Posts

Showing posts from September, 2024

TANZANIA KUSHIRIKI MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA DUNIANI

Image
. Na. Charles Kusaga, PWANI TANZANIA inashiriki Kongamano la tano la Kimataifa la Mashirikiano katika Mapambano Dhidi ya Rushwa. Kongamano hili ni mahusus kwa ajili ya Mamlaka za Kuzuia na Kupambana Rushwa Duniani kubadilishana uzoefu na utaalamu katika jukumu la kuzuia na kupambana na Rushwa. Kongamano hili la siku tano, linahudhuriwa na Mamlaka 219 za Kuzuia na Kupambana na Rushwa kutoka nchi 121 Duniani ikiwemo Tanzania ambapo - Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa wanashiriki. Pamoja na mambo mengine, Kongamano hili lilihusisha Warsha ya Wakuu wa Mamlaka za Kuzuia na Kupambana Rushwa  (HIGH LEVEL FORUM) kutoa uzoefu wao wa namna Serikali zinavyofanikiwa kudhibiti Rushwa katika mataifa yao.   Maeneo yaliyozungumziwa ni pamoja na Maono ya Ulimwengu (GLOBAL VISION), Mfumo wa Kisheria na Kitaasisi (LEGAL AND INSTITUTIONAL FRAMEWORK), Uendeshaji wa Mtandao wa Kimataifa (GLOBAL NETWORK OPERATIONS) na kujenga Ushirikiano. Kupitia Warsha hiyo,  Mkurugenzi Mkuu wa TAK...

MKURUGENZI KIBAHA MJINI AWAANGUKIA VIONGOZI UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA, ATAKA WATUMIE NAFASI ZAO KUHAMASISHA WANANCHI KUJIANDIKISHA

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  MKURUGENZI wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dkt.Rogers Shemwelekwa amewaangukia  viongozi wa makundi mbalimbali  wakiwemo viongozi wa dini, vyama vya Siasa, makundi ya watu wenye ulemavu na wazee maarufu kuwa mabalozi wazuri katika kuhamasisha wananchi kushiriki kwenye michakato ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Dkt.Shemwekwa ametoa kauli hiyo Septemba 26 mwaka huu wakati akifungua kikao maalum cha kutoa elimu ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa viongozi wa makundi hao kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dkt.Rogers Shemwelekwa akifungua kikao cha viongozi wa makundi mbalimbali leo Septemba 26 ikiwa sehemu ya uhamasishaji Wananchi kujitokeza katika michakato ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajia kufanyika Novemba 27 mwaka huu . Amesema kuwa, makundi ya viongozi hao ni muhimu kwakuwa wana uwezo na nafasi kubwa ya kuwaelimisha na kuwahamasisha Wananchi kujitokeza katika michakato mbalimbali y...

Kisa cha Gabriel na Grace: Safari ya huzuni na matumaini Mkoani Pwani.

Image
Mkazi wa Chalinze Pwani Grace Petro akiwa na watoto wake pacha. Julieth Ngarabali, Pwani. Katika kijiji cha Chalinze Mkoani Pwani, Gabriel Chumbi na mkewe Grace Petro wamepiga hatua muhimu katika maisha yao baada ya kupitia safari ndefu yenye huzuni. Kwa miaka mingi walikabiliana na changamoto kubwa ya kupoteza mimba saba mfululizo kwa mujibu wa Gabriel na Grace ambao wameeleza jinsi walivyoishi katika hali hii ngumu. Gabriel anasema kila mimba ilipofikia kati ya miezi mitano na saba walipata huzuni ya kupoteza mtoto aliyejifungua hali iliyoathiri sana maisha yao ya kila siku. “Mimba saba amna hata mtoto mmoja, naenda hospitali nikiwa na  mimba narudi nyumbani bila mtoto haikua rahisi, ilikuwa kipindi kigumu sana kwangu,” anasema Grace, huku akionyesha huzuni iliyokuwa ikiwakabili. Hata hivyo, waliweza kutatua changamoto hiyo baada ya kupata mimba ya nane miaka mitatu iliyopita. Wamesema ni kwa msaada wa wauguzi na madaktari wa hospitali na vituo vya afya waliyokua wakikimbilia iki...

