DR.CHAKOU TINDWA AKAGUA JENGO LA KITEGA UCHUMI CCM MKOA WA PWANI, AELEZA KURIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WAKE
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
Na. Gustaphu Haule, Pwani
MJUMBE wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Pwani na makamu mwenyekiti wa Kamati ya uchumi ya CCM Mkoa Pwani Dr.Chakou Tindwa amefanya ziara maalum ya kutembelea na kukagua mradi wa jengo la kitega uchumi la CCM Mkoa wa Pwani.
Dr.Tindwa amefanya ziara hiyo leo Septamba 13 katika jengo hilo lililopo Kibaha Mjini ambapo pamoja na mambo mengine ameeleza kuridhishwa na kasi ya ujenzi wa jengo hilo .
Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Pwani na makamu mwenyekiti wa kamati ya uchumi Dr.Chakou Tindwa akikagua jengo la kitega uchumi la Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani katika ziara yake aliyoifanya leo Septemba 13.2024.
Akiwa katika jengo hilo Dr .Tindwa amesema kuwa anatamani kuona jengo hilo linakamilika mapema ili kusudi kukisaidia chama kuondokana na usumbufu wa kutumia fedha nyingi kukodi kumbi za watu wengine Kwa ajili ya kufanyia mikutano ya Chama.
"Mimi ni makamu mwenyekiti wa kamati ya uchumi ya CCM Mkoa wa Pwani, hivyo niliona ni vyema leo nikafika hapa kwa ajili ya kukagua jengo hili na kuona maendeleo yake lakini hatahivyo nimeridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa jengo letu,"amesema Dr.Tindwa.
Dr.Tindwa amesema kuwa pamoja na kuchangia fedha kiasi cha Sh.milioni 120 katika harambee iliyofanyika hivi karibuni Jijini Dar es Salaam lakini pia kama kutakuwa na uhitaji mwingine atakuwa tayari kuchangia ili kusudi jengo hilo liweze kukamilika kama iliyokusudiwa.
Mjumbe wa kamati ya Sisa ya Chama Cha Mapinduzi ( CCM) Mkoa wa Pwani na makamu mwenyekiti wa kamati ya uchumi mkoa Dr.Chakou Tindwa akiwa katika jengo la kitega uchumi la CCM Mkoa wa Pwani leo Septemba 13, 2024.
Amewaomba, viongozi wa CCM pamoja na wadau wengine wa maendeleo kuendelea kushirikiana kwa ajili ya kuhakikisha Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani kinapata miradi mingi zaidi ambayo itasaidia kuondoa utegemezi .
Aidha , mwishoni mwa wiki iliyopita Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Taifa Ally Hapo,alitembelea jengo hilo na kusifu jitihada za kamati ya Siasa Mkoa wa Pwani kwa kubuni mradi ambao utakuwa na manufaa kwa chama.
Ziara ya Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Taifa Ally Hapi katika jengo la kitega uchumi la CCM Mkoa wa Pwani aliyoifanya hivi karibuni.
Hapo, amesema kama kila Mkoa kutakuwa na majengo kama hayo ni wazi kuwa CCM itakuwa imara zaidi ambapo ametaka mikoa mingine kuiga mfano huo.
Na Gustaphu Haule, Pwani MWENYEKITI wa Kitongoji cha Kwakibosha kilichopo Kata ya Mapinga Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani Shaban Athumani amewataka vijana kuacha kutumika na watu wachache wenye nia ovyo ya kutaka kuharibu amani na utulivu hapa nchini. Athumani ametoa wito huo katika mdahalo maalum wa kuwajengea uwezo vijana juu ya kukabiliana na vitendo viovu sambamba na kuwahamasisha vijana kulinda amani ya Taifa iliyoasisiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Mmoja wa Vijana wa Kitongoji cha Kwakibosha Mohamed Omary akichangia mada katika mdahalo huo Mdahalo huo umefanyika Juni 14, 2025 katika Kitongoji hicho na kuwashirikisha vijana zaidi ya 500 kutoka makundi mbalimbali wakiwemo bodaboda,mama lishe ,wapaka rangi na hata vijana kutoka UVCCM . Athumani, amesema kuwa mwaka 2025 ni mwaka wa uchaguzi mkuu unaokwenda kuwaweka madarakani viongozi akiwemo Rais, Wabunge na Madiwani na hiyo ndio fursa kwa vijana kuchagua viongozi wanaowataka. Mwenyekiti wa Kitongoji...
Na Gustaphu Haule, Pwani KAMPUNI ya Taifa Gas Tanzania Limited imeendelea kuunga mkono kampeni ya Nishati Safi ya Kupikia ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa elimu na kuhamasisha wananchi juu ya matumizi ya gas ya kupikia inayouzwa na Taifa Gas. Hii ni Gesi ya Petroli iliyoyeyushwa "Liquefied Petroleum Gas" (LPG). Taifa Gas Tanzania imetoa elimu hiyo leo Juni 7, 2025 katika eneo la Loliondo katika Manispaa ya Kibaha Mkoani Pwani ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku ya Nishati Safi Duniani (Gas). Baadhi ya wananchi wa Kibaha Loliondo wakipata elimu juu ya matumizi ya nishati Safi ya kupikia kutoka kwa wafanyakazi wa Taifa Gas Tanzania ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya siku ya gesi Duniani. Meneja Uhusiano na Masoko kutoka Taifa Gas Kitengo cha Nishati Safi Anjellah Bhoke ameongoza kampeni hiyo ambapo amesema lengo la Taifa Gas ni kuhakikisha wanaendelea kumuunga mkono Rais Samia juu ya matumizi ya nishati Safi hapa nchini. "Leo tupo hapa Kibaha ku...
Na Gustaphu Haule, Pwani WIZARA ya afya Kitengo cha Sikoseli imesema kuwa ugonjwa wa Selimundu (Sickle Cell) sio ugonjwa wa kurogwa kama ambavyo jamii inachukulia lakini ugonjwa huo ni wakurithi kutoka kwa mzazi mmoja kwenda kwa mzazi mwingine. Imesema ili kujiepusha na ugonjwa huo ni vyema kabla ya kuingia katika mahusiano jamii inapaswa kuchukua hatua ya kwenda kupima vinasaba vya ugonjwa na endapo watakuwa salama wanaweza kuoana na hatimaye kujenga familia salama isiyo na ugonjwa huo wa Selimundu (Sickle Cell). Daktari Bingwa wa magonjwa ya damu kutoka katika hospitali ya Amana iliyopo Jijini Dar es Salaam Jamila Makame, ametoa kauli hiyo katika semina ya siku moja kwa baadhi ya Waandishi wa Mkoa wa Pwani iliyolenga masuala ya ugonjwa wa Selimundu Semina hiyo iliyofanyika Agosti 12, 2025 katika kituo cha afya Mkoani kilichopo Manispaa ya Kibaha iliwajumuisha baadhi ya Waandishi wa habari ambapo Dr.Makame amesema "Sickle Cell" ni ugonjwa wa kurithi ambao chanzo...
Comments
Post a Comment