Posts

Showing posts from January, 2025

TAKUKURU PWANI YAOKOA ZAIDI YA MILIONI 314 ZILIZOKUWA ZINAPOTEA KATIKA KIZUIZI CHA MALIASILI KIBITI.

Image
Na Gustaphu Haule ,Pwani TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Pwani imesaidia kuokoa fedha zaidi ya Sh.milioni 314 zilizokuwa zinapotea kwa mwaka katika Kizuizi cha Maliasili kilichopo Wilayani Kibiti. Awali kabla Takukuru hawajafanya ufuatiliaji katika Kizuizi hicho makusanyo ya mapato  kwa wiki kwa kutumia mashine ya POS yalikuwa kiasi cha Sh.milioni 4.6 ambapo kwa mwaka ukusanya kiasi cha Sh.milioni 166.7. Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Pwani Alli Sadiki, amewaambia Waandishi wa habari Januari 31, 2025 katika mkutano uliofanyika ofisini kwake Mjini Kibaha kuwa  walifanya ufuatiliaji katika kituo hicho na kubaini fedha nyingi kupotea katika Kizuizi hicho. Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Pwani Alli Sadiki, akizungumza na Waandishi wa habari Januari 31,2025 katika ofisi zake zilizopo Mjini Kibaha kuhusu utekelezaji wa shughuli za taasisi zilizofanyika katika kipindi cha Oktoba hadi Desemba 2024. Sadiki, amesema kuwa katika kipindi cha Oktoba na Desemba 2024 Takukuru ...

TUME YA RAIS YA MABORESHO YA KODI YAINGIA PWANI YAKUTANA NA MAONI, LUKUKI ,RC PWANI AISIFU TUME HIYO.

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani TUME ya Rais ya Maboresho ya Kodi imeingia Mkoani Pwani kwa ajili ya kukusanya maoni, ushauri pamoja na kupokea mapendekezo mbalimbali ya namna ya kuboresha masuala ya Kodi. Tume imeingia Mkoani Pwani Januari 29, 2025 ikiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Tume hiyo Maimuna Tarish akiwa na Mjumbe wake Profesa Florens Luoga ambaye pia ni gavana mstaafu wa Benki Kuu ya Tanzania. Wakiwa Mkoani Pwani siku ya kwanza Tume hiyo imekutana na makundi mbalimbali ikiwemo wafanyabiashara, Wawekezaji,Machinga, Wawakilishi vyama vya Wafanyakazi,Taasisi wezeshi,Sekretarieti ya Mkoa wa Pwani,pamoja na wajasiriamali. Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge, akifungua mkutano wa kukusanya maoni hayo uliofanyika Mjini Kibaha amemshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuona umuhimu wa kuunda Tume hiyo. Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge akizungumza wakati akifungua mkutano wa kupokea maoni,ushauri, changamoto na mapendekezo uliokuwa chini ya Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi,mkuta...

COREFA YAUNDA KAMATI ,YATEUA WALEZI KUENDELEZA SOKA ,YAJINASIBU "PWANI LAZIMA MPIRA UCHEZWE"

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani CHAMA cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) kimeunda kamati  mbalimbali sambamba na kuteua walezi mahususi kwa ajili ya kusimamia na kuendeleza michezo katika maeneo yote ndani ya  Mkoa. Kamati hizo zimeundwa Januari 25 kufuatia kikao cha Kamati ya utendaji kilichoketi katika ukumbi wa Seven Seven uliopo The Art Hotel Kibaha MiembeSaba. Mwenyekiti wa Chama Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) Robert Munisi, ametangaza kamati hizo mbele ya viongozi wa FA kutoka Wilaya  zote  katika mkutano maalum na kwanza wa COREFA ulioitishwa kwa ajili ya kupeana miongozo ya  namna ya kuendeleza Soka la Pwani. Mwenyekiti wa Chama Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) Robert Munisi akizungumza na viongozi wa FA katika mkutano maalum uliofanyika The Art Hotel (Seven Seven) Januari 25 mwaka huu. Katika mkutano huo Munisi, amesema COREFA tayari mpaka sasa imeunda kamati Sita ikiwemo kamati ya fedha na mipango iliyo chini ya mwenyekiti wake Moham...

