DR.CHAKOU TINDWA AKAGUA JENGO LA KITEGA UCHUMI CCM MKOA WA PWANI, AELEZA KURIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WAKE
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
Na. Gustaphu Haule, Pwani
MJUMBE wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Pwani na makamu mwenyekiti wa Kamati ya uchumi ya CCM Mkoa Pwani Dr.Chakou Tindwa amefanya ziara maalum ya kutembelea na kukagua mradi wa jengo la kitega uchumi la CCM Mkoa wa Pwani.
Dr.Tindwa amefanya ziara hiyo leo Septamba 13 katika jengo hilo lililopo Kibaha Mjini ambapo pamoja na mambo mengine ameeleza kuridhishwa na kasi ya ujenzi wa jengo hilo .
Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Pwani na makamu mwenyekiti wa kamati ya uchumi Dr.Chakou Tindwa akikagua jengo la kitega uchumi la Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani katika ziara yake aliyoifanya leo Septemba 13.2024.
Akiwa katika jengo hilo Dr .Tindwa amesema kuwa anatamani kuona jengo hilo linakamilika mapema ili kusudi kukisaidia chama kuondokana na usumbufu wa kutumia fedha nyingi kukodi kumbi za watu wengine Kwa ajili ya kufanyia mikutano ya Chama.
"Mimi ni makamu mwenyekiti wa kamati ya uchumi ya CCM Mkoa wa Pwani, hivyo niliona ni vyema leo nikafika hapa kwa ajili ya kukagua jengo hili na kuona maendeleo yake lakini hatahivyo nimeridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa jengo letu,"amesema Dr.Tindwa.
Dr.Tindwa amesema kuwa pamoja na kuchangia fedha kiasi cha Sh.milioni 120 katika harambee iliyofanyika hivi karibuni Jijini Dar es Salaam lakini pia kama kutakuwa na uhitaji mwingine atakuwa tayari kuchangia ili kusudi jengo hilo liweze kukamilika kama iliyokusudiwa.
Mjumbe wa kamati ya Sisa ya Chama Cha Mapinduzi ( CCM) Mkoa wa Pwani na makamu mwenyekiti wa kamati ya uchumi mkoa Dr.Chakou Tindwa akiwa katika jengo la kitega uchumi la CCM Mkoa wa Pwani leo Septemba 13, 2024.
Amewaomba, viongozi wa CCM pamoja na wadau wengine wa maendeleo kuendelea kushirikiana kwa ajili ya kuhakikisha Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani kinapata miradi mingi zaidi ambayo itasaidia kuondoa utegemezi .
Aidha , mwishoni mwa wiki iliyopita Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Taifa Ally Hapo,alitembelea jengo hilo na kusifu jitihada za kamati ya Siasa Mkoa wa Pwani kwa kubuni mradi ambao utakuwa na manufaa kwa chama.
Ziara ya Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Taifa Ally Hapi katika jengo la kitega uchumi la CCM Mkoa wa Pwani aliyoifanya hivi karibuni.
Hapo, amesema kama kila Mkoa kutakuwa na majengo kama hayo ni wazi kuwa CCM itakuwa imara zaidi ambapo ametaka mikoa mingine kuiga mfano huo.
Na Gustaphu Haule, Pwani CHAMA Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) kimetoa tuzo kwa wachezaji na wadau mbalimbali waliochangia kwa namna au nyingine katika kuendeleza mchezo wa mpira wa Miguu katika msimu wa mwaka 2024/2025. Hafla hiyo imefanyika Agosti 9, 2025 katika ukumbi wa Maisha Plus uliopo karibu na ofisi ya Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani ambapo mgeni rasmi katika hafla hiyo Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Pwani. Katibu Siasa , Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani David Mramba (Kulia)akitoa tuzo kwa mmoja wa wadau wa michezo waliofanya vizuri katika msimu wa mwaka 2023/2024. Katibu Siasa , Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani David Mramba (Kulia)akitoa tuzo kwa mmoja wa wadau wa michezo waliofanya vizuri katika msimu wa mwaka 2023/2024. Zaidi ya wadau 50 walishiriki hafla hiyo wakiwemo waamuzi wa mpira wa miguu, wachezaji wa mpira wa miguu ,viongozi wa vyama vya miche...
Na Gustaphu Haule, Pwani WIZARA ya afya Kitengo cha Sikoseli imesema kuwa ugonjwa wa Selimundu (Sickle Cell) sio ugonjwa wa kurogwa kama ambavyo jamii inachukulia lakini ugonjwa huo ni wakurithi kutoka kwa mzazi mmoja kwenda kwa mzazi mwingine. Imesema ili kujiepusha na ugonjwa huo ni vyema kabla ya kuingia katika mahusiano jamii inapaswa kuchukua hatua ya kwenda kupima vinasaba vya ugonjwa na endapo watakuwa salama wanaweza kuoana na hatimaye kujenga familia salama isiyo na ugonjwa huo wa Selimundu (Sickle Cell). Daktari Bingwa wa magonjwa ya damu kutoka katika hospitali ya Amana iliyopo Jijini Dar es Salaam Jamila Makame, ametoa kauli hiyo katika semina ya siku moja kwa baadhi ya Waandishi wa Mkoa wa Pwani iliyolenga masuala ya ugonjwa wa Selimundu Semina hiyo iliyofanyika Agosti 12, 2025 katika kituo cha afya Mkoani kilichopo Manispaa ya Kibaha iliwajumuisha baadhi ya Waandishi wa habari ambapo Dr.Makame amesema "Sickle Cell" ni ugonjwa wa kurithi ambao chanzo...
Na Gustaphu Haule,Pwani KATIBU Tawala wa Mkoa wa Pwani Pili Mnyema, ameanza ziara yake ya kikazi katika Halmashauri za Mkoa wa Pwani kwa kutembelea Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha. Katika ziara hiyo, Mnyema amesisitiza umuhimu wa ubunifu katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ili kuongeza mapato ya Halmashauri pamoja na Mkoa kwa ujumla. Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Pili Mnyema katika kikao na watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha alipofanya ziara ya kuzungumza na watumishi wa Manispaa hiyo Agosti 12, 2025 "Naomba tumuunge mkono mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kubuni vyanzo vipya vya mapato na hii ni miongoni mwa maagizo niliyopatiwa ili kusaidia kuongeza mapato ya Mkoa wetu," amesema Mnyema. Aidha, amempongeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Kibaha Dkt.Rogers Shemwelekwa kwa kuendelea kubuni na kusimamia miradi mbalimbali yenye tija, ambayo imesababisha ongezeko la mapato ya Manispaa hiyo kila mwaka. ...
Comments
Post a Comment