MOUNT CALVARY SPOTRS ACADEMY YAIOMBA TFF KUSAIDIA VIFAA VYA MICHEZO, YAPANIA KUIBUA VIPAJI VYA WANAFUNZI WAO
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
Na. Gustaphu Haule, Pwani
SHULE ya michezo ya Mount Calvary Sports Academy iliyopo Kiluvya kwa Komba Kata Kibamba Manispaa ya Ubungo Jijini Dar es Salaam imeliomba Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) kuona namna ya kusaidia vifaa vya michezo katika Shule hiyo.
Kocha wa mpira wa miguu kutoka Shule ya mchepuo wa michezo Mount Calvary Sports Academy Christopher Mjema akiwa na timu ya wanafunzi wa darasa la Saba na timu ya madarasa ya chini katika mchezo uliopigwa juzi shuleni hapo .
Aidha, mbali na kuiomba TFF lakini pia uongozi wa Shule hiyo imewaomba wadau na wafadhili mbalimbali kujitokeza katika kusaidia changamoto za kimichezo katika Shule hiyo.
Meneja wa Shule hiyo Erick Kilonzo, akizungumza na mwandishi wa habari katika mahafali ya darasa la Saba yaliyofanyika Shuleni hapo hivi karibuni ambapo amesema kuwa shule hiyo imesajiliwa rasmi kuwa kituo cha michezo ya aina mbalimbali.
Kilonzo, amesema kuwa kwakuwa kituo hicho ni kipya kwa Sekta ya michezo ni wazi kuwa zipo changamoto za ukosefu wa vifaa vya michezo ikiwemo jezi,mipira ,viatu na hata miundombinu ya viwanja kwani viwanja vilivyopo vinahitaji maboresho.
Amesema kuwa, lengo la kuanzisha kituo cha michezo shuleni hapo ni kukuza vipaji vya wanafunzi wanaosoma shuleni hapo ambapo amewaomba wazazi kuhakikisha watoto wenye vipaji wanapelekwa Shuleni hapo
Kilonzo, ameongeza kuwa mtoto ambaye ametokea katika familia yenye kipato duni atapata nafasi ya kuibuliwa kipaji chake bure bila malipo na wale ambao wanataka kusoma basi malipo yake mengine yatabebwa na shule.
Mhadhiri wa chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Frida Ilomo mwenye skafu kulia akiwa na viongozi wa Shule ya Mount Calvary Sports Academy pamoja na timu ya wanafunzi wa darasa la Saba katika mchezo wao uliopigwa Kwa kuwakutanisha wanafunzi wa madarasa ya chini katika Shule hiyo
"Watoto wenye vipaji ambao hawana uwezo wa kifedha tunawachukua na kuwasomesha bure au kwa kulipa nusu ya ada kwakuwa malengo yetu ni kusaidia katika kuibua vipaji vya michezo kwa wanafunzi.
Kilonzo, ameongeza kuwa kwasasa tayari wamempa Mwalimu wa michezo mwenye sifa na vigezo aliyefundisha timu kubwa Christopher Mjema ambaye tayari ameshaanza kazi ya kutekeleza jukumu hilo.
"Mount Calvary Sports Academy tumemwajiri Christopher Mjema kuwa Mwalimu wa michezo (Kocha) katika Shule yetu na tunaimani kwa uzoefu wake tutafika mbali katika michezo hasa katika kuibua vipaji kwa wanafunzi wetu na hata vijana wengine wanajifunza michezo hapa Shuleni,"amesema Kilonzo.
Kwa upande wake Mwalimu wa michezo wa Shule hiyo Christopher Mjema, amesema kuwa ratiba ya michezo shuleni hapo ipo sawa kwani hakuna muingiliano wa masomo na michezo ambapo kwa wiki michezo hufanyika mara mbili mpaka tatu .
Kocha wa michezo katika Shule Mount Calvary Sports Academy Christopher Mjema (katikati) akimueleza Mhadhiri wa chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Frida Ilomo juu ya umuhimu wa kutoa vyeti kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika mpira wa miguu shuleni hapo
Mjema amesema kazi yake kubwa ni kuibua vipaji vya mpira wa miguu na michezo mingine na kwamba michezo hiyo inaanza kufundishwa tangu wanafunzi wa awali mpaka darasa la Saba.
"Nawakaribisha wazazi kuleta wanafunzi wao hapa Mount Calvary Sports Academy kwani mtoto akija hapa anapata faida ya kuibuliwa kipaji chake na faida nyingine ni kufundishwa darasani na walimu wenye uzoefu mkubwa," amesema Mjema
Mjema mbali na kuwa Kocha wa michezo lakini hapo awali ameshawai kuwa Katibu wa Chama Cha Mpira wa Miguu Wilaya Kibaha (Kibaha) , mwenyekiti kamati ya mashindano Chama Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (Corefa) na nafasi mbalimbali za michezo.
