Posts

Showing posts from July, 2025

SHULE YA MSINGI MKOANI YADAI WAZAZI ZAIDI YA SH.MILIONI 168,

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani SHULE ya Msingi mkoani yenye mchepuo wa kiingereza iliyopo kata ya Tumbi katika  Manispaa ya Kibaha Mkoani Pwani ipo katika wakati mgumu wa  kutekeleza majukumu yake kutokana na baadhi ya  wazazi kushindwa kulipa ada kwa wakati. Shule hiyo ya serikali ilianzishwa mwaka 2018 ili kuwawezesha wanafunzi kupata masomo sawa na Shule za Kiingereza za binafsi ( Private) lakini changamoto iliyopo hivi sasa ni wazazi kushindwa kulipa ada ambayo ni Sh.400,000 kwa mwaka. Ada hiyo ni mgawanyo wa mihula miwili ambapo kila baada ya miezi Sita mzazi anatakiwa kulipa Sh.200,000 lakini bado wazazi wanashindwa kulipa jambo ambalo linapelekea uendeshaji wa Shule hiyo kuwa mgumu. Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Adelhelma Chawa akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake juzi amesema kuwa mpaka kufikia Julai 11,2025 shule hiyo inawadai Wazazi kiasi cha Sh.milioni 168,956,000. Mkuu wa Shule ya Msingi Mkoani iliyopo katika Manispaa ya Kibaha Adelhelma Chawa akizungumza na...

93 WAJITOKEZA KUCHUKUA FOMU ZA KUGOMBEA UBUNGE MKOA WA PWANI

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani  WANACHAMA 93 wa Chama Cha Mapinduzi ( CCM) kutoka Mkoani Pwani wamejitokeza  kuchukua fomu za  kuomba kuteuliwa na chama kwa ajili ya kugombea nafasi ya ubunge katika majimbo mbalimbali yaliyopo Mkoani Pwani. Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo wa Mkoa wa Pwani David Mramba ametoa taarifa hiyo Julai 2 ,2025 wakati akizungumza na Waandishi wa habari katika ofisi za CCM Mkoa wa Pwani zilizopo Mjini Kibaha . Mramba amesema kuwa Mkoa wa Pwani una majimbo tisa ambapo tangu dirisha la uchukuaji fomu za kuwania nafasi ya ubunge Mkoa wa Pwani umepata wagombea 93 na kati ya hao Wanaume ni 71 na Wanawake 22. "Mchakato wa uchukuaji fomu na kurudisha kwa ajili ya kuomba ridhaa ya kugombea ubunge katika majimbo ulianza Juni 28 na kumalizika Julai 2, 2025 na katika mchakato huo Pwani wamejitokeza wanaCCM 93 katika majimbo yote tisa",amesema Mramba Mramba ametaja majimbo hayo na idadi ya wagombea  kuwa ni Chalinze yenye wagombea (3) Wanaume akiwemo Ridhiwani...

MANISPAA YA KIBAHA YAFANYA KIKAO KAZI KUIMARISHA UWAJIBIKAJI

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani HALMASHAURI ya Manispaa ya Kibaha imefanya kikao kazi maalum kilichowakutanisha Maafisa Kilimo na Maafisa Maendeleo ya Jamii kwa lengo la kukumbushana wajibu wa kila siku katika kutekeleza majukumu yao ya kiutumishi. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Kibaha Julai 1, 2025 kikilenga kuimarisha utendaji kazi, uwajibikaji, ubunifu katika ukusanyaji wa mapato ya ndani pamoja na utoaji wa huduma bora kwa wananchi. Baadhi ya Watumishi wa Manispaa ya Kibaha wakiwa katika kikao kazi cha kujadili uwajibikaji kazini kilichofanyika jana. Akizungumza wakati wa kikao hicho, Mkurugenzi wa Manispaa ya Kibaha, Dkt. Rogers Shemwelekwa, amewataka watumishi wote kuongeza ubunifu katika kazi zao, kuachana na kufanya kazi kwa mazoea, na kuhakikisha mapato ya ndani yanakusanywa kikamilifu kwa maendeleo ya Halmashauri na wananchi wake. Mkurugenzi wa Manispaa ya Kibaha Dkt.Rogers Shemwelekwa akizungumza katika kikao kazi na watumishi wake kilichofanyika jana katika Uk...