Posts

Showing posts from July, 2025

RAIS SAMIA ATOA SIKU TANO KWA MAMLAKA YA USIMAMIZI WA BANDARI KUHAMISHIA HUDUMA BANDARI KAVU YA KWALA.

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan  ametoa siku tano kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kuhakikisha inapeleka huduma zote muhimu katika Bandari Kavu ya  Kwala ili kurahisisha huduma kwa watumiaji wa Bandari hiyo. Aidha, Rais Samia ameielekeza Wizara ya Uchukuzi kuhakikisha inashirikiana na sekta binafsi kuhamasisha utumiaji wa  miund ombinu ya Bandari Kavu ya Kwala ili  kuondoa msongamano wa malori Jijini Dar es Salaam. Rais Samia ametoa maelekezo hayo Julai 31,2025 wakati akizungumza na Wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kwala Mkoani Pwani mara baada ya kuzindua Bandari Kavu ya Kwala pamoja na kupokea Mabehewa mapya na yaliyokarabatiwa ya MGR. Amesema, kupatikana kwa huduma hizo katika Bandari Kavu ya Kwala itawasaidia wale wanaohitaji huduma hizo wanapofika Vigwaza wanaingia moja kwa moja Kwala na hivyo kuwaondolea usumbufu madereva kwenda Dar es Salaam. "Kutokana na mahitaji muh...

WAZIRI JAFO ASEMA HAKUNA HAJA YA KUFUATA BIDHAA KUTOKA NJE

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani WAZIRI wa Viwanda na Biashara  Dkt. Selemani Jafo ameeleza kuwa ndani ya muda mfupi ujao hakutakuwa na haja ya kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi kwakuwa Tanzania imejiimarisha katika kuzalisha bidhaa zake. Jafo amesema kuwa kwasasa Tanzania inazalisha Bati,Vioo,Nondo,Saruji,TV ,simu  na bidhaa nyingine na kwamba kutokana na hali hiyo hakuna haja ya kufuata bidhaa hizo nje kwakuwa Tanzania inazalisha bidhaa hizo na zenye viwango vya juu.  Jafo ‎amebainisha hayo wakati wa ziara ya Rais Samia Julai 31,2025 mkoani Pwani ambapo alikuwa anafanya uzinduzi wa kongani ya Viwanda Kwala sambamba na uzinduzi wa bandari kavu ya kwala. ‎ Waziri wa Viwanda na Biashara Selemani Jafo akisalimiana na Rais Dkt . Samia Suluhu Hassan wakati alipofanya ziara katika eneo la Kwala katika hafla ya kupokea Mabehewa mapya ya mizigo na uzinduzi wa Bandari Kavu ya Kwala leo Julai 31,2025. ‎"Ndani ya muda mfupi kuanzia sasa hakutakuwa na haja ya kuagiza bidhaa tena kutoka nje k...

HAWA MCHAFU CHAKOMA AIBUKA KINARA UCHAGUZI WA UBUNGE VITIMAALUM MKOA WA PWANI

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani ALIYEKUWA Mbunge wa Vitimaalum kutoka Mkoa wa Pwani Hawa Mchafu Chakoma amefanikiwa kutetea nafasi yake baada ya kujizolea kura 802 na kuwaacha mbali washindani wake. Hawa ameibuka kidedea katika uchaguzi wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania (UWT) uliofanyika Julai 30,2025 katika viwanja vya Shule ya uongozi ya Mwalimu Nyerere iliyopo katika Manispaa ya Kibaha Mkoani Pwani.   Hawa Mchafu pichani akiomba kura kwa wajumbe katika uchaguzi wa Wabunge wa Vitimaalum uliofanyika Julai 30 ,2025 katika Chuo cha uongozi cha Mwalimu Nyerere kilichopo Kibaha Mkoani Pwani  Katika uchaguzi huo Hawa alikuwa akichuana na wenzake Saba lakini hatahivyo amefanikiwa kuwa kinara katika uchaguzi huo  na hivyo kufanikiwa kurudi katika ulingo wa Siasa  kwa nafasi ya ubunge wa Vitimaalum. Wagombea wengine waliokuwa wakichuana na Hawa Mchafu ni Mariam Abdallah ((645),Nancy Mutalemwa (449),Irene Makongoro (56),Fatuma Uwesu(71),Sifa Mwaruka(44) ,Rehema Is...

MAANDALIZI UZINDUZI WA BANDARI KAVU KWALA YANAENDELEA VIZURI.

