Posts

Showing posts from May, 2025

TAKUKURU PWANI YAOKOA ZAIDI YA SH. MILIONI 385 ZA KIJIJI CHA MSUFINI MKURANGA.

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani  TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Pwani imefanikiwa kuokoa zaidi ya Sh.milioni 385  zilizopotea kupitia akaunti feki ya Kijiji cha Msufini Kidete Wilayani Mkuranga Mkoani Pwani  Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Pwani Domina Mukama, ametoa taarifa hiyo leo Mei 29, 2025 katika mkutano wake na Waandishi wa habari ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu yake katika kipindi cha Januari- Machi 2025. Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Pwani Domina Mukama akizungumza na Waandishi wa habari Mei 29,2025 Mjini Kibaha ikiwa sehemu ya utekelezaji wa majukumu yake katika kipindi cha Januari-Machi 2025 Mukama, amesema kuwa katika kipindi hicho Takukuru Mkoa wa Pwani ilifanya uzuiaji wa vitendo vya  rushwa ambapo moja ya vitendo hivyo ni kufanikiwa kuokoa mapato ya asilimia 10 ya mauzo ya ardhi ya Halmashauri ya Kijiji cha Msufini Kidete Wilayani Mkuranga. Mukama, amesema kuwa fedha hizo ambazo ziliwekwa kwenye akaunti feki ya Kijiji hicho iliyogh...

MAPEPELE AWANOA MAAFISA HABARI WA TAMISEMI, ATAKA WAWE WAZALENDO

Image
Na Mwandishi Wetu Mkuu wa Kitengo Cha Mawasilino Serikali na Msemaji Mkuu wa Wizara ya TAMISEMI, John Mapepele ametoa wito kwa Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri zote nchini kutanguliza uzalendo na weledi wakati wa utoaji wa taarifa ili habari hizo ziwe na tija kwa taifa. Mapepele ametoa wito huo mwisho mwa wiki jijini Dodoma   wakati akiwasilisha mada kuhusu Mawasilino ya Kimkakati ya Kutangaza mafanikio ya Sekta za Afya, Elimu na Miundombinu chini ya TAMISEMI kwa Maafisa Habari  zaidi ya 200 wa Mikoa na Halmashauri zote nchini kwenye kikao kazi kilichoratibiwa na Wizara hiyo. Kikao kazi hicho kilichofunguliwa  na  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mohamed Omary Mchengerwa na kufungwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa pamoja na mambo mengine kimejadili mikakati mbalimbali ya kutangaza mafanikio ya Serikali. Pia katika kikao hucho Maafisa habari hao wamejengewa uwezo kwa mada mbalimba...

RC PWANI ASEMA, PWANI INAFURSA NYINGI ZA UWEKEZAJI, MIUNDOMBINU KUBORESHWA ZAIDI.

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amefungua mkutano wa Baraza la Biashara la Mkoa wa Pwani huku akiwahakikishia wawekezaji wakimataifa na  wafanyabiashara wa ndani kuwa Serikali imejipanga kuendelea kuboresha miundombinu ya uwekezaji. Kunenge, ametoa kauli hiyo Mei 22, 2025 katika mkutano uliofanyika Mjini Kibaha na  kuwashirikisha wadau mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara wa sekta binafsi, wakuu wa taasisi za Umma, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na Maafisa biashara wa Halmashauri. Mkuu wa mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge akifungua mkutano wa Baraza la Biashara la Mkoa wa Pwani lililofanyika Mei 22,2025 Mjini Kibaha  Kunenge, amesema kuwa Mkoa wa Pwani unafursa nyingi za uwekezaji ikiwemo katika Viwanda, Kilimo, Ufugaji, Uvuvi, Utalii na hata katika biashara mbalimbali ambapo ametaka wawekezaji kuja kwa wingi kwakuwa Serikali tayari imeweka mazingira rafiki kwao. Amesema kuwa, Serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ...

MBUNGE DR .ALICE KAIJAGE AKABIDHI MITUNGI YA GESI 200 KWA WAFANYAKAZI WA AJIRA MPYA PWANI

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani MBUNGE wa viti maalum kupitia wafanyakazi Dr .Alice Kaijage amekabidhi jumla ya mitungi ya gesi ya  Oryx  200 kwa ajili ya kuwawezesha wafanyakazi wa Mkoa wa Pwani waliopo katika ajira mpya. Dr.Kaijage amekabidhi mitungi hiyo leo Mei 22, 2025 kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Rashid Mchatta hafla ambayo imefanyika katika jengo la ofisi ya Mkuu wa mkoa Pwani . Awali akizungumza kabla ya kukabidhi mitungi hiyo Dr.Kaijage amesema kuwa amefanya hivyo kwa ajili ya kumuunga mkono Rais wa awamu ya Sita Dr.Samia Suluhu Hassan ambaye ndiye kinara wa Nishati Safi Duniani,Afrika na Tanzania. "Nimekuja kumuunga mkono Rais Samia kwa suala nzima la Nishati Safi na hizi gesi katoa yeye na mimi nimwakilishi wake kwa upande wa wafanyakazi ambapo lengo kubwa ni kuhakikisha kampeni ya  matumizi ya Nishati Safi inawafikia watu wote," amesema Kaijage. Aidha, Dr Kaijage amesema kuwa amekabidhi mitungi ya gesi hiyo akiwahamasisha watumishi wa mikoa mbalimbali hapa nchin...

