WAFANYABIASHARA WADOGO DODOMA WAMPONGEZA RAIS SAMIA, WASEMA MACHINGA COMPLEX NI MKOMBOZI WA MAISHA YAO



Na Gustaphu Haule, Tanzania 

#KAZIINAONGEA

WAFANYABIASHARA  wadogo jijini Dodoma, wameipongeza dhamira ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kutaka kuwaondolea umasikini.

Pongezi za wafanyabiashara hao zimekuja mara baada ya Rais Samia kuweka jitihada za kuwatengea mazingira mazuri ya kufanyia biashara zao.

Wafanyabiashara waliompongeza Rais Samia wanatoka katika  Soko la Machinga Complex Jijini Dodoma   ambao wanasema Rais Samia amewafanya waishi katika maeneo mazuri na salama Kwa biashara zao.



Wamesema kuwa kwa namna alivyowahamisha kutoka barabarani walipokuwa wanafanyia biashara zao na kuwajengea soko maalum maarufu kama Machinga imekuwa ni msaada mkubwa kwao tofauti na awali waliokuwa wanafanya biashara kiholela.

 Kaimu mwenyekiti wa Machinga Complex, Lucas Kingamkono, ameishukuru serikali ya Rais Samia huku akisema  uwepo wa soko la Machinga limerahisisha ufanyaji wa biashara kwa wafanyabiashara  wadogo wa Mjini Dodoma.

Kingamkono ,amesema kuwa awali  walikuwa wanafanya biashara katika  maeneo ambayo hayakuwa rasmi na hivyo kufanya biashara kwa mashaka.

Nae Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Anthony Mavunde ameupongeza uongozi wa soko kwa kuandaa mkutano wa kusikiliza kero za wafanyabiashara ambapo pamoja na mambo mengine ameahidi kutunisha mfuko wa soko kwa kuchangia Shilingi Milioni 10.  

Mavunde ameahidi kusaidia upatikanaji wa mikopo kwa wafanyabiashara hao kupitia asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji na taasisi za fedha na kutumia fursa hiyo kuwataka askari mgambo wa Jiji kuacha kutumia mabavu makubwa kushughulika na wafanyabiashara hao.

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Alhaj Jabir Shekimweri ameahidi kusimamia na kushughulikia utatuzi wa kero na changamoto zinazowakabili wafanyabiashara wa soko la Machinga Complex ili kuweka mazingira bora ya biashara.

Club News Editor

Comments

Popular posts from this blog

BARAZA LA MADIWANI KIBAHA MJINI LAMPONGEZA MKURUGENZI WAKE KWA KAZI NZURI ANAYOIFANYA SAMBAMBA NA KUONGEZA MAPATO.

RAIS SAMIA ATANGAZA KIBAHA MJINI KUWA MANISAPAA,MBUNGE KOKA AFURAHIA ASEMA KIBAHA ITANG'AA

RC PWANI AFURAHISHWA NA UTENDAJI KAZI WA MKURUGENZI WA KIBAHA MJINI DKT.ROGERS SHEMWELEKWA