MWEKEZAJI KEDA CERAMICS CO LTD AWAUNGANISHA WANANCHI MBEZI -SHUNGUBWENI, ATOA MILIONI 150 KUJENGA DARAJA,WANANCHI WAFURAHIA UWEKEZAJI HUO.
Na Gustaphu Haule,Pwani
WAWEKEZAJI wa kiwanda cha KEDA (T) Ceramics Co Limited kilichopo Mkiu Wilayani Mkuranga wameendelea kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kujenga daraja kubwa katika Mto Msolwa uliopo barabara ya Mbezi Msolwa inayounganisha Kata ya Mbezi na Shungubweni.
Viongozi wa Kiwanda cha Keda Ceramics Co Ltd wakiwa eneo la ujenzi wa daraja la Mbezi -Shungubweni Wilayani Mkuranga Mkoa wa Pwani.
Utekelezaji wa ujenzi wa daraja hilo ni sehemu ya kukamilisha ahadi ya mwekezaji wa kiwanda hicho ambapo awali aliwaahidi Wananchi wa maeneo hayo kuwajengea daraja hilo ili waweze kupata mawasiliano kwa urahisi ikiwa pamoja na kusafirisha mazao yao.
Aidha, daraja hilo limejengwa likiwa na urefu wa Mita Sita, upana wa Mita Saba na kina cha Mita 1.5 ambapo fedha za utekelezaji wa mradi huo zimetoka katika kiwanda hicho ikiwa ni sehemu ya kurudisha fadhila kwa jamii na hivyo kufanya Wananchi wanaoishi karibu na uwekezaji huo kunufaika.
Muonekano katika picha wa Mradi wa Ujenzi wa Daraja katika Mto Msolwa katika barabara ya Mbezi Msolwa inayounganisha Kata ya Mbezi na Shungubweni.
Akizungumza katika eneo la mradi huo afisa biashara wa kiwanda cha Keda Masoud Suleyman amesema mradi huo wa kuimarisha miundombinu ya barabara utawezesha kata ya Mbezi- Shungubweni kurahisisha shughuli za kiuchumi na huduma za kijamii kwa wananchi wa kata hizo na kurahisisha usafirishaji wa malighafi ya mchanga katika utengenezaji wa bidhaa ya kioo.
Afisa biashara wa kiwanda cha KEDA CERAMICS CO LTD Bw. Masoud Suleyman
"Gharama za mradi umetekelezwa kwa kutumia fedha za ufadhili wa kiwanda cha KEDA ceramics (T) Co Ltd kwa mwaka 2024 gharama ya mradi ikiwa ni Tsh . milioni 150 ambapo utekelezaji wa mradi huo umejengwa kwa kutumia wataalamu,vifaa na malighafi za kiwanda cha Keda Ceramic," amesema Suleyman
Suleyman, amesema kuwa utekelezaji wa mradi huo umeanza tangu Oktoba 28,2024 kwa kushirikiana na wataaalamu kutoka ofisi ya Meneja Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA)Wilaya ya Mkuranga ambapo vifaa na malighafi za ujenzi wake vimetolewa na Keda Ceramics (T) Ltd.
Eneo la ujenzi wa daraja katika Kijiji cha Msolwa Kata ya Mbezi lililojengwa na mwekezaji wa kiwanda cha Keda Ceramic Co Ltd kilichopo Mkiu Wilayani Mkuranga Mkoa wa Pwani.
Amesema kukamilika kwa daraja hilo imekuwa ni mkombozi na kuleta manufaa makubwa kwani mradi huo utawezesha wananchi kupita kiurahisi kipindi chote cha mwaka ikiwemo kipindi cha mvua .
Kwa upande wao baadhi ya wananchi katika VAjeijiji tofauti vilivyonufaika na mradi huo akiwemo Mohammed msumi mkazi wa Kitongoji cha Kikopi Kijiji cha Msolwa anasema walikuwa wakipata tabu kuvuka katika eneo hilo haswa katika kipindi cha mvua.
"Wakati wa mvua maji yalikuwa yanajaa na Watu kushindwa kupitia hivyo Vijana wa maeneo haya walikuwa wakivusha watu kwa pesa lakini baada ya mwekezaji huyu wa Keda kuona changamoto hii waliamua kutusaidia kulijjenga daraja hili katika ubora mzuri na sasa tunapita kwa urahisi zaidi bila shida yoyote,"amesema Msumi.
Aidha Msumi ametumia nafasi hiyo kuwashukuru wawekezaji kutoka Keda Ceramic huku akiwakaribisha wawekezaji wengine waendelee kujitokeza kwa ajili ya kusaidia kutatua changamoto mbalimbali ikiwemo ya ujenzi wa barabara ya Mbezi -Shungubweni na hata katika Sekta ya elimu,na afya.
Nae Amina Juma amewashukuru wawekezaji wa Keda kwa kuwajengea daraja ambalo lilikuwa korofi wakati wa mvua huku akisema eneo hilo lilikuwa linajaa maji ambapo wananchi ,magari kukwama kwa kushindwa kupita hali iliwanyima usingizi wananchi wanaotumia barabara hiyo kwa muda mrefu na kusababisha kurudisha nyuma maendeleo yao.
Jumanne Mtambwe ni mwenyekiti wa kijiji cha Kisayani Mkuranga amesema wanafurahia ujenzi huo kwakuwa daraja hilo limewaunganisha kati ya Kjiji cha Kisayani, Msolwa na Shungubweni amesema ujenzi huo utaleta chachu ya maendeleo kwakuwa barabara zitapitika vizuri kwakuwa mwanzoni daraja lilikuwa bovu halipitiki.
Hatahivyo,Mtambwe ameushukuru uongozi wa Keda kwa kufanikisha ujenzi wa daraja hilo lakini pia amewaomba wawajengee barabara ambayo kwa sasa inasumbua kutokana na kasi ya magari yanayobeba mchanga ambao ni malighafi ya kutengenezea vioo ambayo inatumika katika kiwanda chao.
Hatahivyo,Mtambwe ameushukuru uongozi wa Keda kwa kufanikisha ujenzi wa daraja hilo lakini pia amewaomba wawajengee barabara ambayo kwa sasa inasumbua kutokana na kasi ya magari yanayobeba mchanga ambao ni malighafi ya kutengenezea vioo ambayo inatumika katika kiwanda chao.
Comments
Post a Comment