kwakuwa TFS ina misitu zaidi ya 10 ikiwa na zaidi ya hekta 32,000 ndio maana Kamishna wa Uhifadhi ametoa kiasi ili kusaidia wahanga hao. Amesema,pamoja na kutoa mchango huo lakini bado TFS wataendelea kushika mkono katika kutatua changamoto mbalimbali pale ambapo itahitajik...

KIBAHA HURU YACHANGIA MADAWATI YA MILIONI 3 HALMASHAURI YA MJI.

Image
Na Gustafu Haule, Pwani. KUNDI la mtandao wa kijamii la Whatsapp linalofahamika kwa jina la "Kibaha Huru" limekabidhi madawati 30 yenye thamani ya shilingi milioni tatu (3,000,000) kwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Kibaha Mussa Ndomba ikiwa ni kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan.   Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika leo katika ofisi za Halmashauri ya Mji wa Kibaha tukio ambalo limeshuhudiwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkurugenzi wa  Halmashauri hiyo Dkt.Rogers Shemwelekwa,baadhi ya madiwani na hata wanakikundi wa Kibaha Huru. Kiongozi wa Kibaha Huru Sudi  Mohamed akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukabidhi madawati 30 kwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Kibaha Musa Ndomba katika hafla iliyofanyika April 19, 2024.  Aidha,katika hafla hiyo Ndomba amewashukuru wadau hao huku akiomba wengine kuiga mfano wa kutumia vizuri makundi ya mitandao ya Kijamii kuchangia shughuli za maendeleo. Viongozi wa Kibaha Huru akiwepo mc...

ASKARI WATAKIWA KUICHUKIA RUSHWA PWANI

Image
Na. Julieth Ngarabali, Pwani. Askari wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani wametakiwa kuichukia rushwa na kufanya kazi kwa kuheshimu  Sheria za nchi na maadili ya utumishi wa umma wanapotumikia wananchi. Hayo yamesemwa  Aprili 16, na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), Pius Lutumo wakati akizungumza na maafisa, wakaguzi na askari wa vyeo mbalimbali wakati akifanya majumuisho ya ziara yake ya ukaguzi kwa Wilaya zote za Mkoa wa Pwani. Kamanda Lutumo, ameeleza kuwa jukumu la askari ni kutoa huduma bora kwa wananchi wanaowahudumia na kushindwa kufanya hivyo  husababisha jamii kukosa imani na Jeshi la Polisi.  Aidha, Kamanda Lutumo amekemea vitendo vyote vyenye viashiria vya rushwa kwa askari Polisi wa Mkoa wa Pwani na ameeleza hatasita kuchukua hatua za kinidhamu kwa askari yeyote atakayebainika kujihusisha na  vitendo vya kuomba au kupokea rushwa badala ya kufanya kazi  kwa mujibu wa Sheria za nchi na maadili kwa watumis...

RAIS DK. SAMIA ATOA MSAADA WA VYAKULA KWA WAHANGA WA MAFURIKO RUFIJI NA KIBITI

Image
RAISI wa Jamuhuri ya Muungano Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa msaada binafsi wa Tani 300 za vyakula mbalimbali kwa wahanga wa mafuriko Wilayani Rufiji na Kibiti Mkoani Pwani Mwakilishi wa Rais Innocent Mbilinyi ndiye amekabidhi msaada huo kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge na kutaja vyakula vingine ni Tan 100 za mchele, Maharage tan 100 na Unga tani 100. Akipokea msaada huo, Kunenge ameshukuru na kusema Rais Dk. Samia. amekuwa akipeleka misaada mbalimbali kutoka Serikalini lakini huu wa safari hii ni msaada binafsi kutoka kwa Rais mwenyewe. "Mheshimiwa Rais amekuwa akituletea msaada kutoka Serikalini lakini msaada huu tuliopokea leo ni msaada binafsi kutoka kwa Rais mwenyewe " amesema Kunenge. Aidha, Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Edward Gowelle amemshukuru na kusema msaada huo utakwenda kuondoa changamoto ya mahitaji ya vyakula kwa wananchi wa Rufiji na Kibiti na kuahidi itawafikia walengwa kama ilivyopangwa. Wilayani Rufiji na...

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA ATAKA UMAKINI MATUMIZI YA TEKNOLOJIA

Image
Waziri wa Katiba na Sheria Balozi  Dk Pindi Chana amewataka watumishi wa Wizara hiyo na Watanzania kwa ujumla  kuwa makini na matumizi ya teknolojia hasa Ile ya  akili bandia ili wasije wakapotoshwa katika kutoa au kupokea maamuzi mbalimbali ikiwemo  za  kesi zinazohitaji utafiti wa kutosha . Waziri wa Katiba na Sheria Balozi  Dk Pindi Chana  akifungua  mkutano wa 20 wa  Baraza la wafanyakazi wa tume ya kurekebisha sheria Tanzania Balozi  Chana  amesema  teknolojia ni nzuri lakini inahitajika umakini wa hali ya juu kwani kupitia baadhi ya mifumo maarufu   ''Applications'' (Apps) inaweza ikatengeneza jambo au ikatoa hotuba  fulani isio halisi na endapo hakutakuwepo umakini  watu  watafikiri  kweli  kumbe sio kweli. Akili bandia "Artifial Intelligence" teknolojia iliyotengenezwa kwenye mifumo ya kompyuta kurahisisha kazi zinazotumia akili za kibinadamu Waziri huyo amesema hayo  akifungua...

KUUZWA KWA GESI BEI YA RUZUKU KUPUNGUZA MATUMIZI YA MKAA NA KUNI.

Image
Na Yohana Msafiri, Kibaha. Wakati  wananchi  wengi wanaendelea kupikia mkaa na kuni huku wakikwepa matumizi ya gesi kwa kushindwa  gharama, wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kikongo Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani  wamesema serikali inapaswa kuweka utaratibu utakaowezesha makampuni yanayohusika na nishati hiyo kuwauzia wananchi kwa  bei ya ruzuku. Wametoa kauli hiyo machi 27,2024 wakati wa maadhimisho ya upandaji miti yaliyofanyika  shule ya Sekondari Kikongo kwa ngazi ya Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha. "Miti inateketea, jangwa linaenea, hali ya hewa inazidi kuchafuka, chanzo ni ukataji wa miti unaofanywa na watu ili kutengeneza mkaa na hilo halikwepeki kwa sasa kwakuwa hata hizo bei za gesi ni kubwa ndio maana wananchi wengi wanakimbilia mkaa na kuni kupikia"amesema Khadija Selemani mwanafunzi wa shule hiyo ya Sekondari Kikongo. Na kuongeza“Tumekuwa tukiona ugawaji wa mitungi bure kwa baadhi ya wananchi mama lishe na baba lishe  lakini hi...