WANANCHI KITONGOJI CHA KWAKIBOSHA MAPINGA WAMCHARUKIA PETER JUNIOR ANAYETAKA KUVUNJA NYUMBA ZAO, WAMUOMBA RAIS SAMIA KUINGILIA KATI

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  WANANCHI wa Kitongoji cha Kwakibosha katika Kata ya Mapinga Bagamoyo Mkoani Pwani wameiomba Serikali kumchukulia hatua za kisheria Peter Junior ambaye anadaiwa kutaka kupora ardhi sambamba na kuvunja nyumba za wakazi wa eneo hilo. Wamemuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kuingilia kati jambo hilo ili kusudi kuwafanya Wananchi hao kuishi kwa amani na utulivu na hivyo kuondokana na taharuki iliyopo hivi sasa. Wametoa ombi hilo katika mkutano wao maalum wa kuzungumza na Waandishi wa habari juu ya kutoa kero hiyo ikiwa ni sehemu ya kuiomba Serikali kutafuta ufumbuzi juu ya mgogoro huo ambao hauna afya kwa maisha yao. katika mkutano huo uliofanyika Mei 20, 2025 katika Kitongoji hicho mmoja wa Wananchi hao Elias Kashaga, amesema kuwa anashangazwa kuona Peter Junior amekuwa akiwasumbua na kutaka kupora eneo lao kinyume na utaratibu. Mwananchi wa Kitongoji cha Kwa Kibosha kilichopo Kata ya Mapinga Bagamoyo Mkoani Pwani Elias Kasha...

WANACHAMA CCM NYANG'HWALE WASIKITISHWA KUKWAMA KWA UJENZI WA OFISI YAO ,WATAKA FEDHA ZILIZOCHANGWA ZITUMIKE KUKAMILISHA OFISI HIYO.

Image
Na Mwandishi wetu, Geita  BAADHI ya Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Nyang'hwale Mkoani Geita wameeleza kusikitishwa na kitendo kinachofanywa na baadhi ya viongozi wa chama hicho kukwamisha ujenzi wa jengo la ofisi ya CCM Wilayani humo. Wamesema viongozi hao ,wamekuwa wakitoa sababu ya kukosa fedha za kuendeleza ujenzi wa ofisi hiyo ili hali zipo fedha kutoka kwa wadau pamoja na mmoja wa viongozi wakubwa ambazo zimewekwa bila kutumika ndani ya miezi mitatu sasa. Wanachama hao wamewaambia Waandishi wa habari Mei 03,2025 kuwa mpaka sasa wanafahamu kuwa mmoja wa kiongozi ambaye ni Naibu Waziri Mkuu Dkt.Dotto Biteko tayari amechangia fedha zinazokadiriwa kuwa Sh. milioni 50  lakini hazijatumika . Kwa mujibu wa wanachama hao wamesema kuwa fedha za mchango kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu zilipokelewa na Mbunge wa Jimbo la Nyang'hwale Hussein Nassoro Amar miezi mitatu iliyopita lakini mpaka sasa hakuna kazi iliyofanyika. Wamesema kuwa,fedha hizo zilitolewa ili kukamilish...

SERIKALI YAZIDI KUTEKELEZA MIRADI YENYE TIJA KWA NCHI

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt.Doto Biteko amesema dhamira ya Serikali ni kutekeleza mradi mkubwa wa Kuchakata na kusindika gesi asilia (LNG) ili kuleta faida za kiuchumi. Aidha, kwa sasa kuna maeneo ambayo Serikali inayafanyia kazi kwa kina kupitia majadiliano na Wawekezaji ili mradi husika uwe na tija kwa nchi na wananchi. Ameyasema hayo hivi karibuni bungeni jijini Dodoma wakati akijibu hoja mbalimbali zilizotolewa na Wabunge kuhusu Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati ya shilingi Trilioni 2.2 kwa mwaka 2025/2026 kabla ya kupitishwa kwa kishindo na Bunge hilo kwa asilimia 100. “ Mradi wa LNG umeanza kusemwa kwa muda mrefu na kila mmoja angetamani mradi huu ukamilike jana lakini lazima tukubaliane kuwa lazima tujadiliane kwa kina na wawekezaji ili kupata kilicho bora na kuleta tija, ninachotaka kuwahakikishia ni kuwa timu ya majadiliano ya Serikali na Wawekezaji wanaendelea na majadiliano na tunatarajia kuwa ndani ya mwaka huu 2025 kama tut...