Posts

Showing posts from June, 2024

WATOTO WATAJA VIBANDA UMIZA NA KAMALI VYANZO VYA UKATILI PWANI

Image
Na. Julieth Ngarabali. Utitiri wa vibanda vya maonyesho ya video na michezo ya kamali(kubeti) maeneo mbalimbali Mkoani Pwani kumeelezwa  kuwa ni baadhi ya vyanzo vinavyosababisha  kuenea vitendo vya ukatili na unyanyaswaji  dhidi ya watoto. Mbali na maeneo hayo pia baadhi ya waendesha bodaboda wametajwa na watoto kuwa wamekuwa wakichangia wanafunzi kukatisha masomo kwa kuwapa ujauzito . Hayo yamebainishwa baadhi ya wanafunzi kutoka shule za msingi na sekondari  za Halmashauri ya mji wa Kibaha Mkoani humo  kwenye mdahalo  uliokuwa na lengo la kujadili masuala mbalimbali  ikiwemo ya ukatili yanayowakabili watoto kuanzia umri wa miaka sefuri  na kuendelea ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika Mkoani humo Katika mdahalo huo uliowashirikisha wadau mbalimbali wanaojihusisha na masuala ya watoto mada kuu tatu za ushiriki wa wadau katika kutokomeza ukatili wa jinsia ,wajibu wa wazazi na walezi katika kuwasaidia watoto kuzingatia maadil...

NITAWAPA KILA KITU ILA KADI YA CCM SITAWAPA - RIDHIWANI.

Image
PIGANIENI CHAMA CHENU MSISUBIRI KUKUMBUSHWA Na. Julieth Ngarabali.  Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora  Ridhiwani Kikwete ambaye pia ni Mbunge wa Chalinze Pwani amewaasa vijana wa chama cha Mapinduzi kukipigania chama chao kwa wivu mkubwa ili kulinda na kutekeleza malengo ya chama katika kuwahudumia wananchi na kuleta maendeleo kwa wananchi bila ubaguzi.  .Ridhiwani aliyabainisha hayo Mkoani Morogoro wakati akihutubia Mkutano wa Kuwaaga Wanachama wa CCM Seneti ya vyuo na tv vyuo Vikuu uliofanyika katika chuo cha Mtakatifu Jordan mkoani humo. Amesema "hata kama ikifika siku chama hichi kinaona Ridhiwani hafai kuwa mwanachama wakaamua kunifukuza nitawapa kila kitu lakini kadi ya Chama cha Mapinduzi sitatoa kwasababu Chama cha Mapinduzi kipo moyoni mwangu na huu ndio msingi ambao mnatakiwa muwe nao , piganieni chama chenu msisubiri kukumbushwa jukumu hilo" alisisitiza Mhe. Ridhiwani Club News Editor - Charles Kusaga

MWEKEZAJI GARDEN KIBAHA MJINI AMLILIA RC KUNENGE

Image
Na Mwandishi Wetu,Kibaha MWEKEZAJI wa eneo maarufu  la Garden lililopo Kata ya Tumbi katika Halmashauri ya Mji Kibaha Zakaria Jensen amemuomba Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge kumsaidia kutatua changamoto zinazomkabili ili haweze kufanya biashara yake katika mazingira mazuri . Jensen,amesema kwasasa anafanya biashara zake kwa mashaka makubwa kutokana na baadhi ya watendaji kutoka katika Halmashauri hiyo kutaka kumuondoa kinguvu katika eneo hilo bila kupewa sababu ya msingi. Anasema,anachokishangaa kuona baadhi ya watendaji wa Halmashauri wakifanya njama za kumuondoa wakati yeye amepangishwa eneo hilo na Wakala wa barabara Mkoa wa Pwani (Tanroads). Eneo la garden lililopo Kata ya Tumbi katika Halmashauri ya Mji Kibaha lililowekewa alama nyekundu ya x inayomtaka mmiliki wake Zakaria Jensen kubomoa kama linavyoonekana pichani. Amesema, eneo la Kibaha Mailimoja na eneo la Tumbi lililopo kando ya barabara ya Morogoro ni eneo la Tanroads na kuna wafanyabiashara zaidi ya 3000 ambao ...

