NITAWAPA KILA KITU ILA KADI YA CCM SITAWAPA - RIDHIWANI.



  • PIGANIENI CHAMA CHENU MSISUBIRI KUKUMBUSHWA
Na. Julieth Ngarabali. 

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora  Ridhiwani Kikwete ambaye pia ni Mbunge wa Chalinze Pwani amewaasa vijana wa chama cha Mapinduzi kukipigania chama chao kwa wivu mkubwa ili kulinda na kutekeleza malengo ya chama katika kuwahudumia wananchi na kuleta maendeleo kwa wananchi bila ubaguzi. 


.Ridhiwani aliyabainisha hayo Mkoani Morogoro wakati akihutubia Mkutano wa Kuwaaga Wanachama wa CCM Seneti ya vyuo na tv vyuo Vikuu uliofanyika katika chuo cha Mtakatifu Jordan mkoani humo.

Amesema "hata kama ikifika siku chama hichi kinaona Ridhiwani hafai kuwa mwanachama wakaamua kunifukuza nitawapa kila kitu lakini kadi ya Chama cha Mapinduzi sitatoa kwasababu Chama cha Mapinduzi kipo moyoni mwangu na huu ndio msingi ambao mnatakiwa muwe nao , piganieni chama chenu msisubiri kukumbushwa jukumu hilo" alisisitiza Mhe. Ridhiwani




Club News Editor - Charles Kusaga

Comments

Popular posts from this blog

RC PWANI AONGOZA WAKAZI PWANI KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA

BARAZA LA MADIWANI KIBAHA MJINI LAMPONGEZA MKURUGENZI WAKE KWA KAZI NZURI ANAYOIFANYA SAMBAMBA NA KUONGEZA MAPATO.

RAIS SAMIA ATANGAZA KIBAHA MJINI KUWA MANISAPAA,MBUNGE KOKA AFURAHIA ASEMA KIBAHA ITANG'AA