Hatahivyo, kutokana na hali hiyo Mhadhiri wa chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Frida Ilomo ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo amesema changamoto ya vifaa vya michezo ameichukua na atakwenda kuifanyiakazi
Kocha wa mpira wa miguu katika Shule ya Mount Calvary Sports Academy iliyopo Kiluvya kwa Komba Ubungo Jijini Dar es Salaam Christopher Mjema akimuongoza Mhadhiri wa chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Frida Ilomo pamoja na viongozi wa Shule hiyo kukagua timu za michezo za Shule hiyo katika mahafali ya darasa la Saba yaliyofanyika Shuleni hapo juzi
Ilomo, amesema kuwa ifikapo mwaka 2025 vifaa vingi vya michezo vitakuwa vimepatikana shuleni hapo huku akiomba wafadhili wengine kujitokeza.
Na Gustaphu Haule, Pwani MWENYEKITI wa Kitongoji cha Kwakibosha kilichopo Kata ya Mapinga Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani Shaban Athumani amewataka vijana kuacha kutumika na watu wachache wenye nia ovyo ya kutaka kuharibu amani na utulivu hapa nchini. Athumani ametoa wito huo katika mdahalo maalum wa kuwajengea uwezo vijana juu ya kukabiliana na vitendo viovu sambamba na kuwahamasisha vijana kulinda amani ya Taifa iliyoasisiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Mmoja wa Vijana wa Kitongoji cha Kwakibosha Mohamed Omary akichangia mada katika mdahalo huo Mdahalo huo umefanyika Juni 14, 2025 katika Kitongoji hicho na kuwashirikisha vijana zaidi ya 500 kutoka makundi mbalimbali wakiwemo bodaboda,mama lishe ,wapaka rangi na hata vijana kutoka UVCCM . Athumani, amesema kuwa mwaka 2025 ni mwaka wa uchaguzi mkuu unaokwenda kuwaweka madarakani viongozi akiwemo Rais, Wabunge na Madiwani na hiyo ndio fursa kwa vijana kuchagua viongozi wanaowataka. Mwenyekiti wa Kitongoji...
Na Gustaphu Haule, Pwani WIZARA ya afya Kitengo cha Sikoseli imesema kuwa ugonjwa wa Selimundu (Sickle Cell) sio ugonjwa wa kurogwa kama ambavyo jamii inachukulia lakini ugonjwa huo ni wakurithi kutoka kwa mzazi mmoja kwenda kwa mzazi mwingine. Imesema ili kujiepusha na ugonjwa huo ni vyema kabla ya kuingia katika mahusiano jamii inapaswa kuchukua hatua ya kwenda kupima vinasaba vya ugonjwa na endapo watakuwa salama wanaweza kuoana na hatimaye kujenga familia salama isiyo na ugonjwa huo wa Selimundu (Sickle Cell). Daktari Bingwa wa magonjwa ya damu kutoka katika hospitali ya Amana iliyopo Jijini Dar es Salaam Jamila Makame, ametoa kauli hiyo katika semina ya siku moja kwa baadhi ya Waandishi wa Mkoa wa Pwani iliyolenga masuala ya ugonjwa wa Selimundu Semina hiyo iliyofanyika Agosti 12, 2025 katika kituo cha afya Mkoani kilichopo Manispaa ya Kibaha iliwajumuisha baadhi ya Waandishi wa habari ambapo Dr.Makame amesema "Sickle Cell" ni ugonjwa wa kurithi ambao chanzo...
Na Gustaphu Haule, Pwani KAMPUNI ya Taifa Gas Tanzania Limited imeendelea kuunga mkono kampeni ya Nishati Safi ya Kupikia ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa elimu na kuhamasisha wananchi juu ya matumizi ya gas ya kupikia inayouzwa na Taifa Gas. Hii ni Gesi ya Petroli iliyoyeyushwa "Liquefied Petroleum Gas" (LPG). Taifa Gas Tanzania imetoa elimu hiyo leo Juni 7, 2025 katika eneo la Loliondo katika Manispaa ya Kibaha Mkoani Pwani ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku ya Nishati Safi Duniani (Gas). Baadhi ya wananchi wa Kibaha Loliondo wakipata elimu juu ya matumizi ya nishati Safi ya kupikia kutoka kwa wafanyakazi wa Taifa Gas Tanzania ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya siku ya gesi Duniani. Meneja Uhusiano na Masoko kutoka Taifa Gas Kitengo cha Nishati Safi Anjellah Bhoke ameongoza kampeni hiyo ambapo amesema lengo la Taifa Gas ni kuhakikisha wanaendelea kumuunga mkono Rais Samia juu ya matumizi ya nishati Safi hapa nchini. "Leo tupo hapa Kibaha ku...
Comments
Post a Comment