RAIS SAMIA ATANGAZA KIBAHA MJINI KUWA MANISAPAA,MBUNGE KOKA AFURAHIA ASEMA KIBAHA ITANG'AA

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan ameridhia Halmashauri ya Mji Kibaha iliyopo Mkoani Pwani kupandishwa hadi na kuwa Manispaa. Uamuzi huo umetangazwa leo Januari 27 na Waziri wa Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa Mjini Kibaha. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Mohamed Mchengerwa akizungumza katika mkutano wa CCM uliofanyika Januari 27 katika viwanja vya stendi ya zamani Mailimoja Kibaha Mkoani Pwani. Mchengerwa, ametangaza hilo wakati akizungumza na wanachama wa CCM pamoja na Wananchi katika mkutano mkubwa wa kuunga mkono maazimio ya mkutano Mkuu wa CCM Taifa uliomteua Rais Samia kuwa mgombea wa Urais mwaka 2025. Wanachama wa CCM pamoja na Wananchi mbalimbali walioshiriki mkutano wa kuunga mkono azimio la Mkutano Mkuu wa Taifa CCM la kumteua Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea pekee wa Urais kupitia CCM katika uchaguzi wa mwaka 2025, Mkutan...

BARAZA LA WAFANYAKAZI OFISI YA MWANASHERIA MKUU LAKUTANA KUFANYA TATHMINI YA UTENDAJI KAZI MWAKA 2024/2025.

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani BARAZA  la wafanyakazi la ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali limekutana katika kikao chake cha kwanza kwa ajili ya kujadili masuala  mbalimbali yatakayosaidia kurahisisha utendaji kazi na kutoa huduma za kisheria kwa wananchi. Kikao hicho kimeanza kufanyika  juzi katika Chuo Cha uongozi cha Mwalimu Nyerere kilichopo Kibaha kwa Mfipa Mkoa wa Pwani kwa kuwashirikisha wajumbe mbalimbali wakiwemo wakuu wa vitengo,wakurugenzi wasaidizi ,wakuu wa divisheni,mawakili wa Serikali na wajumbe wa Tughe. Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali uliofanyika leo Januari 24,2025 katika Chuo cha uongozi cha Mwalimu Nyerere kilichopo Kibaha Mkoani Pwani. Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) Hamza Johari, amesema kuwa lengo la kukutana katika kikao hicho ni kufanya tathmini ya namna ambavyo utendaji kazi wao ulivyokuwa katika kipindi cha mwaka uliopita na namna wakatavyoendelea mwaka 2025. Johari, amesema kuwa ni wazi kuwa mwaka uliopita...

JESHI LA POLISI MKOA WA PWANI LAMSHIKILIA ALIYETENGENEZA NA KUSAMBAZA PICHA CHAFU ZA UTUPU MITANDAONI.

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani JESHI la Polisi Mkoa wa Pwani limefanikiwa kumkamata mtu mmoja ambaye anadaiwa kutengeneza na kusambaza katika mitandao ya kijamii picha chafu za utupu zisizo za maadili jambo ambalo ni kinyume na Sheria ya nchi. Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani ACP Salim Morcase, amewaambia Waandishi wa habari  Januari 20, 2025 kuwa kitendo kilichofanywa na mtuhumiwa huyo hakiwezi kuvumilika kwa nchi yenye maadili mema kama ya Tanzania kwakuwa jambo hilo ni kinyume na Sheria za nchi. Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani ACP Salim Morcase akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu tukio la kukamatwa kwa mtuhumiwa aliyetengeneza na kusambaza picha za utupu katika mitandao ya kijamii. Morcase, amesema kuwa picha hizo chafu na zisizo za kimaadili waliotengeneza waliunganisha na baadhi ya majengo ya Shule ya Baobab ili kuaminisha Umma kuwa vitendo hivyo vinafanyika Shuleni hapo. Kamanda Morcase, amesema kuwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani Januari 3, 2025 lilipokea taar...

