Posts

Showing posts from March, 2024

MATOKEO YA SENSA 2022 NA MATUMIZI YAKE KWA MAENDELEO YA TAIFA, WANAHABARI WAJENGEWA UWEZO KUELIMISHA JAMII.

Image
  Na mwandishi wetu Pwani. Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilifanya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022. Baada ya  kukamilisha awamu mbili za kwanza za utekelezaji wa Sensa hiyo, Serikali imo katika awamu ya tatu na ya mwisho ya utekelezaji wa Sensa hiyo inayojumuisha uchakataji, uchambuzi, uandishi wa ripoti, usambazaji na mafunzo ya Matumizi ya Matokeo hayo ya Sensa ya Mwaka 2022. Katika awamu ya tatu ya utekelezaji wa Sensa ya Watu na Makazi ya 2022 Wanahabari wa mikoa ya Pwani, Morogoro na Tanga wamejengewa uwezo namna ya kupata Matokeo, kuyatafsiri na kuyatumia katika kusambaza na Kuelimisha jamii kuhusu namna ya Matumizi yake.   Akifungua Mafunzo hayo yalifanyika kwa siku mbili tarehe 16 na 17 Jijini Tanga. Katika ufunguzi wa Mafunzo hayo Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Ndugu Sebastian Masanja ameeleza umuhimu wa kazi za wanahabari katika jamii na Wananchi wanatambua kazi hizo. Alitoa Rai kwa wanahabari kwenda kuelimisha wananchi juu ya Matok...

KIKWETE AKABIDHI PIKIPIKI KWA MAAFISA UGANI CHALINZE

Image
Julieth Ngarabali, Chalinze Mbunge wa Jimbo la Chalinze Mkoani Pwani Ridhiwani Kikwtete amekabidhi pikipiki sita  kwa Maafisa Ugani wa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze ikiwa ni sehemu ya kuendelea kuwapatia Vitendea kazi Watumishi wa kada hiyo katika sekta ya Kilimo na Mifugo kwenye halmashairi hiyo. Ikumbukwe kuwa Ridhiwani pia ni Naibu Waziri katika Ofisi ya Rais  manejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora. Amesema pikipiki  hizo zimetolewa na Serikali Kuu kupitia Wizara ya Kilimo na kwamba  zinalenga kuwawezesha  maafisa Ugani kuweza kufika katika maeneo ya kwa wenye uhitaji ili kuwezesha kilimo bora. Kugawiwa kwa pikipiki hizi kunafanya maafisa ugani waliopewa vifaa hivyo kufika 14 kati ya kata 16 za Halmashauri hiyo. Halmashauri ya Chalinze ni moja kati ya Halmashauri zinazoongoza kwa kilimo katika eneo  la Mashariki ya Tanzania. Club News Editor

HIVI NDIVYO KAMPENI YA UCHAGUZI CCM MSANGANI ILIVYOANZA KIBAHA

Image
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais ,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Mohamed Mchengerwa akimnadi mgombea wa udiwani wa Kata ya Msangani kwa tiketi ya CCM Gunze Chongela katika ufunguzi wa kampeni uliofanyika jana katika viwanja vya juhudi vilivyopo kwenye Kata hiyo  Na Gustafu Haule,Pwani WAZIRI wa Nchi,Ofisi ya Rais ,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Mohamed Mchengerwa,amesema Serikali ya awamu ya Sita imeweka mpango maalum wa kuhakikisha inajenga Shule za Sekondari na Msingi katika Kata ambazo hazina Shule. Mchengerwa ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa( NEC) ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na wananchi,wanachama na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi katika uzinduzi wa kampeni za udiwani Kata ya Msangani Halmashauri ya Kibaha Mjini zilizofanyika Machi 9 . Amesema kuwa,Serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan inatambua umuhimu wa elimu hapa nchini na kwamba kila siku inaendelea kuweka juhudi za kuimarisha miundombinu ...

