Posts

Showing posts from November, 2024

SERIKALI YA RAIS SAMIA YAONDOA MALALAMIKO YA WAGONJWA ULANGA.

Image
Na Gustaphu Haule, Tanzania  #KAZIINAONGEA HATUA ya Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kukamilisha ujenzi wa kituo cha kupoza umeme cha Ifakara imesaidia kwa kiasi kikubwa kuondoa malalamiko ya wananchi ya kuchelewa kupata huduma za afya kwenye hospitali ya Wilaya ya Mahenge. Kituo cha kupoza umeme cha Ifakara Hayo yamethibitishwa na Katibu wa afya Hospitali ya Wilaya ya Ulanga, Goodluck Malya ambae amesema kabla ya kuwepo kwa huduma ya nishati kutoka kwenye kituo hicho hali ilikuwa ni mbaya kwani kuna huduma zilikuwa hazipatikaniki lakini pia gharama za nishati zilikuwa za juu kutokana na kutumia genereta. "Toka kuwashwa kwa kituo cha kupoza umeme Ifakara hospitali ya wilaya ya Ulanga imeona mabadiliko makubwa kwa huduma mbalimbali zinazotegemea nishati ya umeme zimekuwa na mafanikio makubwa,"amesema Malya "Awali kuna mambo yalikuwa hayawezi kufanyika na hospitali ilikuwa ikiingia gharama kubwa katika shughuli za uendeshaji hasahasa katika nishati ya umeme lakini b...

SERIKALI YAPUNGUZA VIFO VYA WAJAWAZITO KWA ASILIMIA 81.

Image
Na Gustaphu Haule, Tanzania. SERIKALI YAPUNGUZA VIFO VYA WAJAWAZITO KWA ASILIMIA 81 *●Ni vya kipindi cha kujifungua* #KAZIINAONGEA  SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, inafanya jitihada za hali na mali kuhakikisha vifo vya wajawazito wakati wa kujifungua vinapungua kwa kiasi kikubwa. Katika kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wa Rais Samia, umeweza kupunguza vifo vya wajawazito wakati wa kujifungua kwa asilimia 81 na hii imetokana na matunda ya uwekezaji sahihi katika kuboresha Sekta ya afya. Takwimu za Wizara ya Afya zinaonyesha kuwa, vifo vya wajawazito kwa mwaka 2016 vilikuwa 556 ambapo hadi kufikia mwaka 2023 vifo hivyo vimepungua na kufikia 104 kwa kila vizazi 100. Miongoni mwa sababu zinazotajwa kuchangiwa kupungua kwa vifo hivyo ni pamoja na mtindo wa maisha wenye afya unaozingatia lishe bora, mazoezi na kuepuka vitu vinavyoweza kuwa na madhara kwa mjamzito ili ujauzito uendelee kukuwa vizuri. Serikali ya Tanzania kw...

MUENDELEZO WA KAMPENI YA SIKU 16 KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA KWA MWAKA 2024 - SIKU YA 5

Image
SIKU YA 5: Jamii inawezaje kuwasaidia manusura wa ukatili wa kijinsia kupata haki yao, pamoja                     na  msaada wa kisaikolojia ili waweze kupona kutokana na changamoto walizokutana nazo? Tujue rasilimali zinazopatikana kusaidia Manusura wa Ukatili wa Kijinsia Manusura wa ukatili wa kijinsia wanastahili kupata msaada na ulinzi. Kuna rasilimali nyingi zinazopatikana ili kuwasaidia kupona na kujenga upya maisha yao. Aina za Rasilimali Msaada wa Kisaikolojia:   Ushauri: Wataalamu wa afya ya akili wanaweza kusaidia manusura kushughulikia mkazo, hofu, unyogovu, na hisia nyingine ngumu. Tiba ya kikundi: Kuungana na watu wengine waliopitia hali kama hiyo kunaweza kuwa na manufaa makubwa. Programu za kupona:  Kunaweza kukawa na Programu zitakazoweza kutoa mikakati ya kukabiliana na athari za kiwewe.       2 . Msaada wa Kisheria Mawakili: Wanawez...

SERIKALI YAENDELEA KUPAMBANA NA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI

Image
Na Gustaphu Haule, Tanzania *●Ruvuma yaongoza upimaji na utumiaji dawa* #KAZIINAONGEA JITIHADA za Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan zimezaa matunda baada Mkoa wa Ruvuma kutajwa kuwa kinara kwa watu kujitokeza kupima Virusi vya Ukimwi na utumiaji dawa wa kufubaza Virusi vya ugonjwa huo. Hayo yamebainika wakati Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas akifungua wiki ya maadhimisho ya siku ya Ukimwi  Duniani ambayo Kitaifa yanafanyika Mkoani humo. Kanali Abbas amesema, Wananchi wa Mkoa huo wametajwa kuwa mstari wa mbele kujitokeza kupima Virusi vya Ukimwi pamoja na kutumia dawa za kufubaza virusi hivyo kwa wagonjwa waliobainika kupata maambukizi ya Virusi hivyo. Taarifa hizo pia zimeeleza kuwa, Mkoa huo umefanikiwa kupunguza maambukizi ya HIV ambapo maambukizi mapya yamepungua kwa asilimia 0.7 kutoka asilimia 5.6 mwaka 2017 hadi kufikia asilimia 4.9 mwaka 2022. Mkoa wa Ruvuma umeendelea kufanya vizuri katika viwango vya “95 95 95” ambapo utafiti ...