COREFA YATOA BARAKA KWA VIJANA 16 WALIOCHAGULIWA NA FIFA KUJIUNGA NA KAMBI YA TANGA,YAWAASA WAZAZI KULINDA VIPAJI VYA WATOTO WAO.

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani CHAMA cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani ( COREFA) chini ya mwenyekiti wake Robert Munisi kimekutana na wazazi wa  vijana 16 walioteuliwa na FIFA pamoja na TFF kwa ajili ya kuwatakia heri ya kwenda kujiunga na kambi ya FIFA na TFF inayofanyika Mkoani Tanga kuanzia Januari 12 hadi Januari 18 mwaka huu. Kikao cha COREFA, wazazi, na vijana hao kimefanyika Januari 11,2025 katika ofisi za chama hicho zilizopo Kibaha kwa Mathias ambapo moja ya malengo ya kikao hicho ni kuwaaga vijana hao kwa heshima pamoja na kuwahakikishia wazazi usalama wa watoto wao na umuhimu wa Kambi hiyo. Vijana 16 walioteuliwa na FIFA kujiunga na kambi ya wiki moja Mkoani Tanga wakiwa na wazazi wao katika ofisi ya COREFA iliyopo Mjini Kibaha chini ya uongozi wa mwenyekiti Robert Munisi  "COREFA imepata heshima kubwa kutoka FIFA na TFF kwa kuchagua vijana wetu 16 kwenda katika Kambi ya Tanga kwahiyo tukaona sio vyema vijana hawa wakaondoka bila utaratibu,niwaambie tu vijana wenu wapo sala...

MANARA AZINDUA MASHINDANO YA SAMIA CUP KIBAHA VIJIJINI, ACHANGIA SH.MILIONI 1

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani MDAU wa mpira wa miguu Nchini Haji Manara, ameahidi kutoa kiasi cha Sh. milioni 1 kwa ajili ya kuchangia  mashindano ya kombe la Samia "Samia Cup" yanayofanyika katika Halmashauri ya Kibaha Vijijini chini ya uratibu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilayani humo.  Manara ametoa  ahadi hiyo kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Mtongani uliopo  Mlandizi Kibaha wakati akizindua michuano hiyo Januari 11,2025 ambayo inashirikisha timu 104 kutoka katika Kata zote za Halmashauri ya Wilaya hiyo. Mdau wa michezo Haji Manara akizungumza katika ufunguzi wa Mashindano ya Samia Cup yaliyofanyika Januari 11 ,2025 katika viwanja vya Mtongani Mlandizi Kibaha Vijijini,Kulia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC) Hamoud Jumaa na kushoto ni mwenyekiti wa CCM Kibaha Vijijini Mkali Kanusu pamoja na mwenyekiti wa Chama Cha Mpira wa Miguu ( COREFA) Robert Munisi. Kwa mujibu wa Manara amesema kuwa  lengo la mashindano hayo ni kuhamasisha w...

DIPLOMASIA YA RAIS SAMIA YAZAA MATUNDA

Image
Na Gustaphu Haule, Tanzania  *●Yawaleta Wakuu wa nchi Afrika kushiriki Mkutano wa M300* IMEELEZWA kuwa Tanzania imechaguliwa kuwa mwenyeji wa Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika ujulikanao kama Mission 300 kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo diplomasia ya kiuchumi chini ya uongozi wa Rais, Dkt.Samia Suluhu Hassan  Hayo yamesemwa Januari 10, 2025 na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt.Doto Biteko wakati akizungumzia Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika utakaofanyika Januari 27 na 28  2025 jijini Dar es Salaam. “Rais, Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan amefanya kazi kubwa sana ya kuitangaza Tanzania kimataifa, hii imepeleka taasisi za kimataifa, kampuni na wawekezaji kuona Tanzania kuwa ni sehemu sahihi ya kufanya biashara na uwekezaji na mfano halisi ni Benki ya Dunia na Benki ya Maendeleo Afrika kuichagua Tanzania kufanya mkutano huu mkubwa wa kimataifa utakaohudhuriwa na viongozi kutoka nchi 54 barani Afrika.” Amesema Dkt. Biteko Ameongeza kuwa, sab...