Posts

Showing posts from March, 2025

SERIKALI KUTENGENEZA SERA YA UINGIZAJI MAGARI NCHINI, MAGARI MABOVU HAYATARUHUSIWA TENA.

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ipo mbioni kutengeneza sera ya magari ambayo itazuia uingizaji wa magari chakavu hapa nchini. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais ,Mipango na Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo ametoa kauli hiyo Machi 26, 2025 mbele ya Waandishi wa habari mara baada ya kutembelea kiwanda cha kuunganisha magari cha GF Vehicle Assemblers Limited kilichopo Kibaha Mkoani Pwani. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo wa pili kutoka kulia akitembelea kiwanda cha GF Vehicle Assemblers Limited kilichopo Kibaha eneo la  Tamco alipotembelea Machi 26,2025 kujionea maendeleo ya kiwanda hicho. Kiwanda hicho kilichopo eneo la Tamco- Kibaha Mjini kinaunganisha magari makubwa ya mizigo aina ya FAW yenye uwezo wa kubeba mzigo tani 30. Akiwa katika kiwanda hicho Profesa Mkumbo, amesema kuwa sasa hivi Tanzania mtu anaruhusiwa kuingiza magari hata kama lina miaka 50. Amesema...

PROFESA KITILA MKUMBO ASEMA BIDHAA ZA KINGLION ZINAITANGAZA NCHI KIMATAIFA,AAHIDI KUTOA USHIRIKIANO KWA WAWEKEZAJI.

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo amesema vifaa vya ujenzi vinavyozalishwa hapa nchini vinajitosheleza na kwamba hakuna sababu ya  watanzania kuendelea kununua vifaa hivyo kutoka nje ya nchi. Aidha, Mkumbo  amesema kuwa Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan inaendelea kusimamia kwenye uwekezaji wa viwanda ili viweze kulipa wafanyakazi kwa kuzingatia viwango vinavyotakiwa. Mkumbo ameyasema hayo Mjini Kibaha alipofanya ziara ya siku moja ya  kukagua uzalishaji unaofanyika katika kiwanda cha Kinglion kinachounganisha pikipiki, kutengeneza mabati na vifaa vingine vya ujenzi. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo wa pili kutoka kushoto akiangalia namna bati zinavyozalishwa katika kiwanda cha Kinglion kilichopo Kibaha Mkoani Pwani alipofanya ziara ya kutembelea kiwanda hicho Machi 26, 2025. Mkumbo,amesema kuwa  kwasasa Tanzania imepiga hatua ...

MAKAMU WA RAIS DKT .PHILIP MPANGO KUZINDUA MBIO ZA MWENGE WA UHURU APRIL 2,KIBAHA PWANI.

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Philip Mpango anatarajia kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa utakaofanyika katika viwanja vya Shirika la Elimu Tumbi Kibaha Mkoani Pwani April 2, 2025. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu,Kazi ,Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu  Ridhiwani Kikwete,ametoa taarifa hiyo Machi 26, 2025 wakati akizungumza na Waandishi wa habari Mjini Kibaha. Kikwete,amesema kuwa katika uzinduzi huo Dkt.Mpango atawakabidhi vijana sita walioandaliwa kutoka Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar kwa ajili ya kukimbiza Mwenge huo kote nchini. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu,Kazi,Vijana ,Ajira na Wenye Ulemavu Ridhiwani Kikwete akitoa taarifa ya maandalizi ya uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa Waandishi wa habari leo Machi 26,2025 Mjini Kibaha  "Ninayofuraha kuwajulisha wananchi kuwa Makamu wa Rais Dkt.Philip Mpango atakuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru...

MAANDALIZI YA UZINDUZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU KITAIFA YAMEFIKIA ASILIMIA 96

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani  MAANDALIZI ya uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa unaotarajia kuwashwa April 2, 2025 katika viwanja vya Shirika la Elimu Tumbi Kibaha Mkoani Pwani yamefikia asilimia 96. Uwanja wa Shirika la Elimu Tumbi Kibaha Mkoani unaotarajia kutumika katika hafla ya uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa April 2, 2025. Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge, ametoa taarifa hiyo wakati akizungumza na Waandishi wa habari leo Machi 25 katika viwanja vya Shirika la Elimu Tumbi Kibaha mahali ambapo uzinduzi huo utafanyika. Kunenge,amezungumza na Waandishi wa habari hao mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi huo akiwa pamoja na timu ya maandalizi kutoka katika ofisi yake  pamoja na timu kutoka ofisi ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa. Kunenge, amesema Mkoa wa Pwani upo vizuri na umejipanga kikamilifu katika kuhakikisha tukio hilo kubwa la kihistoria na heshima linafanyika ndani ya Mkoa. Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge akizungumza na Waandishi wa habari...

MNEC JUMAA ASEMA MIAKA MINNE YA RAIS SAMIA IMEKUWA YA MAFANIKIO MAKUBWA ,ATAJA MAMBO MAKUBWA MANNE MUHIMU.