LIGI YA SOKA YA MABINGWA WA MIKOA YAANZA KWA MBWEMBWE PWANI

Image
Na Gustafu Haule,Pwani MASHINDANO ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa yameanza kutimua vumbi Machi 8, mwaka huu katika viwanja vya Tamco vilivyopo Mjini Kibaha kwa kuzikutanisha timu ya  Kiduli FC  na Black Six ya Jijini Dar es Salaam . Katika mchezo huo Black Six wameibuka na ushindi wa bao 1-0  lililofungwa katika dakika 41 ya  kipindi cha kwanza kupitia mchezaji wao Kelvin madalisto aliyefunga kupitia mpira wa kichkiwa uliopigwa kutoka kulia mwa dimba hilo. Kocha wa Kiduli FC Hery Kisanga , amesema kuwa mchezo wao wa kwanza wamefungwa kutokana na makosa yaliyofanywa na wachezaji wake lakini kufungwa kwao hakuwafanyi kukata tamaa . Kocha wa Kiduli FC Hery Kisanga ,akizungumza  mara baada ya kumalizika kwa mchezo dhidi ya Black Six uliopigwa katika dimba la Tamco -Kibaha Machi 08 ,2024. Kisanga, amesema kuwa kwasasa wanajipanga na michezo mingine inayofuata na watakwenda kuyafanyiakazi mapungufu yaliyojitokeza na ana imani michezo ijayo itakwenda kuzaa matunda. "Leo t...

WANAOJIFUNGUA WATOTO NJITI WALIA NA SHERIA YA AJIRA NA MAHUSIANO KAZINI,

Image
Watoto Njiti ni wale wanaozaliwa kabla ya miezi tisa ya ujauzito.  Soma chanzo cha kuzaliwa , changamoto zao. Julieth Ngarabali, Pwani.   Wafanya kazi  wanawake  waliojifungua watoto kabla ya muda  wake maarufu watoto  njiti  wamesema siku 84 zilizowekwa kisheria kama likizo ya uzazi hazitoshelezi  kulea  watoto njiti  na kwamba kuna umuhimu wa Serikali kuangalia upya  uwezekano wa kuboresha sheria ya ajira na mahusiano kazini  sura ya 366 na marekebisho yake ya mwaka 2019 . Katika sheria hiyo kifungu kidogo cha 33 kifungu kidogo cha 6 (a ) kinasema mtumishi mwanamke aliyejifungua mtoto mmoja atapata likizo ya siku 84  huku kifungu cha 33 kifungu kidogo cha 6 ( b ) inaeleza kuwa mtumishi mwanamke aliyejifungua watoto zaidi ya mmoja atapata likizo ya siku 100 ambapo sheria hiyo imeishia hapo haijasema kama atajifungua watoto njiti atapata muda wa ziada na hivyo shida imeanzia hapo  Mmoja wa wanawake wali...

BALOZI NCHIMBI: TUWEKEZE KWA WANAWAKE KWA MAENDELEO YA TAIFA

Image
             Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi  Na Mwandishi wetu ,Zanzibar,  Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi ametoa wito kwa jamii ya kitanzania kuendelea na jitihada zake za kuwawezesha wanawake katika nyanja mbalimbali za maisha, ili kuharakisha kasi ya maendeleo ya taifa. Katika salaam zake za heri kwa wanawake wote, katika kilele cha Siku ya Wanawake Duniani, inayoadhimishwa tarehe 8, Machi, kila mwaka, Balozi Nchimbi, akirejea kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu 2024, amesisitiza umuhimu wa kuwekeza kwa wanawake ili kuharakisha maendeleo na ustawi wa jamii kwa taifa. “Kama kauli mbiu yetu yam waka huu inavyosema Wekeza kwa Wanawake: Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii, inatuhimiza umuhimu wa kuwawezesha wanawake katika jamii yetu, kiuchumi, kielimu, na kisiasa ili kuchangia kasi ya maendeleo ya Taifa na kuboresha ustawi wa jamii kwa ujumla. Nasi k...

UMEME WAKUTOSHA UNAKUJA WAWEKEZAJI TULIENI, ASEMA RC KUNENGE

Image
      Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge,akizungumza wakati akifungua kikao cha Baraza la Biashara la Mkoa wa Pwani kilichofanyika Machi 06 ,2024 Mjini Kibaha Na Gustafu Haule,Pwani MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge,amefungua Baraza la Biashara la Mkoa huku akiwatoa wasiwasi wawekezaji kuhusu suala la umeme  kwakusema changamoto hiyo inakwenda  kuisha kwakuwa Serikali imeweka mipango mizuri.  Kunenge, amesema kuwa Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan imefanyakazi kubwa ya kutengeneza miundombinu ya umeme ikiwemo ujenzi wa bwawa la Mwalimu Nyerere lililopo Wilayani Rufiji ambalo tayari  mpaka sasa limeanza kufua umeme Kwa kuwasha mambo mmoja unaozalisha megawati zaidi ya 200. Kunenge,amesema hayo wakati akifungua baraza hilo leo Machi 06 lililofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa uliopo Mjini Kibaha kikao ambacho kimehudhuriwa na wawekezaji mbalimbali wa viwanda, viongozi wa chemba ya biashara Mkoa, Taasis...