MOUNT CALVARY SPOTRS ACADEMY YAIOMBA TFF KUSAIDIA VIFAA VYA MICHEZO, YAPANIA KUIBUA VIPAJI VYA WANAFUNZI WAO
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
Na. Gustaphu Haule, Pwani
SHULE ya michezo ya Mount Calvary Sports Academy iliyopo Kiluvya kwa Komba Kata Kibamba Manispaa ya Ubungo Jijini Dar es Salaam imeliomba Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) kuona namna ya kusaidia vifaa vya michezo katika Shule hiyo.
Kocha wa mpira wa miguu kutoka Shule ya mchepuo wa michezo Mount Calvary Sports Academy Christopher Mjema akiwa na timu ya wanafunzi wa darasa la Saba na timu ya madarasa ya chini katika mchezo uliopigwa juzi shuleni hapo .
Aidha, mbali na kuiomba TFF lakini pia uongozi wa Shule hiyo imewaomba wadau na wafadhili mbalimbali kujitokeza katika kusaidia changamoto za kimichezo katika Shule hiyo.
Meneja wa Shule hiyo Erick Kilonzo, akizungumza na mwandishi wa habari katika mahafali ya darasa la Saba yaliyofanyika Shuleni hapo hivi karibuni ambapo amesema kuwa shule hiyo imesajiliwa rasmi kuwa kituo cha michezo ya aina mbalimbali.
Kilonzo, amesema kuwa kwakuwa kituo hicho ni kipya kwa Sekta ya michezo ni wazi kuwa zipo changamoto za ukosefu wa vifaa vya michezo ikiwemo jezi,mipira ,viatu na hata miundombinu ya viwanja kwani viwanja vilivyopo vinahitaji maboresho.
Amesema kuwa, lengo la kuanzisha kituo cha michezo shuleni hapo ni kukuza vipaji vya wanafunzi wanaosoma shuleni hapo ambapo amewaomba wazazi kuhakikisha watoto wenye vipaji wanapelekwa Shuleni hapo
Kilonzo, ameongeza kuwa mtoto ambaye ametokea katika familia yenye kipato duni atapata nafasi ya kuibuliwa kipaji chake bure bila malipo na wale ambao wanataka kusoma basi malipo yake mengine yatabebwa na shule.
Mhadhiri wa chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Frida Ilomo mwenye skafu kulia akiwa na viongozi wa Shule ya Mount Calvary Sports Academy pamoja na timu ya wanafunzi wa darasa la Saba katika mchezo wao uliopigwa Kwa kuwakutanisha wanafunzi wa madarasa ya chini katika Shule hiyo
"Watoto wenye vipaji ambao hawana uwezo wa kifedha tunawachukua na kuwasomesha bure au kwa kulipa nusu ya ada kwakuwa malengo yetu ni kusaidia katika kuibua vipaji vya michezo kwa wanafunzi.
Kilonzo, ameongeza kuwa kwasasa tayari wamempa Mwalimu wa michezo mwenye sifa na vigezo aliyefundisha timu kubwa Christopher Mjema ambaye tayari ameshaanza kazi ya kutekeleza jukumu hilo.
"Mount Calvary Sports Academy tumemwajiri Christopher Mjema kuwa Mwalimu wa michezo (Kocha) katika Shule yetu na tunaimani kwa uzoefu wake tutafika mbali katika michezo hasa katika kuibua vipaji kwa wanafunzi wetu na hata vijana wengine wanajifunza michezo hapa Shuleni,"amesema Kilonzo.
Kwa upande wake Mwalimu wa michezo wa Shule hiyo Christopher Mjema, amesema kuwa ratiba ya michezo shuleni hapo ipo sawa kwani hakuna muingiliano wa masomo na michezo ambapo kwa wiki michezo hufanyika mara mbili mpaka tatu .
Kocha wa michezo katika Shule Mount Calvary Sports Academy Christopher Mjema (katikati) akimueleza Mhadhiri wa chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Frida Ilomo juu ya umuhimu wa kutoa vyeti kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika mpira wa miguu shuleni hapo
Mjema amesema kazi yake kubwa ni kuibua vipaji vya mpira wa miguu na michezo mingine na kwamba michezo hiyo inaanza kufundishwa tangu wanafunzi wa awali mpaka darasa la Saba.
"Nawakaribisha wazazi kuleta wanafunzi wao hapa Mount Calvary Sports Academy kwani mtoto akija hapa anapata faida ya kuibuliwa kipaji chake na faida nyingine ni kufundishwa darasani na walimu wenye uzoefu mkubwa," amesema Mjema
Mjema mbali na kuwa Kocha wa michezo lakini hapo awali ameshawai kuwa Katibu wa Chama Cha Mpira wa Miguu Wilaya Kibaha (Kibaha) , mwenyekiti kamati ya mashindano Chama Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (Corefa) na nafasi mbalimbali za michezo.