RC - PWANI AWAONGOZA WANANCHI KUPIGA KURA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge mapema leo saa 2:15 asubuhi amewaongoza wakazi wa Mkoa wa Pwani kupiga kura kwa ajili ya kuwachagua viongozi wa Serikali za Mitaa watakaokaa madarakani kwa muda wa miaka mitano ijayo. Kunenge,amepiga kura katika Mtaa wa Mkoani "A" uliopo Kata ya Tumbi  Halmashauri ya Kibaha Mjini ambapo pamoja na mambo mengine ameeleza kuwa hali ya Mkoa wa Pwani kiusalama ipo shwari. Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge watano mwenye shati ya bluu akipanga mstari kwa ajili ya kupiga kura kuwachagua viongozi wa Serikali ya Mtaa leo Novemba 27 katika kituo cha Mkoani "A" kilichopo Kata ya Tumbi Kibaha Mjini. Amesema, uchaguzi huo ni muhimu kwani unakwenda kutoa viongozi ambao watahudumia Wananchi kwa ukaribu zaidi kwa ajili kuleta maendeleo hivyo ni vyema kila mwananchi ajitokeza kutimiza haki yake ya kikatiba. Amesema, muda wa kupiga kura ni kuanzia saa 2 asubuhi mpaka saa 10 jioni na kwamba muda ukimalizika watu waliop...

TAKUKURU YATOA ONYO KWA WAPIGA KURA NA WAGOMBEA UCHAGUZI SERIKALI YA MTAA

Image
Na Gustaphu Haule, Tanzania  #KAZIINAONGEA SERIKALI ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imewaonya wapiga kura na wagombea kuacha kujihusisha na vitendo vya rushwa  kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji unaotarajiwa kufanyika Novemba 27,2024. Hitaji la Rais Samia ni kuona kunakuwa na uchaguzi wa huru na haki bila kujali ni mgombea wa chama gani atashinda. Kwa kulifanikisha hilo Novemba 26,2024, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Ilala imesema itachuka hatua kwa yeyote atayepokea ,kutoa au kujihusisha na rushwa. Hayo ameyasema Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Ilala Sosthness Kibwengo wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam. "Uchaguzi ni maisha uchaguzi ni maendeleo tunaelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa tufahamu kwamba rushwa ni kikwazo katika maendeleo, rushwa ni kikwazo kufanya uchaguzi ambao upo sahihi, rushwa ni kikwazo katika kukuwezesha wewe katika kuchagua kiongozi ambaye ni bora,"amesema...

SERIKALI YA DKT .SAMIA YATUMIA MILIONI 771.3 KUBORESHA BARABARA HIFADHI YA SERENGETI

Image
Na Gustaphu Haule, Tanzania  *●Lengo ni kuweka mazingira bora kuvutia Watalii* #KAZIINAONGEA SERIKALI ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, inaendelea kutumia fedha na nguvu nyingi katika kuboresha mazingira ya vivutio vya utalii na uwekezaji nchini. Jitihada hizi za Serikali ya awamu ya sita zimeendelea kwa kuleta mafanikio chanya kwa kasi kubwa katika Sekta ya utalii nchini katika kipindi cha miaka mitatu tangu Rais Samia alipoingia madarakani. Miongoni mwa jitihada hizo za Serikali katika kuinua sekta ya utalii ni kwa kuanzisha miradi katika hifadhi ya Serengeti Mkoani Mara ili kuboresha mazingira ya utalii na uwekezaji na hatimaye kuinua kipato cha Taifa. Miradi wa barabara ya utalii kilomita 22 uliogharimu takribani Milioni 761.3 na mradi wa ujenzi wa vituo viwili vya kupokea na kukagua wageni i(Ikona Gate na Visitors  Gate) uliogharimu takribani Shilingi Milioni 143.5 . Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Ikona iliyopo Wilaya ya Serengeti Mkoani Mara ni miongoni mwa miradi ina...

SHAURI YOMBAYOMBA :LAMI KUANZA JANUARI ,NIPENI KURA MZIDI KUFURAHI

Image
Na Gustaphu Haule,Kibaha MGOMBEA wa nafasi ya mwenyekiti katika Mtaa wa Mailimoja" B" uliopo Kata ya Tangini katika Halmashauri ya Mji Kibaha Shauri Yombayomba amewaomba wakazi wa Mtaa huo kuendelea kumuamini katika miaka mitano ijayo. Shauri, ametoa ombi hilo wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wake wa kampeni uliof: anyika katika viwanja vya kanisa la TAG lililopo Mtaa wa Mailimoja "B" Katika mkutano huo Yombayomba amesema kuwa miaka mitano ya kwanza walimuamini na kumchagua lakini alifanyakazi kubwa ya kufungua barabara ambazo miaka mingi hazikupitika. Amesema, awamu hii wakimchagua kasi ya maendeleo itakuwa kubwa ikiwa pamoja na kuendeleza zoezi la kufungua barabara za Mitaa ambazo kwasasa hazipitiki na hivyo kuleta changamoto kwa Wananchi. Ameongeza kuwa ,mbali na kufungua barabara hizo lakini pia Mtaa wake umefanikiwa kupata barabara za lami ikiwemo kutoka kwa kwa Malata kupitia Mailimoja Pharmacy mpaka kufika katika ofisi ya Mtaa na kuunganisha Mina...

