DR.CHAKOU TINDWA AKAGUA JENGO LA KITEGA UCHUMI CCM MKOA WA PWANI, AELEZA KURIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WAKE
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
Na. Gustaphu Haule, Pwani
MJUMBE wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Pwani na makamu mwenyekiti wa Kamati ya uchumi ya CCM Mkoa Pwani Dr.Chakou Tindwa amefanya ziara maalum ya kutembelea na kukagua mradi wa jengo la kitega uchumi la CCM Mkoa wa Pwani.
Dr.Tindwa amefanya ziara hiyo leo Septamba 13 katika jengo hilo lililopo Kibaha Mjini ambapo pamoja na mambo mengine ameeleza kuridhishwa na kasi ya ujenzi wa jengo hilo .
Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Pwani na makamu mwenyekiti wa kamati ya uchumi Dr.Chakou Tindwa akikagua jengo la kitega uchumi la Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani katika ziara yake aliyoifanya leo Septemba 13.2024.
Akiwa katika jengo hilo Dr .Tindwa amesema kuwa anatamani kuona jengo hilo linakamilika mapema ili kusudi kukisaidia chama kuondokana na usumbufu wa kutumia fedha nyingi kukodi kumbi za watu wengine Kwa ajili ya kufanyia mikutano ya Chama.
"Mimi ni makamu mwenyekiti wa kamati ya uchumi ya CCM Mkoa wa Pwani, hivyo niliona ni vyema leo nikafika hapa kwa ajili ya kukagua jengo hili na kuona maendeleo yake lakini hatahivyo nimeridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa jengo letu,"amesema Dr.Tindwa.
Dr.Tindwa amesema kuwa pamoja na kuchangia fedha kiasi cha Sh.milioni 120 katika harambee iliyofanyika hivi karibuni Jijini Dar es Salaam lakini pia kama kutakuwa na uhitaji mwingine atakuwa tayari kuchangia ili kusudi jengo hilo liweze kukamilika kama iliyokusudiwa.
Mjumbe wa kamati ya Sisa ya Chama Cha Mapinduzi ( CCM) Mkoa wa Pwani na makamu mwenyekiti wa kamati ya uchumi mkoa Dr.Chakou Tindwa akiwa katika jengo la kitega uchumi la CCM Mkoa wa Pwani leo Septemba 13, 2024.
Amewaomba, viongozi wa CCM pamoja na wadau wengine wa maendeleo kuendelea kushirikiana kwa ajili ya kuhakikisha Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani kinapata miradi mingi zaidi ambayo itasaidia kuondoa utegemezi .
Aidha , mwishoni mwa wiki iliyopita Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Taifa Ally Hapo,alitembelea jengo hilo na kusifu jitihada za kamati ya Siasa Mkoa wa Pwani kwa kubuni mradi ambao utakuwa na manufaa kwa chama.
Ziara ya Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Taifa Ally Hapi katika jengo la kitega uchumi la CCM Mkoa wa Pwani aliyoifanya hivi karibuni.
Hapo, amesema kama kila Mkoa kutakuwa na majengo kama hayo ni wazi kuwa CCM itakuwa imara zaidi ambapo ametaka mikoa mingine kuiga mfano huo.
Na Gustaphu Haule, Pwani MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge amewaongoza wakazi wa Mtaa wa Mkoani" A" uliopo Kata ya Tumbi Halmashauri ya Mji Kibaha katika zoezi la kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura lililoanza leo Mkoani Pwani. Aidha, Kunenge akiwa katika kituo hicho aliambatana na Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Rashid Mchatta, Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson Saimoni pamoja na mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Rogers Shemwelekwa. Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge akiwaongoza Wananchi wa Mtaa wa Mkoani "A", Kata ya Tumbi Halmashauri ya Mji Kibaha kujiandikisha katika daftari la wapiga kura zoezi ambalo limeanza leo Oktoba 11 hadi Oktoba 20 mwaka huu Akizungumza mara baada ya kujiandikisha katika kituo hicho Kunenge amesema kuwa zoezi hilo limeanza kufanyika Mkoa wa Pwani leo Oktoba 11 na litamalizika Oktoba 20 mwaka huu. Kunenge amesema kuwa kufanyika kwa zoezi hilo ni maandalizi ya kuelekea katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajia ...
Na Gustaphu Haule,Pwani BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Mji Kibaha limempongeza mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Dkt.Rogers Shemwelekwa kwa usimamizi mzuri katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Shemwelekwa ameshushiwa pongezi hizo Aprili 29, 2025 katika kikao cha Baraza hilo kilichofanyika katika Ukumbi wa soko kubwa la kisasa (Kibaha Shopping Mall) ambapo kwa kiasi kikubwa lilikuwa Baraza za kuonyesha mafanikio katika kipindi cha mwaka 2020/2025. Pongezi hizo zilikuja mara baada ya Wenyeviti wa kamati mbalimbali ikiwemo kamati ya fedha, kamati ya Mipango Miji, kamati ya Afya na Elimu pamoja na kamati ya huduma za jamii kueleza mafanikio ndani ya kipindi hicho cha miaka mitano. Mwenyekiti wa kamati ya fedha Karim Ntambo,amesema kuwa katika kipindi cha miaka mitano Manispaa ya Kibaha Mjini imepata mafanikio makubwa ambapo moja ya mafanikio hayo ni pamoja na ongezeko la mapato. Ntambo, amesema kuwa wakati wanaingia madarakani ukusanyaji mapato ulikuwa ni kiasi cha Sh.bilioni 4 la...
Na Gustaphu Haule,Pwani RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan ameridhia Halmashauri ya Mji Kibaha iliyopo Mkoani Pwani kupandishwa hadi na kuwa Manispaa. Uamuzi huo umetangazwa leo Januari 27 na Waziri wa Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa Mjini Kibaha. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Mohamed Mchengerwa akizungumza katika mkutano wa CCM uliofanyika Januari 27 katika viwanja vya stendi ya zamani Mailimoja Kibaha Mkoani Pwani. Mchengerwa, ametangaza hilo wakati akizungumza na wanachama wa CCM pamoja na Wananchi katika mkutano mkubwa wa kuunga mkono maazimio ya mkutano Mkuu wa CCM Taifa uliomteua Rais Samia kuwa mgombea wa Urais mwaka 2025. Wanachama wa CCM pamoja na Wananchi mbalimbali walioshiriki mkutano wa kuunga mkono azimio la Mkutano Mkuu wa Taifa CCM la kumteua Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea pekee wa Urais kupitia CCM katika uchaguzi wa mwaka 2025, Mkutan...
Comments
Post a Comment