Posts

Showing posts from October, 2024

RAIS SAMIA ATOA MIKOPO ISIYO NA MASHARTI NGAZI YA KATA NCHINI

Image
Na. Gustaphu Haule, Tanzania  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameanzisha mpango maalum wa kutoa mikopo isiyo na masharti kwa wananchi wasiojiweza kuanzia ngazi ya Kata. Rais Samia ametoa fursa hiyo akiwalenga zaidi  vijana walio na umri wa kuanzia miaka 18 hadi 45 kwa jinsia zote, wanawake  na walemavu.   Wanufaika wa mkopo huo watalazimika kulipa riba ndogo iliyogawanywa  katika makundi matatu, ambapo kundi la vijana litalipa asilimia nne, wanawake asilimia nne na kundi la walemavu litalipa  asilimia mbili. Mpango huo ni endelevu uliolenga kuwasaidia wananchi wote wenye kipato cha chini ili kujikwamua kiuchumi. Katika kuhakikisha hakuna vikwazo hatua zote za kisheria kwa wananchi kwa ajili ya kuchukua mkopo huo  zimerahisishwa na  hakuna kulipia gharama zozote za awali. Mkopo huu umewalenga Watanzania wa maeneo yote mijini na vijijini. Club News Editor - Charles Kusaga

RAIS DKT.SAMIA APAMBANIA MIUNDOMBINU YA BARABARA NCHINI, AFANIKIWA KUJENGA KILOMITA 819.22 ZA LAMI.

Image
Na Gustaphu Haule, Tanzania  SERIKALI  ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imefanikiwa kujenga barabara za lami za umbali wa Kilometa 819.22 na kuongeza za kiwango cha changarawe. Ujenzi wa barabara hizo umeongeza mtandao wa barabara za lami kutoka kilometa 2,404.90 hadi kufikia  kilometa 3,224.12. Ujenzi wa barabara za changarawe kilometa 11,924.36 na hivyo  kuongezeka kwa mtandao wa barabara za changarawe kutoka kilometa 29,183.17 hadi kilometa 41,107.52. Mbali na ujenzi wa barabara pia Wakala wa Barabara (TARURA) wameweza kujenga madaraja makubwa sita (6) ambayo ni ya Berega (140m) (Kilosa,) Msadya (60m) (Mpimbwe DC), Mwasanga (40m) (Mbeya) ambayo tayari yameanza kutumika. Daraja la Berega Aidha ujenzi wa madaraja ya Kiwila (40m)-Ileje, Mkomanzi-Korogwe (60m) na Kalambo (80m)-(Kalambo), unaendelea. TARURA imeeleza kuwa, katika kupunguza gharama, wameazimia kujenga barabara na madaraja kwa kutumia malighafi zinazopatik...

MAMA SAMIA AJA NA KAMPENI YA KUTOA MSAADA WA KISHERIA KWA WANANCHI BURE

Image
Na Gustaphu Haule, Tanzania  MOJA ya maeneo ambayo yanawatesa Watanzania wengi kutokana na kukosa uwezo ni eneo la kupata huduma za kisheria hasa Mahakamani. Gharama za uendeshaji kesi kwa kutumia Mawakili ni kubwa jambo ambalo limekuwa likiwashinda wananchi wengi wa hali ya chini. Kwa kuliona hilo serikali ya awamu ya Sita iliyo chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kushirikiana na wadau wengine imekuja na kampeni maalum ya kutoa huduma za kisheria kwa wananchi. Huduma hiyo inatolewa  bure huku ikipewa jina  kama Mama Samia Legal Aid. Oktoba 28,2024 Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kwa kushirikiana na Wizara ya Katiba na Sheria wamefanya kikao kazi kilichokusudia kuandaa mkakati wa pamoja wa kutoa msaada wa huduma za kisheria kwa wananchi bure kupitia kampeni hiyo. Akizungumza wakati wa kikao hicho kilichofanyika  Mkoani Iringa, Rais wa TLS, Wakili Boniface Mwabukusi, amesisitiza umuhimu wa TLS na Serikali kuwafikia wananchi wa pembezoni ambao hawawezi kum...

TGNP NA TADIO YAWANOA WAANDISHI WA HABARI KUANDIKA HABARI ZENYE MLENGO WA JINSIA, YATAKA WAANDISHI KUHAMASISHA WANAWAKE KUGOMBEA.

Image
Na Gustaphu Haule  MTANDAO wa Jinsia Tanzania (TGNP) kwa kushirikiana na mtandao wa Radio Jamii Tanzania wameendelea kuwapiga msasa Waandishi wa habari kuhusu kuhamasisha ushiriki wa Wanawake katika uongozi hasa katika kipindi cha kuelekea katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Mafunzo hayo ya siku tatu yameanza kufanyika leo Oktoba 29 katika ofisi za TGNP zilizopo Jijini Dar es Salaam na kumalizika Oktoba 31 mwaka huu yakiwa chini ya wakufunzi wawili akiwemo Deogratius Temba na Vera Assenga. Katika mafunzo hayo TGNP imewakutanisha waandishi wa habari zaidi ya 50 kutoka mikoa mbalimbali ikiwemo Mtwara, Lindi, Pwani na Dar es Salaam. Akifungua mafunzo hayo afisa habari wa TGNP Monica John, amesema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuendelea kuhamasisha Wanawake kutumia fursa zilizopo hasa katika uchaguzi kugombea nafasi mbalimbali. Afisa habari wa Mtandao wa Kijinsia Tanzania  Monica John (kushoto) akifungua mafunzo ya siku tatu kwa Waandishi wa habari kuhusu masuala ya kuandika hab...

