DR.CHAKOU TINDWA AKAGUA JENGO LA KITEGA UCHUMI CCM MKOA WA PWANI, AELEZA KURIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WAKE
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
Na. Gustaphu Haule, Pwani
MJUMBE wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Pwani na makamu mwenyekiti wa Kamati ya uchumi ya CCM Mkoa Pwani Dr.Chakou Tindwa amefanya ziara maalum ya kutembelea na kukagua mradi wa jengo la kitega uchumi la CCM Mkoa wa Pwani.
Dr.Tindwa amefanya ziara hiyo leo Septamba 13 katika jengo hilo lililopo Kibaha Mjini ambapo pamoja na mambo mengine ameeleza kuridhishwa na kasi ya ujenzi wa jengo hilo .
Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Pwani na makamu mwenyekiti wa kamati ya uchumi Dr.Chakou Tindwa akikagua jengo la kitega uchumi la Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani katika ziara yake aliyoifanya leo Septemba 13.2024.
Akiwa katika jengo hilo Dr .Tindwa amesema kuwa anatamani kuona jengo hilo linakamilika mapema ili kusudi kukisaidia chama kuondokana na usumbufu wa kutumia fedha nyingi kukodi kumbi za watu wengine Kwa ajili ya kufanyia mikutano ya Chama.
"Mimi ni makamu mwenyekiti wa kamati ya uchumi ya CCM Mkoa wa Pwani, hivyo niliona ni vyema leo nikafika hapa kwa ajili ya kukagua jengo hili na kuona maendeleo yake lakini hatahivyo nimeridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa jengo letu,"amesema Dr.Tindwa.
Dr.Tindwa amesema kuwa pamoja na kuchangia fedha kiasi cha Sh.milioni 120 katika harambee iliyofanyika hivi karibuni Jijini Dar es Salaam lakini pia kama kutakuwa na uhitaji mwingine atakuwa tayari kuchangia ili kusudi jengo hilo liweze kukamilika kama iliyokusudiwa.
Mjumbe wa kamati ya Sisa ya Chama Cha Mapinduzi ( CCM) Mkoa wa Pwani na makamu mwenyekiti wa kamati ya uchumi mkoa Dr.Chakou Tindwa akiwa katika jengo la kitega uchumi la CCM Mkoa wa Pwani leo Septemba 13, 2024.
Amewaomba, viongozi wa CCM pamoja na wadau wengine wa maendeleo kuendelea kushirikiana kwa ajili ya kuhakikisha Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani kinapata miradi mingi zaidi ambayo itasaidia kuondoa utegemezi .
Aidha , mwishoni mwa wiki iliyopita Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Taifa Ally Hapo,alitembelea jengo hilo na kusifu jitihada za kamati ya Siasa Mkoa wa Pwani kwa kubuni mradi ambao utakuwa na manufaa kwa chama.
Ziara ya Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Taifa Ally Hapi katika jengo la kitega uchumi la CCM Mkoa wa Pwani aliyoifanya hivi karibuni.
Hapo, amesema kama kila Mkoa kutakuwa na majengo kama hayo ni wazi kuwa CCM itakuwa imara zaidi ambapo ametaka mikoa mingine kuiga mfano huo.
Na Gustaphu Haule,Pwani BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Mji Kibaha limempongeza mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Dkt.Rogers Shemwelekwa kwa usimamizi mzuri katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Shemwelekwa ameshushiwa pongezi hizo Aprili 29, 2025 katika kikao cha Baraza hilo kilichofanyika katika Ukumbi wa soko kubwa la kisasa (Kibaha Shopping Mall) ambapo kwa kiasi kikubwa lilikuwa Baraza za kuonyesha mafanikio katika kipindi cha mwaka 2020/2025. Pongezi hizo zilikuja mara baada ya Wenyeviti wa kamati mbalimbali ikiwemo kamati ya fedha, kamati ya Mipango Miji, kamati ya Afya na Elimu pamoja na kamati ya huduma za jamii kueleza mafanikio ndani ya kipindi hicho cha miaka mitano. Mwenyekiti wa kamati ya fedha Karim Ntambo,amesema kuwa katika kipindi cha miaka mitano Manispaa ya Kibaha Mjini imepata mafanikio makubwa ambapo moja ya mafanikio hayo ni pamoja na ongezeko la mapato. Ntambo, amesema kuwa wakati wanaingia madarakani ukusanyaji mapato ulikuwa ni kiasi cha Sh.bilioni 4 la...
Na Gustaphu Haule,Pwani MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge,amelipongeza Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Mji Kibaha kupitia mkurugenzi wake Dkt.Rogers Shemwelekwa kwa kazi nzuri ya kutekeleza miradi ya maendeleo iliyofanywa kwa kipindi cha mwaka 2020/2025. Aidha, Kunenge amesisitiza Baraza hilo kuwa katika kipindi cha mwaka 2025 /2030 wahakikishe wanapanga miradi yenye kipaumbele ili kuleta matokeo chanya katika jamii. Kunenge,ameyasema hayo Juni 16,2025 wakati akizungumza katika kikao maalum cha Baraza la Madiwani kwa ajili ya kujibu hoja za mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali (CAG)kikao ambacho kimefanyika katika Halmashauri ya Mji Kibaha. Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Musa Ndomba akizungumza katika kikao cha Baraza maalum la kujibu hoja za mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) kilichofanyika Juni 16,2025 Amesema kuwa Kibaha Mjini imekuwa Halmashauri ya kuigwa kwakuwa katika kipindi kifupi tangu mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Dkt.Shemwelekwa kui...
Na Gustaphu Haule Pwani WAKALA ya Barabara Tanzania ( TANROADS) imetoa ufafanuzi kuhusu gari la mizigo la kampuni ya Simba Logistics Limited lililozuiliwa katika kituo cha Mizani ya Vigwaza Mkoani Pwani baada ya kupimwa na kukutwa limezidisha uzito. Meneja wa TANROADS Mkoa wa Pwani Mhandisi Baraka Mwambage,amesema kuwa gari la Simba Logistics Limited lilifika katika kituo cha Mizani ya Vigwaza Machi 13 mwaka huu likitokea katika nchi jirani ya Zambia likiendeshwa na Pamela Bukumbi. Meneja Wakala ya Barabara (TANROADS) Mkoa wa Pwani Mhandisi Baraka Mwambage, akitoa ufafanuzi kwa Waandishi wa habari kuhusu kutozwa faini kwa gari la mizigo la Simba Logistics Machi 13,2025 katika kituo cha Mizani ya Vigwaza iliyopo Mkoani Pwani . Amesema gari hilo lilikuwa limebeba mzigo wa Madini ya Shaba( Copper ) na baada ya kupimwa lilibainika kuzidi uzito na hivyo kupaswa kulipa gharama ya Sh. 900,000 za Kitanzania. Mwambage, amesema kuwa shughuli za upimaji na udhibiti wa uzito...
Comments
Post a Comment