Maboresho ya ushoroba yapunguza maumivu ya tembo Kilombero

Image
Uvamizi wa tembo kwenye makazi ya watu na mashamba yapungua ndani ya miaka mitatu.  Baadhi ya waumini wa Kiislamu na Kikristo wabadili ratiba za ibada kukwepa madhila ya wanyamapori. Na Gustaphu Haule, Kilombero  Miaka mitatu iliyopita ilikuwa ni kawaida kwa baadhi ya waumini wa kiislamu na kikristo wanaowahi asubuhi kufanya ibada katika Kijiji cha Magombera wilayani Kilombero kukutana na tembo njiani mara kwa mara. Sehemu kubwa ya wakazi hao walikuwa wanakutana na wanyamapori hao katika ibada zinazoanzia 11:00 alfajiri hadi angalau Saa 2:00 asubuhi.  Mbali na kukutana na waamini hao njiani, baadhi ya wanyama hao walivamia hadi nyumba za ibada ikiwemo makanisa na misikiti.  Ili kuwanusuru waumini hao wa kata ya Mkura, viongozi wa dini katika maeneo hayo walilazimika kubadili muda wa kufanya ibada ili kupunguza hatari za kuathiriwa na wanyamapori hao. "Tembo wamekuwa wakisumbua sana hapa kijijini kwetu na  tunashindwa kuswali swala tano kwa kuwa tunaogopa kuvamiw...

MLAO AWATEGA WABUNGE NA MADIWANI ,ASEMA WATAPIMWA KWA KAZI ZAO,AVUNJA NGOME YA CUF NA CHADEMA MKURANGA.

Image
Na GUSTAPHU HAULE, PWANI  MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Mkoa wa Pwani  Mwinshehe Mlao amewataka wabunge na madiwani kujiandaa kisaikolojia kwani kurudi au kutokurudi kwa majina yao kutapimwa na kazi zao walizofanya. Mlao,ametoa kauli hiyo Juni 7 mwaka huu akiwa katika ziara yake Wilayani Mkuranga iliyokuwa inalenga kufanya tathmini ya kuelekea katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa,Vijiji,na Vitongoji kwa mwaka 2024. Katika ziara hiyo, Mlao aliambatana na Watendaji mbalimbali akiwemo Katibu wa CCM Mkoa Bernard Ghaty, Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Pwani na Makamu mwenyekiti wa Kamati ya uchumi Dkt. Chakou Tindwa,Katibu wa UWT Mkoa Fatuma Ndee  na watendaji wengine. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani Mwinshehe Mlao,akizungumza na wanachama wa CCM Wilayani Mkuranga ikiwa ni sehemu ya ziara yake aliyoifanya Juni 7 mwaka huu. Aidha,Mlao  alipita katika Kata ya Dondo,Kitomondo,na Kata ya Njia nne zilizopo katika tarafa ya Kisiju ambapo akiwa k...

Jinsi kamera zinavyosaidia kurejesha uhusiano kati ya binadamu na tembo Shoroba ya Nyerere Selous-Udzungwa

Image
Na Julieth Mkireri, Ifakara Inawezekana kabisa usiwe mgeni wa njia ya barabara ya Ifakara-Mikumi. Ikiwa umewahi kupita hapa, bila shaka umekutana na moja ya alama muhimu – bango la Hifadhi ya Taifa ya Udzungwa likiwa na maneno “Welcome to Udzungwa National Park.”  Ukiwa unatoka Ifakara kuelekea Mikumi, bango hili lipo upande wako wa kushoto unapofika Mang'ula, na ukiwa unasafiri kutoka Mikumi kuelekea Ifakara, bango hilo lipo upande wako wa kulia. Lakini usilolifahamu ni kwamba mbele kidogo ya bango hilo, kuna ushoroba wa Nyerere Selous-Udzungwa. Hii ni njia muhimu inayotumiwa na wanyama, hususan tembo, kutoka Hifadhi ya Taifa ya Udzungwa kwenda Hifadhi ya Nyerere Selous. Ili kuhakikisha ushoroba huu unakuwa salama kwa wanyama na binadamu, hatua mbalimbali za kuboresha mazingira zimechukuliwa. Hii ni pamoja na ufungaji wa kamera na ujenzi wa miundombinu rahisi ya kupita wanyama Moja ya Kamera zinazofungwa shoroba ya Nyerere SELOUS--Udzungwa  Amina Mohamed, mkazi wa Mang’ula B,...