RAIS SAMIA AZIDI KUMWONDOLEA MTANZANIA UMASKINI, AIPAISHA TANZANIA KWENYE UKUAJI WA UCHUMI AFRIKA.

Image
Na Gustaphu Haule,Tanzania  KIU ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kutaka kumwondoa Mtanzania kwenye umasikini pamoja na uongozi wake madhubuti umeifanya Tanzania kuingia kwenye 10 bora za ukuaji wa uchumi barani Afrika. Mara baada ya Rais Samia kuingia madarakani Machi 19,2021 amekuwa akifanya kazi kubwa ya kufungua milango ya maendeleo kwenye kila sekta. Ameweza kuwakaribisha wafanyabiashara wenye mitaji kutoka ndani na nje ya nchi kuwekeza nchini. Dhamira yake hiyo ya kumwondolea mwananchi umasikini imemfanya Rais Dkt. Samia kuwa kiongozi pekee mwanamke aliyeingiza nchi kwenye 10 bora za ukuaji wa uchumi Afrika, akiziacha nchi 44 nyuma. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Shirika la Fedha duniani (IMF), mwishoni mwa wiki iliyopita, licha ya changamoto zinazoukumba uchumi wa dunia kwa sasa kutokana na vita na magonjwa mbalimbali ya milipuko, Rais Dkt. Samia ameendelea kuifanya  Tanzania kuwa imara kwenye ukuaji wake kiuchumi kwa mwaka 2024. Ukuaji wa pato la Taifa (GDP) kwa s...

SHAURI AFUNGUA DIRISHA UCHUKUAJI FOMU UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA

Image
Na Gustaphu Haule  MGOMBEA wa nafasi ya  Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Mailimoja "B" kupitia Chama Cha Mapinduzi" CCM" Shauri Yombayomba  tayari amechukua fomu kwa ajili ya kuwania nafasi hiyo. Yombayomba amechukua fomu hiyo mapema leo Oktoba 28 katika ofisi za Mtaa huo akiambatana na wajumbe wake watano akiwemo Webina Gimasa, Josephu Sanga, Mwanaidi Ndotia, Omari Mfaume na Zainabu Charles. Mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti Serikali ya Mtaa Mailimoja B Shauri Yombayomba (CCM) akipokea fomu kutoka kwa Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi katika Mtaa huo Suzana Awiti leo Oktoba 28, 2024 Miongoni mwa viongozi alioongozana nao ni Mwenyekiti wa CCM tawi la Yombayomba, Amina Musa, Katibu wa tawi Kizito Iyulu na Katibu wa itikadi uenezi na mafunzo Chedy Shaban. Akiwa ofisini hapo Yombayomba alikabidhiwa fomu hiyo na msimamizi Msaidizi wa uchaguzi Mtaa wa Mailimoja "B" Suzana Awiti ambaye alimueleza mgombea huyo kuwa ofisi hiyo inakuwa wazi mpaka saa 10 jioni. Akizungumz...

MILIONI 410 ZA MAPATO YA NDANI ZATENGENEZA MADAWATI 4000 KIBAHA MJINI

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  HALMASHAURI ya Mji Kibaha iliyopo Mkoani Pwani imetoa kiasi cha Sh .milioni 410 za makusanyo ya mapato ya ndani kwa ajili ya Kutengeneza madawati 4000 ya Shule za Msingi na Sekondari zilizopo katika Halmashauri hiyo. Hafla ya uzinduzi wa ugawaji madawati hayo imefanyika leo Oktoba 25 mwaka huu katika viwanja vya Shule ya Msingi Mkoani iliyopo Kata ya Tumbi ambapo mgeni rasmi katika hafla hiyo ni Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka. Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka( katikati) akikata utepe kwa ajili ya uzinduzi wa ugawaji wa madawati, viti na meza 4000 kwa Shule za Msingi na Sekondari zilizopo katika Halmashauri ya Kibaha Mjini ,hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 25 kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Mkoani iliyopo Kata ya Tumbi. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dkt.Rogers Shemwelekwa amesema kuwa ugawaji wa madawati hayo ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa awamu ya Sita Dkt,Samia Suluhu Hassan anayetaka kuhakikisha changamo...

