MAPATO YA USHURU WA HUDUMA YAPAA KWA KASI KIBAHA MJINI KUTOKA MIL 420 YA MWAKA 2024 MPAKA BILIONI 1.4 YA MWAKA 2025

Na Gustaphu Haule, Pwani HALMASHAURI ya Mji Kibaha chini ya Mkurugenzi wake Dkt.Rogers Shemwelekwa imefanikiwa kupandisha mapato yatokanayo na ushuru wa huduma (Service Levy) kutoka Sh.milioni 420 mpaka kufikia Sh.bilioni 1.4. Ongezeko la mapato hayo ni katika kipindi cha mwaka mmoja ikiwa ni kuanzia Machi 2024 hadi Aprili 2025. Taarifa ya ukusanyaji wa mapato hayo imetolewa na mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Dkt.Shemwelekwa katika kikao cha Baraza la Madiwani kilichoketi leo Aprili 29,2025 kikilenga kubainisha mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha mwaka 2020)2025. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dkt.Rogers Shemwelekwa (Pichani)akizungumza katika kikao cha Baraza la Madiwani kilichoketi Aprili 29,2025 katika Ukumbi wa Kibaha Shopping Mall. Kikao hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa Kibaha Shopping Mall licha ya kuhudhuriwa na Madiwani hao lakini pia kiliwashirikisha watumishi mbalimbali wakiwemo Watendaji Kata na walimu. Wafanyakazi wa kada mbalimbali kat...