DR.CHAKOU TINDWA AKAGUA JENGO LA KITEGA UCHUMI CCM MKOA WA PWANI, AELEZA KURIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WAKE

Image
Na. Gustaphu Haule, Pwani MJUMBE wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Pwani na makamu mwenyekiti wa Kamati ya uchumi ya CCM Mkoa Pwani Dr.Chakou Tindwa amefanya ziara maalum ya kutembelea na kukagua mradi wa jengo la kitega uchumi la CCM Mkoa wa Pwani. Dr.Tindwa amefanya ziara hiyo leo Septamba 13 katika jengo hilo lililopo Kibaha Mjini ambapo pamoja na mambo mengine ameeleza kuridhishwa na kasi ya ujenzi wa jengo hilo . Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Pwani na makamu mwenyekiti wa kamati ya uchumi Dr.Chakou Tindwa akikagua jengo la kitega uchumi la Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani katika ziara yake aliyoifanya leo Septemba 13.2024. Akiwa katika jengo hilo Dr .Tindwa amesema kuwa anatamani kuona jengo hilo linakamilika mapema ili kusudi kukisaidia chama kuondokana na usumbufu wa kutumia fedha nyingi kukodi kumbi za watu wengine Kwa ajili ya kufanyia mikutano ya Chama. "Mimi ni makamu mwenyekiti wa kamati ya uchumi ya CCM Mkoa wa Pwani, hivyo niliona ni vyema leo ni...

DR CHAKOU TINDWA AWASHIKA MKONO WAUMINI WA KANISA LA ANGLIKANA MJINI MKURANGA,ACHANGIA ZAIDI YA MILIONI 3 KUJENGA UZIO WA KANISA.

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  MJUMBE wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Pwani Dr.Chakou Tindwa ameungana na waumini wa kanisa la Anglikana lililopo Mkuranga Mjini katika kuendesha harambee ya kuchangia ujenzi wa uzio wa Kanisa hilo. Dr.Tindwa ambaye alikuwa mgeni rasmi katika harambee hiyo alichangia papo hapo fedha taslimu kiasi cha  Sh.milioni tatu ikiwa ni sehemu ya mchango wake katika ujenzi wa uzio huo. Dr.Tindwa ameendesha harambee hiyo juzi kanisani  hapo mbele ya viongozi wa wa Kanisa hilo pamoja na waumini mbalimbali waliokusanyika mahususi kwa ajili ya harambee hiyo. Mbali na kuchangia fedha hizo lakini pia Dr.Tindwa alitoa fedha nyingine kiasi cha Sh.laki nne kwa ajili ya kumuongezea Mwalimu wake wa Shule ya Sekondari Mwinyi ambaye awali aliahidi kuchangia lakini Moja . "Jamani huyu Mwalimu wangu kwakuwa ameshatoa laki Moja mimi nitamuongezea lakini nne na sasa atakuwa amechangia Sh.500,000",amesema Dr.Tindwa. Kutokana na hali hiyo Mwalimu huyo alijikuta amefikisha kiasi c...