UCHAGUZI KURA ZA MAONI CCM WATIKISA, WENGI WASHINDA KWA KISHINDO

Image
Na Gustaphu Haule, Kibaha PWANI UCHAGUZI wa kura za maoni ndani ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) kwa ajili ya kuwapata wagombea katika kinyanga' nyiro cha uchaguzi wa Serikali za Mitaa umefanyika jana Oktoba 23 katika maeneo mbalimbali huku baadhi wa wagombea wakiibuka na ushindi mnono. Wagombea walioibuka kinara katika uchaguzi huo ni pamoja na Shauri YombaYomba Mwenyekiti mstaafu wa Mtaa wa Mailimoja"B" kutoka tawi la  Yombayomba aliyeibuka mshindi kwa kupata kura 186 dhidi Shamira Salum aliyepata kura mbili na Anthony Fudua   akiambulia kura Moja. Mwenyekiti mstaafu wa Serikali ya Mtaa Mailimoja "B"Shauri Yombayomba akiwashukuru wajumbe mara baada ya kutangazwa kuwa mshindi katika wa uchaguzi wa kura za maoni tawi la Yombayomba uliofanyika Oktoba 23 mwaka huu. Uchaguzi wa tawi la Yombayomba umesimamiwa na Juma Kasheshe pamoja na Yohana Mwananzila  kutoka CCM Kata ya Tangini ambapo hatahivyo waliendesha uchaguzi huo kwa utaratibu mzuri uliowavutia wagombea na wapig...

BASHUNGWA AKAGUA NA KUZINDUA MIRADI MKURANGA - PWANI.

Image
Na. Julieth Ngarabali, PWANI Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amezindua jengo la utawala katika Shule ya Sekondari ya Mwandege lililojengwa na kukamilika kupitia fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga lililogharimu kiasi cha Shilingi Milioni 119.9. Bashungwa amezindua jengo hilo Oktoba 23,   2024 Wilayani Mkuranga Mkoani Pwani ikiwa ni muendelezo wa ziara yake maalum katika Mkoa huo ya kukagua utekelezaji na kuzindua miradi ya maendeleo pamoja na kuzungumza na wananchi. Bashungwa amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha za miradi ya maendeleo kwenye Sekta mbalimbali katika Mkoa wa Pwani na ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga kwa kazi nzuri ya usimamizi wa fedha hizo. Katika hatua nyingine, Waziri Bashungwa amezindua daraja katika barabara ya Mwanambaya – Mipeko eneo la bonde la mto Mzinga lililojengwa na kusimamiwa  na Wakala ya Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) kwa ajili ya kuimarisha miundombinu ...

RC PWANI AFANYA HAMASA YA KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA KUPIGIA KURA KUTUMIA MBIO ZA JOGING.

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge ameendelea kuhamasisha wananchi kujitokeza kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura kwa kuendesha mbio za taratibu za kukimbia (Joging) zenye zaidi ya kilomita 5. Mbio hizo zimefanyika Mjini Kibaha  Oktoba 12 kuanzia ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani kupitia barabara ya Morogoro na kuelekea Soko la Loliondo na kisha kumalizia katika viwanja vya stendi ya zamani iliyopo Mailimoja Kibaha Mjini. Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge akikimbia mbio za taratibu (Joging) kwa ajili ya kuhamasisha wananchi kujitokeza kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura ,Joging hiyo imefanyika Oktoba 12 Mjini Kibaha. Akizungumza na Wananchi waliokusanyika katika viwanja hivyo Kunenge amesema kuwa lengo la joging hiyo ni kuendelea kuhamasisha wananchi wajitokeze kwa wingi katika kujiandikisha na hata kupiga kura siku itakapowadia. Amesema, uchaguzi wa Serikali za Mitaa ndio unaotoa dira ya maendeleo hapa nchini kwakuwa kila jambo linaan...

MKURUGENZI KIBAHA MJINI AFUATILIA KUJIANDIKISHA VITUONI, ATEMBEA KUHAMASISHA WANANCHI

Image
Na Gustaphu Haule,Kibaha MKURUGENZI wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dkt .Rogers Shemwelekwa amefanya ufuatiliaji katika vituo vya uandikishaji wa daftari la wapiga kura katika Kata mbalimbali ikiwemo  Kata ya  Kongowe, Viziwaziwa na Picha ya Ndege. Dkt. Shemwelekwa ambaye awali aliambatana na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge katika uzinduzi wa zoezi hilo Mtaa wa Mkoani" A" amelazimika kufanya ufuatiliaji huo ili kujua kama kuna changamoto katika vituo hivyo. Akiwa katika vituo hivyo kwa wakati tofauti Dkt .Shemwelekwa alipata nafasi ya kuongea na makundi mbalimbali wakiwemo wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya Kata na Mitaa, Waandikishaji na Wananchi. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dkt.Rogers Shemwelekwa mwenye koti nyeusi akifuatilia zoezi la uandikishaji wa daftari la wapiga kura katika moja ya vituo vilivyopo katika Halmashauri yake Leo Oktoba 11. Aidha, amewataka mawakala wa vyama vyote kuhakikisha wanafanya kazi kwa amani, utulivu na upendo vituoni mwao ...