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi ( CCM) kupitia Jumuiya ya Wazazi Hamoud Jumaa( MNEC), amesema kuwa miaka minne ya uongozi wa Rais Dkt .Samia Suluhu Hassan imekuwa na mafanikio makubwa kwa Taifa na Wananchi wake. Jumaa amesema mafanikio hayo yametokana na sera na mikakati ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambayo imekuwa ikilenga kuongeza ushirikiano na maendeleo ya jamii kwa ujumla. Kauli hiyo ya Jumaa imekuja ikiwa ni sehemu ya kumpongeza Rais Samia kwa kazi alizofanya katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wake tangu aliporidhi kiti hicho kutoka kwa mtangulizi wake Hayyati John Pombe Magufuli (JPM) aliyefariki Machi 2021. Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Hamoud Jumaa (MNEC) katikati akiteta jambo na Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka (kushoto) na Kulia ni Waziri wa Tawala za Mikoa na  Serikali za Mitaa (Tamisemi) ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Rufiji Mohamed Mchengerwa. Jumaa am...

TANROADS YATOA UFAFANUZI KUTOZWA FAINI GARI LA SIMBA LOGISTICS KITUO CHA MIZANI YA VIGWAZA MKOA WA PWANI

Image
Na Gustaphu Haule Pwani  WAKALA ya Barabara Tanzania ( TANROADS) imetoa ufafanuzi kuhusu gari la mizigo la kampuni ya Simba Logistics Limited lililozuiliwa katika kituo cha  Mizani ya Vigwaza Mkoani Pwani baada ya kupimwa na kukutwa limezidisha uzito. Meneja wa TANROADS Mkoa wa Pwani Mhandisi Baraka Mwambage,amesema kuwa gari la Simba Logistics Limited lilifika katika kituo cha Mizani ya Vigwaza Machi 13 mwaka huu likitokea katika nchi jirani ya Zambia likiendeshwa na Pamela Bukumbi. Meneja Wakala ya Barabara  (TANROADS) Mkoa wa Pwani Mhandisi Baraka Mwambage, akitoa ufafanuzi kwa Waandishi wa habari kuhusu kutozwa faini kwa gari la mizigo la Simba Logistics Machi 13,2025 katika kituo cha Mizani ya Vigwaza iliyopo Mkoani Pwani . Amesema gari hilo lilikuwa limebeba mzigo wa Madini ya Shaba( Copper ) na baada ya kupimwa  lilibainika kuzidi uzito na hivyo kupaswa kulipa gharama ya Sh. 900,000 za Kitanzania. Mwambage, amesema kuwa shughuli za upimaji na udhibiti wa uzito...

RAIS SAMIA AWAFUTURISHA YATIMA PWANI, NI UTARATIBU WAKE WA KILA MWAKA

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan amewafuturisha zaidi ya watoto yatima  400 na wale waishio katika mazingira magumu kutoka katika Wilaya tofauti za Mkoa wa Pwani . Rais Samia amewafuturisha watoto hao Machi 9,2025 katika viwanja vya Ikulu ndogo ya Mkoa wa Pwani ambapo katika iftari hiyo Rais Samia amewakilishwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge. Akizungumza katika iftari hiyo Kunenge amesema kuwa Rais Samia amekuwa na tabia ya kila mwaka kukaa na watoto yatima katika mwezi mtukufu na kuwaandalia futari na kwamba mwaka huu ni mara yake ya nne. Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge akizungumza katika hafla fupi ya iftari iliyofanyika Machi 9,katika viwanja vya Ikulu ndogo ya Mkoa wa Pwani, Iftari hiyo imetolewa na Rais Samia kwa watoto yatima. Kunenge, amesema kuwa katika futari hiyo Rais Samia  angependa kuungana pamoja na watoto hao lakini kulingana na majukumu yake imebidi amwakilishe katika kutimiza adhma yake. ...

WANANCHI 14,428 WAFIKIWA KAMPENI YA KISHERIA YA MAMA SAMIA KIBAHA VIJIJINI.

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani KAMPENI ya msaada wa Kisheria ya Mama Samia (Mama Samia Legal Aid Campaign) katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani imefanikiwa kuwafikia zaidi ya Wananchi 14,428. Wakili wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Yasmin Makanya, ametoa taarifa hiyo Machi 6,2025 wakati akiwa katika kikao maalum na Katibu Tawala wa Wilaya ya Kibaha Moses Magogwa ikiwa sehemu ya kukabidhi ripoti ya kampeni hiyo. Wakili wa Serikali katika Halmashauri ya Wilaya Kibaha Yasmin Makanya katika kikao cha kukabidhi ripoti ya kampeni ya Mama Samia (Mama Samia Legal Aid Campaign) Aidha, Makanya katika kikao hicho ameongozana na baadhi ya  timu iliyofanyakazi katika Halmashauri hiyo akiwemo afisa ardhi wa Halmashauri hiyo Neema Adrian,afisa maendeleo ya Jamii ambaye pia Msaidizi wa dawati la kisheria Diana Brandus na Mkuu wa dawati la Jinsia kutoka Wilaya ya Kipolisi Mlandizi Inspekta Tumaini Ulimboka. Afisa Maendeleo ya Jamii na Msajili Msaidizi wa dawati la kisheria katika Halmasha...