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge  amesema maandalizi ya uzinduzi wa Bandari Kavu katika eneo la Kwala unaotarajia kufanywa na  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan Julai 31,2025 yanaendelea vizuri. Kunenge, ameyasema hayo wakati akizungumza na Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali Julai 30, 2025 mara baada ya kutembelea na kukagua maandalizi ya uzinduzi huo katika maeneo yote muhimu. Mkuu wa mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge akizungumza na Waandishi wa habari katika eneo la Bandari Kavu ya Kwala iliyopo Kibaha Vijijini Julai inayotarajia kuzinduliwa Julai 31,2025  na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan. Amesema, Mkoa umejipanga vizuri katika kupokea ugeni huo ambapo amemshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kukubali ombi la kuwa mgeni rasmi kwakuwa anafahamu ratiba zake ni ngumu. Kunenge, amesema kuwa Rais Samia akiwa katika eneo la Kwala atafanya shughuli mbalimbali ikiwemo  kuzindua safari rasmi safari  ya ...

RC PWANI AWAFUNDA WATUMISHI MANISPAA YA KIBAHA, AWATAKA WAFANYEKAZI KWA BIDII.

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amefunga mafunzo ya kikao kazi cha Watumishi wa Manispa ya Kibaha kwa kuwataka watumishi hao kujenga tabia ya kufanya kazi kwa bidii ili kuleta matokeo chanya. Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge akizungumza katika kikao kazi cha Watumishi wa Manispaa ya Kibaha kilichofanyika Julai 26 na 27,2025 katika Shule ya uongozi ya Mwalimu Nyerere iliyopo Kibaha kwa Mfipa. Kunenge amesema anatamani kuwe na mfumo wa anayezalisha zaidi alipwe zaidi utaratibu ambao utamfanya kila mtumishi kufanya kazi kwa bidii kuleta matokeo chanya kwa jamii. Kunenge ameyasema hayo Julai 27, 2025 alipokuwa akifunga mafunzo kwa watumishi wa Manispaa ya Kibaha yaliyolenga kufanya tathmini ya  utendaji wa  kazi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya mwaka wa fedha wa 2024/2025 na kuangalia bajeti ya 2025/2026. "Kigezo sio cheti kazini lakini utendaji kazi wako ndio unaotakiwa kazi yako ikiwa nzuri mwisho utaonyesha kwamba imetokana na cheti ...

MHARIRI MAKALA UHURU PUBLICATIONS LTD SELINA WILSON ATETEA NAFASI YAKE KIBAHA.

Image
Na Gustaphu Haule ,Pwani MHARIRI Makala wa Uhuru Publications Ltd ya Jijini Dar es Salaam Selina Wilson Msenga amefanikiwa kutetea nafasi yake ya udiwani wa Vitimaalum katika Manispaa ya Kibaha kwa kupata kura 527. Selina ambaye kwasasa ni awamu yake ya nne kushinda katika nafasi hiyo amekuwa na mvuto wa aina yake kwa Jamii ya Manispaa ya Kibaha licha ya kuwa katika uchaguzi huo amekutana na vipingamizi mbalimbali. Aidha, katika uchaguzi wa UWT uliofanyika Julai 20, 2025 Kata ya Mkuza Kibaha Selina alipewa asilimia chache za ushindi kutokana na mvutano mkali wa kisiasa uliokuwepo kati yake na wapinzani wake lakini iliwaduwaza baadhi ya wanaCCM baada ya kuibuka kuwa mshindi katika uchaguzi huo. Selina Wilson watatu kutoka kulia akiwa pamoja na wagombea wenzake katika uchaguzi wa UWT Manispaa ya Kibaha uliofanyika Julai 20,2025  Licha ya Selina kupewa asilimia chache za ushindi katika uchaguzi huo lakini alijikuta anapenya na kuwa miongoni mwa washindi waliokuwa wanahitajika katika n...

RAIS SAMIA KUZINDUA BANDARI KAVU YA KWALA JULAI 31,2025

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan anatarajia kufanya ziara mkoani Pwani Julai 31, 2025 hususani katika Kata ya Kwala Halmashauri ya Kibaha Vijijini ambapo pamoja na mambo mengine Rais Samia atazindua Kongani ya viwanda ya Kwala yenye viwanda 250. Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge ametoa kauli hiyo Julai 22, 2025 wakati akizungumza na Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali katika mkutano uliofanyika katika jengo la ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani lililopo Manispaa ya Kibaha. Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge katika mkutano na Waandishi wa habari Julai 22,2025  Kunenge amesema kuwa,Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan atafanya ziara katika eneo la Kwala sehemu ambayo Serikali imefanya uwekezaji mkubwa ambapo akiwa katika eneo hilo atafanya mambo mbalimbali makubwa. Amesema Rais akiwa katika eneo la Kwala miongoni mwa shughuli atakazozifanya ni pamoja na  kuzindua safari rasmi ya treni ya Mwendokasi (SGR) ya kubeba Makasha...

