Posts

Showing posts from June, 2025

ASASI ZA KIRAIA ZAOMBWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SERIKALI.

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani KAIMU Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Nsajigwa George, amezitaka asasi za kiraia na mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) kufanya kazi kwa kuzingatia sheria, kanuni, uwazi na uwajibikaji ili kuongeza tija katika utoaji wa huduma kwa jamii. Nsajigwa ametoa kauli hiyo Juni 26, 2025 wakati akifungua mkutano wa jukwaa la mashirika yasiyo ya kiserikali mkoa wa Pwani uliofanyika katika Ukumbi wa mdogo wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Pwani. Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani George Nsajigwa akizungumza katika kikao cha mashirika yasiyo ya kiserikali Juni 26,2025 Mjini Kibaha  Katika hotuba yake Nsajigwa amesisitiza umuhimu wa mashirika hayo kuzingatia taratibu za kisheria katika utekelezaji wa majukumu yao  hasa katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye mchakato wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025. “Mwaka 2025 ni mwaka wa uchaguzi, naomba niagize kuwa mashirika yote yafanye kazi kwa kuzingatia sheria na kanuni,msibadilike na kuwa sehemu ya migawanyiko ya kis...

DKT.CHARLES MWAMAJA AIPIGA TAFU KLABU YA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA PWANI.

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani MDAU wa maendeleo na mkazi wa Kibaha Mjini Mkoani Pwani Dkt.Charles Mwamaja ameipiga tafu Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Pwani kwa kuwapa samani za ofisi ikiwemo viti. Mwamaja, ambaye pia ni Kamishna kutoka Wizara ya fedha amekabidhi vifaa hivyo Juni 24, 2025 kupitia mwakilishi wake Philemon Maliga hafla ambayo imefanyika katika ofisi za Waandishi wa habari zilizopo Kibaha Mjini. Picha za makabidhiano ya samani za ofisi baina ya mdau wa maendeleo Dkt.Charles Mwamaja na Klabu ya Waandishi wa habari wa Mkoa wa Pwani. Awali, akizungumza kabla ya kukabidhi samani hizo  Maliga amesema kuwa  samani hizo ni sehemu ya kuonyesha ushirikiano kati ya Klabu ya waandishi wa habari na wadau wa maendeleo.  Maliga amesema  kuwa Waandishi wa Habari ni chombo ambacho kinachotumika kuelimisha jamii katika mambo mbalimbali hivyo wanatakiwa kupewa ushirikiano kutatua vikwazo vyao. Maliga, ameongeza kuwa msaada wa  samani hizo sio mwisho kwani ataendele...

MWENYEKITI KITONGOJI CHA KWAKIBOSHA MAPINGA AWAPIGA MSASA VIJANA 500 KULINDA AMANI YA TAIFA.

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani MWENYEKITI wa Kitongoji cha Kwakibosha kilichopo Kata ya Mapinga Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani Shaban Athumani amewataka vijana kuacha kutumika na watu wachache wenye nia ovyo ya kutaka  kuharibu amani na utulivu hapa nchini. Athumani ametoa wito huo katika mdahalo maalum wa kuwajengea uwezo vijana juu ya kukabiliana na vitendo viovu sambamba na kuwahamasisha vijana kulinda amani ya Taifa iliyoasisiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Mmoja wa Vijana wa Kitongoji cha Kwakibosha Mohamed Omary akichangia mada katika mdahalo huo Mdahalo huo umefanyika Juni 14, 2025  katika Kitongoji hicho na kuwashirikisha vijana zaidi ya 500 kutoka makundi mbalimbali wakiwemo bodaboda,mama lishe ,wapaka rangi na hata vijana kutoka UVCCM . Athumani, amesema kuwa mwaka 2025 ni mwaka wa uchaguzi mkuu unaokwenda kuwaweka madarakani viongozi akiwemo Rais, Wabunge na Madiwani na hiyo ndio fursa kwa vijana kuchagua viongozi wanaowataka. Mwenyekiti wa Kitongoji...

RC PWANI AFURAHISHWA NA UTENDAJI KAZI WA MKURUGENZI WA KIBAHA MJINI DKT.ROGERS SHEMWELEKWA

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani  MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge,amelipongeza Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Mji Kibaha kupitia mkurugenzi wake Dkt.Rogers Shemwelekwa kwa kazi nzuri ya kutekeleza miradi ya maendeleo iliyofanywa kwa kipindi cha mwaka 2020/2025. Aidha, Kunenge amesisitiza Baraza hilo kuwa katika kipindi cha mwaka 2025 /2030 wahakikishe wanapanga miradi yenye kipaumbele ili kuleta matokeo chanya katika jamii. Kunenge,ameyasema hayo Juni 16,2025 wakati akizungumza katika kikao maalum cha Baraza la Madiwani kwa ajili ya kujibu hoja za mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali (CAG)kikao ambacho kimefanyika katika Halmashauri ya Mji Kibaha. Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Musa Ndomba akizungumza katika kikao cha  Baraza maalum la kujibu hoja za mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) kilichofanyika Juni 16,2025  Amesema kuwa Kibaha Mjini imekuwa Halmashauri ya kuigwa kwakuwa katika kipindi kifupi tangu mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Dkt.Shemwelekwa kui...

