MOUNT CALVARY SPOTRS ACADEMY YAIOMBA TFF KUSAIDIA VIFAA VYA MICHEZO, YAPANIA KUIBUA VIPAJI VYA WANAFUNZI WAO
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
Na. Gustaphu Haule, Pwani
SHULE ya michezo ya Mount Calvary Sports Academy iliyopo Kiluvya kwa Komba Kata Kibamba Manispaa ya Ubungo Jijini Dar es Salaam imeliomba Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) kuona namna ya kusaidia vifaa vya michezo katika Shule hiyo.
Kocha wa mpira wa miguu kutoka Shule ya mchepuo wa michezo Mount Calvary Sports Academy Christopher Mjema akiwa na timu ya wanafunzi wa darasa la Saba na timu ya madarasa ya chini katika mchezo uliopigwa juzi shuleni hapo .
Aidha, mbali na kuiomba TFF lakini pia uongozi wa Shule hiyo imewaomba wadau na wafadhili mbalimbali kujitokeza katika kusaidia changamoto za kimichezo katika Shule hiyo.
Meneja wa Shule hiyo Erick Kilonzo, akizungumza na mwandishi wa habari katika mahafali ya darasa la Saba yaliyofanyika Shuleni hapo hivi karibuni ambapo amesema kuwa shule hiyo imesajiliwa rasmi kuwa kituo cha michezo ya aina mbalimbali.
Kilonzo, amesema kuwa kwakuwa kituo hicho ni kipya kwa Sekta ya michezo ni wazi kuwa zipo changamoto za ukosefu wa vifaa vya michezo ikiwemo jezi,mipira ,viatu na hata miundombinu ya viwanja kwani viwanja vilivyopo vinahitaji maboresho.
Amesema kuwa, lengo la kuanzisha kituo cha michezo shuleni hapo ni kukuza vipaji vya wanafunzi wanaosoma shuleni hapo ambapo amewaomba wazazi kuhakikisha watoto wenye vipaji wanapelekwa Shuleni hapo
Kilonzo, ameongeza kuwa mtoto ambaye ametokea katika familia yenye kipato duni atapata nafasi ya kuibuliwa kipaji chake bure bila malipo na wale ambao wanataka kusoma basi malipo yake mengine yatabebwa na shule.
Mhadhiri wa chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Frida Ilomo mwenye skafu kulia akiwa na viongozi wa Shule ya Mount Calvary Sports Academy pamoja na timu ya wanafunzi wa darasa la Saba katika mchezo wao uliopigwa Kwa kuwakutanisha wanafunzi wa madarasa ya chini katika Shule hiyo
"Watoto wenye vipaji ambao hawana uwezo wa kifedha tunawachukua na kuwasomesha bure au kwa kulipa nusu ya ada kwakuwa malengo yetu ni kusaidia katika kuibua vipaji vya michezo kwa wanafunzi.
Kilonzo, ameongeza kuwa kwasasa tayari wamempa Mwalimu wa michezo mwenye sifa na vigezo aliyefundisha timu kubwa Christopher Mjema ambaye tayari ameshaanza kazi ya kutekeleza jukumu hilo.
"Mount Calvary Sports Academy tumemwajiri Christopher Mjema kuwa Mwalimu wa michezo (Kocha) katika Shule yetu na tunaimani kwa uzoefu wake tutafika mbali katika michezo hasa katika kuibua vipaji kwa wanafunzi wetu na hata vijana wengine wanajifunza michezo hapa Shuleni,"amesema Kilonzo.
Kwa upande wake Mwalimu wa michezo wa Shule hiyo Christopher Mjema, amesema kuwa ratiba ya michezo shuleni hapo ipo sawa kwani hakuna muingiliano wa masomo na michezo ambapo kwa wiki michezo hufanyika mara mbili mpaka tatu .
Kocha wa michezo katika Shule Mount Calvary Sports Academy Christopher Mjema (katikati) akimueleza Mhadhiri wa chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Frida Ilomo juu ya umuhimu wa kutoa vyeti kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika mpira wa miguu shuleni hapo
Mjema amesema kazi yake kubwa ni kuibua vipaji vya mpira wa miguu na michezo mingine na kwamba michezo hiyo inaanza kufundishwa tangu wanafunzi wa awali mpaka darasa la Saba.
"Nawakaribisha wazazi kuleta wanafunzi wao hapa Mount Calvary Sports Academy kwani mtoto akija hapa anapata faida ya kuibuliwa kipaji chake na faida nyingine ni kufundishwa darasani na walimu wenye uzoefu mkubwa," amesema Mjema
Mjema mbali na kuwa Kocha wa michezo lakini hapo awali ameshawai kuwa Katibu wa Chama Cha Mpira wa Miguu Wilaya Kibaha (Kibaha) , mwenyekiti kamati ya mashindano Chama Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (Corefa) na nafasi mbalimbali za michezo.