MEDIA BRAINS YAWAPIGA MSASA WAANDISHI WA HABARI PWANI

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  WAANDISHI wa habari wa Mkoa wa Pwani wametakiwa kutumia taaluma yao kuwaelimisha Wananchi juu ya umuhimu wa kushiriki  masuala ya uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba mwaka huu. Wito huo umetolewa na Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya habari ya Media Brains iliyopo Jijini Dar es Salaam Jesse Kwayu wakati akifungua mafunzo ya siku moja ya masuala ya uchaguzi kwa Waandishi hao. Mafunzo hayo yaliyofanyika Julai 9, 2025 Mjini Kibaha yaliwashirikisha Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali huku yakiwa chini ya wakufunzi wawili akiwemo mwandishi wa habari mkongwe Absalom Kibanda na Jesse Kwayu. Katika mafunzo hayo Kibanda alifundisha kuhusu masuala ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC),Sheria ya Vyama vya Siasa pamoja na sheria ya uchaguzi ya Rais,Wabunge na Madiwani huku Jesse Kwayu akifundisha wajibu wa Waandishi wa habari katika kuripoti habari za uchaguzi mkuu na masuala ya Jinsia. Mwandishi wa habari wa Channel Ten Margareth Malisa akionyesha ...

SHULE YA MSINGI MKOANI YADAI WAZAZI ZAIDI YA SH.MILIONI 168,

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani SHULE ya Msingi mkoani yenye mchepuo wa kiingereza iliyopo kata ya Tumbi katika  Manispaa ya Kibaha Mkoani Pwani ipo katika wakati mgumu wa  kutekeleza majukumu yake kutokana na baadhi ya  wazazi kushindwa kulipa ada kwa wakati. Shule hiyo ya serikali ilianzishwa mwaka 2018 ili kuwawezesha wanafunzi kupata masomo sawa na Shule za Kiingereza za binafsi ( Private) lakini changamoto iliyopo hivi sasa ni wazazi kushindwa kulipa ada ambayo ni Sh.400,000 kwa mwaka. Ada hiyo ni mgawanyo wa mihula miwili ambapo kila baada ya miezi Sita mzazi anatakiwa kulipa Sh.200,000 lakini bado wazazi wanashindwa kulipa jambo ambalo linapelekea uendeshaji wa Shule hiyo kuwa mgumu. Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Adelhelma Chawa akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake juzi amesema kuwa mpaka kufikia Julai 11,2025 shule hiyo inawadai Wazazi kiasi cha Sh.milioni 168,956,000. Mkuu wa Shule ya Msingi Mkoani iliyopo katika Manispaa ya Kibaha Adelhelma Chawa akizungumza na...

93 WAJITOKEZA KUCHUKUA FOMU ZA KUGOMBEA UBUNGE MKOA WA PWANI

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani  WANACHAMA 93 wa Chama Cha Mapinduzi ( CCM) kutoka Mkoani Pwani wamejitokeza  kuchukua fomu za  kuomba kuteuliwa na chama kwa ajili ya kugombea nafasi ya ubunge katika majimbo mbalimbali yaliyopo Mkoani Pwani. Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo wa Mkoa wa Pwani David Mramba ametoa taarifa hiyo Julai 2 ,2025 wakati akizungumza na Waandishi wa habari katika ofisi za CCM Mkoa wa Pwani zilizopo Mjini Kibaha . Mramba amesema kuwa Mkoa wa Pwani una majimbo tisa ambapo tangu dirisha la uchukuaji fomu za kuwania nafasi ya ubunge Mkoa wa Pwani umepata wagombea 93 na kati ya hao Wanaume ni 71 na Wanawake 22. "Mchakato wa uchukuaji fomu na kurudisha kwa ajili ya kuomba ridhaa ya kugombea ubunge katika majimbo ulianza Juni 28 na kumalizika Julai 2, 2025 na katika mchakato huo Pwani wamejitokeza wanaCCM 93 katika majimbo yote tisa",amesema Mramba Mramba ametaja majimbo hayo na idadi ya wagombea  kuwa ni Chalinze yenye wagombea (3) Wanaume akiwemo Ridhiwani...