KIKWETE AKABIDHI PIKIPIKI KWA MAAFISA UGANI CHALINZE



Julieth Ngarabali, Chalinze

Mbunge wa Jimbo la Chalinze Mkoani Pwani Ridhiwani Kikwtete amekabidhi pikipiki sita  kwa Maafisa Ugani wa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze ikiwa ni sehemu ya kuendelea kuwapatia Vitendea kazi Watumishi wa kada hiyo katika sekta ya Kilimo na Mifugo kwenye halmashairi hiyo.

Ikumbukwe kuwa Ridhiwani pia ni Naibu Waziri katika Ofisi ya Rais  manejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora.


Amesema pikipiki  hizo zimetolewa na Serikali Kuu kupitia Wizara ya Kilimo na kwamba  zinalenga kuwawezesha  maafisa Ugani kuweza kufika katika maeneo ya kwa wenye uhitaji ili kuwezesha kilimo bora.

Kugawiwa kwa pikipiki hizi kunafanya maafisa ugani waliopewa vifaa hivyo kufika 14 kati ya kata 16 za Halmashauri hiyo.

Halmashauri ya Chalinze ni moja kati ya Halmashauri zinazoongoza kwa kilimo katika eneo  la Mashariki ya Tanzania.





Club News Editor

Comments

Popular posts from this blog

RC PWANI AONGOZA WAKAZI PWANI KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA

BARAZA LA MADIWANI KIBAHA MJINI LAMPONGEZA MKURUGENZI WAKE KWA KAZI NZURI ANAYOIFANYA SAMBAMBA NA KUONGEZA MAPATO.

RAIS SAMIA ATANGAZA KIBAHA MJINI KUWA MANISAPAA,MBUNGE KOKA AFURAHIA ASEMA KIBAHA ITANG'AA