FELISTER MSILLU, AZINDUA ALBAMU YA NYIMBO ZA INJILI, AOMBA WADAU WAMPE SAPOTI,ATAMANI KUMILIKI STUDIO

Image
Na Gustaphu Haule  MUIMBAJI wa nyimbo za injili Felister Msillu, amezindua albamu yake Septemba 8, 2024 huku akiwaomba wadau mbalimbali kumuunga mkono ili aweze kuendeleza kipaji chake cha kumtumikia Mungu. Uzinduzi wa albamu hiyo yenye nyimbo 11 na video 9 imebeba jina la "Niseme nini mbele zake Mungu" ikiwa na maana ya kuwa Mungu ametenda mengi makubwa na hakuna wa kuweza kumlipa. Katika hafla ya uzinduzi wa albamu hiyo uliofanyika katika ukumbi wa Mwitongo uliopo Mailimoja  Msillu aliambatana na viongozi wa dini kutoka Kanisa la KKKT Mailimoja  pamoja na waimbaji mbalimbali wa nyimbo za injili. Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi huo Msillu ametaja baadhi ya nyimbo katika albamu hiyo kuwa ni Niseme nini mbele zake Mungu, Mungu mtenda miujiza, Jina la Yesu,Hakuna Mungu kama wewe,na Mungu anamajina mengi. Msillu, amesema kuwa kilichomsukuma kuimba nyimbo za injili ni kutaka kumtumikia Mungu kupitia nyimbo hizo kwakuwa anaamini nyimbo hizo zitaishi m...

MOUNT CALVARY SPOTRS ACADEMY YAIOMBA TFF KUSAIDIA VIFAA VYA MICHEZO, YAPANIA KUIBUA VIPAJI VYA WANAFUNZI WAO

Image
Na. Gustaphu Haule, Pwani SHULE ya michezo ya Mount Calvary Sports Academy iliyopo Kiluvya kwa Komba  Kata Kibamba Manispaa ya Ubungo Jijini Dar es Salaam imeliomba Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) kuona namna ya kusaidia vifaa vya michezo katika Shule hiyo. Kocha wa mpira wa miguu kutoka Shule ya mchepuo wa michezo Mount Calvary Sports Academy Christopher Mjema akiwa na timu ya wanafunzi wa darasa la Saba na timu ya madarasa ya chini katika mchezo uliopigwa juzi shuleni hapo . Aidha, mbali na kuiomba TFF lakini pia uongozi wa Shule hiyo imewaomba wadau na wafadhili mbalimbali kujitokeza katika kusaidia changamoto za kimichezo katika Shule hiyo. Meneja wa Shule hiyo Erick Kilonzo, akizungumza na mwandishi wa habari katika mahafali ya darasa la Saba yaliyofanyika Shuleni hapo hivi karibuni ambapo amesema kuwa shule hiyo imesajiliwa rasmi kuwa kituo cha michezo ya aina mbalimbali. Kilonzo, amesema kuwa kwakuwa kituo hicho ni kipya kwa Sekta ya michezo ni waz...

Mpango wa malezi Kiwangwa umeleta matarajio mapya kwa mtoto Amani

Image
Julieth Ngarabali, Pwani. Katika Mkoa wa Pwani, kijiji cha Kiwangwa, mpango wa malezi, makuzi, na maendeleo ya awali ya mtoto umeleta mabadiliko makubwa kwa mtoto Amani Juma mwenye umri wa miaka saba. Amani ambaye alikumbwa na changamoto za afya na elimu kutokana na ukosefu wa rasilimali, ameweza kupambana na utapiamlo na sasa anaendelea vizuri katika masomo yake. Kwa msaada wa huduma za afya na lishe bora zilizotolewa kupitia kliniki za watoto na elimu ya malezi, Amani anaonekana kuwa na maendeleo ya kuridhisha. Fatuma Juma (43) ni mama mzazi wa mtoto huyo anasema  Amani alikumbwa na changamoto za afya na elimu kutokana na ukosefu wa rasilimali na huduma bora, hii ilimfanya kuchelewa pia kuanza shule na kuwa na matatizo ya kiafya kwani alipata utapiamlo miaka mitano  iliyopita. "'mwaka 2018 nilijifungua lakini baada ya mwaka mmoja niligudua kupitia kwa wataalamu wa afya wa kituo cha afya Lugoba kuwa Amani ana uzito mdogo sana usioendana na umri wake''amesema  Anasem...