WAZAZI PWANI WAPEWA NASAHA ULINZI NA MALEZI YA WATOTO KUNUSURU UKATILI WA KIJINSIA

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  KAIMU katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali Watu kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani Peter Billa amewataka Wazazi, Walezi na Jamii kwa ujumla kuwa walizi wa watoto ili kuhakikisha mtoto anakuwa katika mazingira bora. Katibu Tawala msaidizi Utawala na Raslimali watu wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Pwani Peter Billa akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika Juni 16,2025 katika viwanja vya Shule ya Msingi Kambarage iliyopo Kata ya Tumbi Kibaha Mjini. Billa ameyasema hayo leo Juni 16, 2025 kwa niaba ya katibu ya Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Rashid Mchatta wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika ambayo kimkoa yamefanyika katika Shule ya Msingi Kambarage iliyopo kata ya Tumbi, Kibaha Mkoani Pwani. Wanafunzi wa Shule mbalimbali za Msingi wakiwa katika maandamano ya siku ya Maadhimisho ya Mtoto wa Afrika ambapo kwa Mkoa wa Pwani yamefanyika katika Shule ya Msingi Kambarage iliyopo Kata ya Tumbi Kibaha Mjini. "...

MAKAMU MWENYEKITI UWT TAIFA ARIDHISHWA UJENZI SHULE YA ENGLISH MEDIUM KATA YA SOFU

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  MAKAMU mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania ( UWT) Zainabu Shomari ameeleza kuridhishwa na ujenzi wa mradi wa Shule ya awali na Msingi ya Mwalimu Nyerere unaotekelezwa katika Kata ya Sofu Halmashauri ya Mji Kibaha. Makamu mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Zainabu Shomari akisaini kitabu cha wageni katika Shule ya mchepuo wa Kiingereza ya awali na Msingi ya Mwalimu Nyerere iliyopo Kata ya Sofu Manispaa ya Kibaha  alipokwenda kwa ajili ya kukagua Shule hiyo Juni 15,2025. Makamu mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Zainabu Shomari akisaini kitabu cha wageni katika Shule ya mchepuo wa Kiingereza ya awali na Msingi ya Mwalimu Nyerere iliyopo Kata ya Sofu Manispaa ya Kibaha  alipokwenda kwa ajili ya kukagua Shule hiyo Juni 15,2025. Mradi huo wa Shule yenye mchepuo wa kiingereza unatekelezwa na Halmashauri ya Mji Kibaha kwa fedha za makusanyo ya  mapato ya ndani zaidi ya Sh .milioni 700 kupitia forc...

TAIFA GAS TANZANIA YAMUUNGA MKONO RAIS SAMIA KAMPENI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  KAMPUNI ya Taifa Gas Tanzania Limited imeendelea kuunga mkono kampeni ya Nishati Safi ya Kupikia ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa elimu na kuhamasisha  wananchi juu ya matumizi ya gas ya kupikia inayouzwa na Taifa Gas. Hii ni Gesi ya Petroli iliyoyeyushwa "Liquefied Petroleum Gas"  (LPG).  Taifa Gas Tanzania imetoa elimu hiyo leo Juni 7, 2025 katika eneo la Loliondo katika Manispaa ya Kibaha Mkoani Pwani  ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku ya Nishati Safi Duniani (Gas). Baadhi ya wananchi wa Kibaha Loliondo wakipata elimu juu ya matumizi ya nishati Safi ya kupikia kutoka kwa wafanyakazi wa Taifa Gas Tanzania ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya siku ya gesi Duniani. Meneja Uhusiano na Masoko kutoka Taifa Gas Kitengo cha Nishati Safi Anjellah Bhoke ameongoza kampeni hiyo ambapo amesema lengo la Taifa Gas ni kuhakikisha  wanaendelea kumuunga mkono Rais Samia juu ya matumizi ya nishati Safi hapa nchini. "Leo tupo hapa Kibaha ku...

MADAKTARI BINGWA WA RAIS SAMIA WAPIGA KAMBI PWANI

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani   TIMU ya madaktari bingwa 64 ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan imepokelewa Mkoani Pwani kwa ajili ya kuanza kazi maalum ya  kutoa huduma ya matibabu na uchunguzi wa Wananchi wa maeneo mbalimbali yaliyopo Mkoani Pwani. Timu hiyo imepokelewa leo Juni 9, 2025 katika ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Pwani na Mganga Mkuu wa Mkoa huo Kusirye Ukio ambaye katika hafla hiyo Ukio amemwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Rashid Mchatta. Mganga Mkuu wa mkoa wa Pwani Kusirye Ukio, akizungumza na madaktari bingwa wa Rais Samia mara baada ya kuwasili Mkoani humo leo kwa ajili ya kuanza kutoa huduma kwa jamii. Akizungumza katika hafla ya kuwapokea madaktari hao Ukio amewapongeza madaktari hao kwa utayari wao huku akiwaomba kwenda kujitoa kwa ajili kuwasaidia Wananchi na jamii kiujumla katika kupata huduma bora ya uchunguzi na matibabu. Ukio, amesema kuwa Rais Dkt.Samia ameanzisha jambo kubwa na nzuri lenye maslahi ya Wananchi wake na kwamb...