MBARONI KWA KUMDHALILISHA NA KUMTISHIA PINGU WAZIRI NA MBUNGE MSTAAFU.


  Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani Pius Lutumo.

  • Diwani Mstaafu na Askari Mgambo wakamatwa na Polisi Bagamoyo
  • Wapata dhamana, kufikishwa Mahakamani wakati wowote

 Na Mwandishi wetu Bagamoyo

Jeshi la Polisi mkoani Pwani limemkamata Diwani mstaafu wa kata ya Kiromo Bagamoyo Hassani Usinga maarufu Wembe pamoja na askari mgambo Abdala Mgeni kwa tuhuma ya kumshambulia kwa maneno makali ,kumdhalilisha na kumtishia kumfunga pingu kama muhalifu Waziri na Mbunge mstaafu jimbo la Bagamoyo Dk. Shukuru Kawambwa  hali iliyopelekea taharuki kubwa kwa jamii ndani na nje ya Wilaya hiyo.

Watuhumiwa hao wanadaiwa kutenda kosa  hilo Aprili 24 saa nane mchana na kuonekana kupitia kwenye clip ya video iliyosambaa  kwenye mitandao ya kijamii Aprili 25 ikimuonyesha Waziri na Mbunge mstaafu Dk. Shukuru Kawambwa na mtu mwingine aitwaye Cathbert Madondola wakishambuliwa kwa maneno makali,vitisho, dharau na kutishiwa kufungwa pingu na Diwani huyo mstaafu akiwa na askari mgambo huyo.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani Pius Lutumo watuhumiwa hao wamekamatwa na wanatarajiwa kufikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.

Lutumo amebainisha kuwa chanzo cha tukio hilo magari ya mchanga ya mtuhumiwa kuharibu barabara na mashamba ya watu yakipita kwenda kubeba mchanga eneo la hilo hali iliyopelekea wananchi kufunga barabara kwa magogo ili kuzuia uharibifu huo wa barabara usiendelee.

Katika clip ya video iliyokua inasambaa mitandaoni iliambatana na maneno yaliyosomeka kuwa ‘ Shukuru Kawambwa Waziri wa Miundombnu enzi hizo sasa ni dalali wa viwanja  Bagamoyo na muhalifu wa kawaida (common criminal)

‘’Jeshi la Polisi linamtaka mtu aliyechukua na kusambaza video hiyo mitandaoni ajisalimishe kituo cha Polisi Bagamoyo mara moja”amesema Kamanda Lutumo

Aidha Jeshi la Polisi Pwani linawataka wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi wafuate sheria za nchi na kuwatumia viongozi walionao kutatua matatizo yao.











Club News Editor 

Comments

Popular posts from this blog

RC PWANI AONGOZA WAKAZI PWANI KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA

BARAZA LA MADIWANI KIBAHA MJINI LAMPONGEZA MKURUGENZI WAKE KWA KAZI NZURI ANAYOIFANYA SAMBAMBA NA KUONGEZA MAPATO.

RAIS SAMIA ATANGAZA KIBAHA MJINI KUWA MANISAPAA,MBUNGE KOKA AFURAHIA ASEMA KIBAHA ITANG'AA