WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA ATAKA UMAKINI MATUMIZI YA TEKNOLOJIA




Waziri wa Katiba na Sheria Balozi  Dk Pindi Chana amewataka watumishi wa Wizara hiyo na Watanzania kwa ujumla  kuwa makini na matumizi ya teknolojia hasa Ile ya  akili bandia ili wasije wakapotoshwa katika kutoa au kupokea maamuzi mbalimbali ikiwemo  za  kesi zinazohitaji utafiti wa kutosha .

Waziri wa Katiba na Sheria Balozi  Dk Pindi Chana akifungua  mkutano wa 20 wa  Baraza la wafanyakazi wa tume ya kurekebisha sheria Tanzania


Balozi  Chana  amesema  teknolojia ni nzuri lakini inahitajika umakini wa hali ya juu kwani kupitia baadhi ya mifumo maarufu   ''Applications'' (Apps) inaweza ikatengeneza jambo au ikatoa hotuba  fulani isio halisi na endapo hakutakuwepo umakini  watu  watafikiri  kweli  kumbe sio kweli.

Akili bandia "Artifial Intelligence" teknolojia iliyotengenezwa kwenye mifumo ya kompyuta kurahisisha kazi zinazotumia akili za kibinadamu


Waziri huyo amesema hayo  akifungua  mkutano wa 20 wa  Baraza la wafanyakazi wa tume ya kurekebisha sheria Tanzania na.kwamba mkutano huo  unafanyika kwa siku mbili  kwenye  ukumbi wa shule ya uongozi  ya  Mwalimu Nyerere Kwamfipa Kibaha Mkoani Pwani 

Sehemu ya Washiriki wa mkutano wa 20 wa  Baraza la wafanyakazi wa tume ya kurekebisha sheria Tanzania wakifuatilia jambo wakati wa mkutano huo.


"Hivi sasa unaposema Teknolojia  kuja Apps za kila aina  kiasi kwamba vitu vingi  unaweza ukauliza  kwenye App ukapewa majibu  sasa wakati tunatumia teknolojia aina hii  tuwe macho kwanza kujiridhisha  lwamba majibu tulioletewa ni sahihi "amesema na kuongeza

"Lakini pia vijana wetu,watumishi wetu na wa Tanzania wasiache kutumia  uwepo wao wenyewe binafsi  wa akili kutafiti kama jinsi ambavyo enzi za nyuma tumekua tukifanya"

George Mandepo ni Katibu mtendaji Tume ya  kurekebisha sheria Tanzania kwa pamoja na Baadhi ya wajumbe wa Baraza hilo wamesema  malengo, umuhimu na matarajio yao kwanza ni kuwashirikisha wafanyakazi   katika maamuzi  kwa sababu ni sawa la Bunge la wafanyakazi maeneo ya kazi.

 Katibu mtendaji Tume ya  kurekebisha sheria Tanzania Ndugu George Mandepo


Masuala yote yanayohusiana na taasisi ikiwemo bajeti ,muundo  yanajadiliwa kwenye kikao  kaka hicho cha Baraza la wafanyakazi 




Club News Editor - Charles Kusaga

Comments

Popular posts from this blog

RC PWANI AONGOZA WAKAZI PWANI KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA

BARAZA LA MADIWANI KIBAHA MJINI LAMPONGEZA MKURUGENZI WAKE KWA KAZI NZURI ANAYOIFANYA SAMBAMBA NA KUONGEZA MAPATO.

RAIS SAMIA ATANGAZA KIBAHA MJINI KUWA MANISAPAA,MBUNGE KOKA AFURAHIA ASEMA KIBAHA ITANG'AA