MAONYO JUU YA KUKITHIRI KWA VITENDO VYA UKATILI NA UKANDAMIZAJI DHIDI YA WAANDISHI WA HABARI



 Na. Mwandishi Wetu.

Raisi wa Muungano wa Klabu za Waandishi wa habari Tanzania Bw. Deogratius Nsokolo ametoa wito kwa umma kuelimishwa juu ya umuhimu wa uhuru wa vyombo vya habari na nafasi ya Waandishi wa habari katika jamii.

 

Ameyazungumza hayo wakati akifungua Mkutano wa Maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya kukomesha uhalifu dhidi ya Waandishi wa habari ulioendeshwa kwa njia ya mtandao (Zoom Meeting).

 

Maadhimisho hayo kwa Mwaka 2023 yamelenga kuongeza uelewa kuhusu changamoto wanazokabiliana nazo Waandishi wa habari katika kutekeleza majukumu yao, na pia kuonya juu ya kukithiri kwa vitendo vya ukatili na ukandamizi dhidi ya Waandishi wa habari.

 

Katika hotuba yake ameelezea mambo muhimu katika jamii kama  Kuimarisha Demokrasia, kulinda haki za Binadamu na  kujenga Mazingira salama kwa Waandishi wa habari.


Comments

Popular posts from this blog

RC PWANI AONGOZA WAKAZI PWANI KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA

BARAZA LA MADIWANI KIBAHA MJINI LAMPONGEZA MKURUGENZI WAKE KWA KAZI NZURI ANAYOIFANYA SAMBAMBA NA KUONGEZA MAPATO.

RAIS SAMIA ATANGAZA KIBAHA MJINI KUWA MANISAPAA,MBUNGE KOKA AFURAHIA ASEMA KIBAHA ITANG'AA