Hatahivyo, kutokana na hali hiyo Mhadhiri wa chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Frida Ilomo ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo amesema changamoto ya vifaa vya michezo ameichukua na atakwenda kuifanyiakazi
Kocha wa mpira wa miguu katika Shule ya Mount Calvary Sports Academy iliyopo Kiluvya kwa Komba Ubungo Jijini Dar es Salaam Christopher Mjema akimuongoza Mhadhiri wa chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Frida Ilomo pamoja na viongozi wa Shule hiyo kukagua timu za michezo za Shule hiyo katika mahafali ya darasa la Saba yaliyofanyika Shuleni hapo juzi
Ilomo, amesema kuwa ifikapo mwaka 2025 vifaa vingi vya michezo vitakuwa vimepatikana shuleni hapo huku akiomba wafadhili wengine kujitokeza.
Na Gustaphu Haule, Pwani MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge amewaongoza wakazi wa Mtaa wa Mkoani" A" uliopo Kata ya Tumbi Halmashauri ya Mji Kibaha katika zoezi la kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura lililoanza leo Mkoani Pwani. Aidha, Kunenge akiwa katika kituo hicho aliambatana na Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Rashid Mchatta, Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson Saimoni pamoja na mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Rogers Shemwelekwa. Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge akiwaongoza Wananchi wa Mtaa wa Mkoani "A", Kata ya Tumbi Halmashauri ya Mji Kibaha kujiandikisha katika daftari la wapiga kura zoezi ambalo limeanza leo Oktoba 11 hadi Oktoba 20 mwaka huu Akizungumza mara baada ya kujiandikisha katika kituo hicho Kunenge amesema kuwa zoezi hilo limeanza kufanyika Mkoa wa Pwani leo Oktoba 11 na litamalizika Oktoba 20 mwaka huu. Kunenge amesema kuwa kufanyika kwa zoezi hilo ni maandalizi ya kuelekea katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajia ...
Na Gustaphu Haule,Pwani BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Mji Kibaha limempongeza mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Dkt.Rogers Shemwelekwa kwa usimamizi mzuri katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Shemwelekwa ameshushiwa pongezi hizo Aprili 29, 2025 katika kikao cha Baraza hilo kilichofanyika katika Ukumbi wa soko kubwa la kisasa (Kibaha Shopping Mall) ambapo kwa kiasi kikubwa lilikuwa Baraza za kuonyesha mafanikio katika kipindi cha mwaka 2020/2025. Pongezi hizo zilikuja mara baada ya Wenyeviti wa kamati mbalimbali ikiwemo kamati ya fedha, kamati ya Mipango Miji, kamati ya Afya na Elimu pamoja na kamati ya huduma za jamii kueleza mafanikio ndani ya kipindi hicho cha miaka mitano. Mwenyekiti wa kamati ya fedha Karim Ntambo,amesema kuwa katika kipindi cha miaka mitano Manispaa ya Kibaha Mjini imepata mafanikio makubwa ambapo moja ya mafanikio hayo ni pamoja na ongezeko la mapato. Ntambo, amesema kuwa wakati wanaingia madarakani ukusanyaji mapato ulikuwa ni kiasi cha Sh.bilioni 4 la...
Na Gustaphu Haule,Pwani RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan ameridhia Halmashauri ya Mji Kibaha iliyopo Mkoani Pwani kupandishwa hadi na kuwa Manispaa. Uamuzi huo umetangazwa leo Januari 27 na Waziri wa Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa Mjini Kibaha. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Mohamed Mchengerwa akizungumza katika mkutano wa CCM uliofanyika Januari 27 katika viwanja vya stendi ya zamani Mailimoja Kibaha Mkoani Pwani. Mchengerwa, ametangaza hilo wakati akizungumza na wanachama wa CCM pamoja na Wananchi katika mkutano mkubwa wa kuunga mkono maazimio ya mkutano Mkuu wa CCM Taifa uliomteua Rais Samia kuwa mgombea wa Urais mwaka 2025. Wanachama wa CCM pamoja na Wananchi mbalimbali walioshiriki mkutano wa kuunga mkono azimio la Mkutano Mkuu wa Taifa CCM la kumteua Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea pekee wa Urais kupitia CCM katika uchaguzi wa mwaka 2025, Mkutan...
Comments
Post a Comment