Hatahivyo, kutokana na hali hiyo Mhadhiri wa chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Frida Ilomo ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo amesema changamoto ya vifaa vya michezo ameichukua na atakwenda kuifanyiakazi
Kocha wa mpira wa miguu katika Shule ya Mount Calvary Sports Academy iliyopo Kiluvya kwa Komba Ubungo Jijini Dar es Salaam Christopher Mjema akimuongoza Mhadhiri wa chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Frida Ilomo pamoja na viongozi wa Shule hiyo kukagua timu za michezo za Shule hiyo katika mahafali ya darasa la Saba yaliyofanyika Shuleni hapo juzi
Ilomo, amesema kuwa ifikapo mwaka 2025 vifaa vingi vya michezo vitakuwa vimepatikana shuleni hapo huku akiomba wafadhili wengine kujitokeza.
Na Gustaphu Haule, Pwani CHAMA Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) kimetoa tuzo kwa wachezaji na wadau mbalimbali waliochangia kwa namna au nyingine katika kuendeleza mchezo wa mpira wa Miguu katika msimu wa mwaka 2024/2025. Hafla hiyo imefanyika Agosti 9, 2025 katika ukumbi wa Maisha Plus uliopo karibu na ofisi ya Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani ambapo mgeni rasmi katika hafla hiyo Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Pwani. Katibu Siasa , Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani David Mramba (Kulia)akitoa tuzo kwa mmoja wa wadau wa michezo waliofanya vizuri katika msimu wa mwaka 2023/2024. Katibu Siasa , Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani David Mramba (Kulia)akitoa tuzo kwa mmoja wa wadau wa michezo waliofanya vizuri katika msimu wa mwaka 2023/2024. Zaidi ya wadau 50 walishiriki hafla hiyo wakiwemo waamuzi wa mpira wa miguu, wachezaji wa mpira wa miguu ,viongozi wa vyama vya miche...
Na Gustaphu Haule, Pwani WIZARA ya afya Kitengo cha Sikoseli imesema kuwa ugonjwa wa Selimundu (Sickle Cell) sio ugonjwa wa kurogwa kama ambavyo jamii inachukulia lakini ugonjwa huo ni wakurithi kutoka kwa mzazi mmoja kwenda kwa mzazi mwingine. Imesema ili kujiepusha na ugonjwa huo ni vyema kabla ya kuingia katika mahusiano jamii inapaswa kuchukua hatua ya kwenda kupima vinasaba vya ugonjwa na endapo watakuwa salama wanaweza kuoana na hatimaye kujenga familia salama isiyo na ugonjwa huo wa Selimundu (Sickle Cell). Daktari Bingwa wa magonjwa ya damu kutoka katika hospitali ya Amana iliyopo Jijini Dar es Salaam Jamila Makame, ametoa kauli hiyo katika semina ya siku moja kwa baadhi ya Waandishi wa Mkoa wa Pwani iliyolenga masuala ya ugonjwa wa Selimundu Semina hiyo iliyofanyika Agosti 12, 2025 katika kituo cha afya Mkoani kilichopo Manispaa ya Kibaha iliwajumuisha baadhi ya Waandishi wa habari ambapo Dr.Makame amesema "Sickle Cell" ni ugonjwa wa kurithi ambao chanzo...
Na Gustaphu Haule,Pwani KATIBU Tawala wa Mkoa wa Pwani Pili Mnyema, ameanza ziara yake ya kikazi katika Halmashauri za Mkoa wa Pwani kwa kutembelea Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha. Katika ziara hiyo, Mnyema amesisitiza umuhimu wa ubunifu katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ili kuongeza mapato ya Halmashauri pamoja na Mkoa kwa ujumla. Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Pili Mnyema katika kikao na watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha alipofanya ziara ya kuzungumza na watumishi wa Manispaa hiyo Agosti 12, 2025 "Naomba tumuunge mkono mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kubuni vyanzo vipya vya mapato na hii ni miongoni mwa maagizo niliyopatiwa ili kusaidia kuongeza mapato ya Mkoa wetu," amesema Mnyema. Aidha, amempongeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Kibaha Dkt.Rogers Shemwelekwa kwa kuendelea kubuni na kusimamia miradi mbalimbali yenye tija, ambayo imesababisha ongezeko la mapato ya Manispaa hiyo kila mwaka. ...
Comments
Post a Comment