HOSPITALI YA RUFAA TUMBI YATOA HUDUMA YA MACHO BURE

Na Gustafu Haule, Pwani Hospitali ya Rufa ya Mkoa wa Pwani Tumbi iliyopo Kibaha Mkoani Pwani kwa kushirikiana na taasisi ya Qatar Charity imetoa huduma ya upimaji na upasuaji wa macho bure Kwa wananchi zaidi ya 1000 waishio katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo. Huduma hiyo ilianza kutolewa Novemba 15 mwaka huu na kumalizika Novemba 18 ambapo katika huduma hiyo wananchi walipimwa macho na yeyote aliyebainika kuwa na tatizo alipata dawa na wengine kufanyiwa upasuaji bure . Pichani watoa huduma katika Hospitali ya Rufaa Tumbi wakiwa wamejipanga kwa ajili ya kutoa huduma kwa Wananchi Daktari Bingwa wa Macho katika hospitali hiyo Dr.Mathew Yinza, amesema kuwa toka wameanza kutoa huduma hiyo Novemba 15 imekuwa na mwitikio mkubwa wa wananchi kwani mpaka Sasa zaidi ya wananchi 1000 wamejitokeza na kupata huduma. Dr. Nyinza, amesema kuwa mwananchi anayepimwa na kugundulika na ugonjwa wa macho anapata huduma kulingana na hali yake jinsi il...