MBONI MKOMWA: NITAJENGA SHULE YA MSINGI NA ZAHANATI MTAA WA BAMBA,WANANCHI NICHAGUENI

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani  MBONI Mkomwa ni mgombea wa nafasi ya mwenyekiti katika Serikali ya Mtaa wa Bamba Kata ya Kongowe katika Halmashauri ya Mji Kibaha Mkoa wa Pwani. Mboni, anaingia katika kinyang'anyiro cha nafasi hiyo kwa mara ya kwanza licha ya kuwa awali alikuwa mjumbe wa Serikali ya Mtaa huo kwa muda wa miaka mitano iliyopita. Uzoefu wa Mboni katika kutumikia nafasi hiyo kumempa uzoefu mkubwa katika uongozi na hivyo kuona anaweza kuongoza Mtaa huo kwa nafasi ya mwenyekiti. Kwasasa Mboni (39) ni Mjane na mama wa watoto watatu anayejishughulisha na biashara ndogondogo ambayo kwa kiasi kikubwa ndio inayompa kipato cha kuendesha maisha. Katika mahojiano yake na mwandishi wa makala haya katika moja ya mikutano yake ya kampeni Mboni anaanza kwa kukishukuru Chama Cha Mapinduzi (CCM)kwa kumuamini na kumpa nafasi ya kupeperusha bendera ya Chama hicho. Amesema, mbali na chama hicho lakini pia anawashukuru wanachama wa CCM pamoja na wananchi mbalimbali wa Mtaa wa Bamba kwa kumpa moyo...

RAIS SAMIA APONGEZWA KWA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA NCHINI

Image
Na Gustaphu Haule,Tanzania  #KAZIINAONGEA WAZIRI wa Madini Anthony Mavunde amempongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha mazingira ya biashara nchini, ambapo pia ameikaribisha Jumuiya ya  Wafanyabiashara kutoka Nchini Finland kuwekeza kwenye sekta ya madini.   Amesema  Tanzania imejaaliwa kuwa na rasilimali za kutosha za madini,mazingira ya uwekezaji rafiki na sera zinazotabirika. Waziri Mavunde ameyasema hayo Novemba 20,2024 Masaki Jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano wa kifungua kinywa ulioandaliwa na Ubalozi wa Finland nchini kwa lengo la kuwakutanisha wafanyabiashara wa Madini kutoka Finland na Wizara ya Madini ili kubaini maeneo ya ushirikiano na fursa za kiuchumi zilizopo katika sekta ya madini nchini Tanzania. Akizungumza katika hafla hiyo Balozi wa Finland nchini Tanzania Theresa Zitting amesema Tanzania na Finland ni nchi zenye ushirikiano mkubwa kwenye masuala ya kiuchumi na hivyo ni wakati muafaka sasa kuimarisha mahusiano hayo kupitia uwekezaj...

MAFANIKIO YA RAIS DKT.SAMIA KATIKA USAFIRI WA TRENI YA SGR YAONEKANA.

Image
Na Gustaphu Haule, Tanzania  *● Imesafirisha abiria zaidi ya 1,000,000 katika kipindi cha miezi minne* # KAZIINAONGEA MAFANIKIO makubwa yaliyotokana na jitihada za Rais wa awamu ya tatu Dkt.Samia Suluhu Hassan tangu alipoingia madarakani yameonekana hasa katika kuleta unafuu mkubwa kwa Watanzania kwenye suala zima la usafiri wa Treni ya umeme (SGR) kutoka Dar es Salaam kwenda Morogoro na Dodoma. Kuanzishwa kwa usafiri huo kumesaidia kutoa unafuu katika Sekta ya usafiri ambapo pia Shirika la Reli Tanzania (TRC) limefanikiwa kusafirisha abiria zaidi ya 1,000,000 katika kipindi cha miezi minne tangu uzinduzi wa njia ya Treni za umeme kati ya Dar es Salaam na Dodoma, mnamo Juni 2024. Idadi hiyo ni mara mbili ya abiria waliosafirishwa na Treni ya zamani (MGR) ambayo ilisafirisha jumla ya abiria 400,000 katika kipindi cha mwaka mmoja ambapo kuanzishwa kwa treni ya SGR kumefanya idadi ya abiria wa Treni hiyo kuongezeka siku hadi siku.    Shirika hilo la Reli (TRC) inatambua umuh...