SHAURI AFUNGUA DIRISHA UCHUKUAJI FOMU UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA



Na Gustaphu Haule 

MGOMBEA wa nafasi ya  Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Mailimoja "B" kupitia Chama Cha Mapinduzi" CCM" Shauri Yombayomba  tayari amechukua fomu kwa ajili ya kuwania nafasi hiyo.

Yombayomba amechukua fomu hiyo mapema leo Oktoba 28 katika ofisi za Mtaa huo akiambatana na wajumbe wake watano akiwemo Webina Gimasa, Josephu Sanga, Mwanaidi Ndotia, Omari Mfaume na Zainabu Charles.

Mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti Serikali ya Mtaa Mailimoja B Shauri Yombayomba (CCM) akipokea fomu kutoka kwa Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi katika Mtaa huo Suzana Awiti leo Oktoba 28, 2024

Miongoni mwa viongozi alioongozana nao ni Mwenyekiti wa CCM tawi la Yombayomba, Amina Musa, Katibu wa tawi Kizito Iyulu na Katibu wa itikadi uenezi na mafunzo Chedy Shaban.

Akiwa ofisini hapo Yombayomba alikabidhiwa fomu hiyo na msimamizi Msaidizi wa uchaguzi Mtaa wa Mailimoja "B" Suzana Awiti ambaye alimueleza mgombea huyo kuwa ofisi hiyo inakuwa wazi mpaka saa 10 jioni.

Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu hiyo Yombayomba amesema amechukua fomu hiyo pasipo changamoto yoyote kutokea huku akiwashukuru viongozi wa CCM kwa ushirikiano mkubwa wanaotoa.

Yombayomba, amesema kuwa zoezi la kuchukua fomu limepita lakini zipo hatua nyingine ambazo zinafuata ikiwemo kurudisha fomu na hata kusubiri michakato mingine inayofuata.

Amewaomba Wananchi wa Mtaa wa Mailimoja B kuendelea kumpa  ushirikiano yeye binafsi na kwa chama chake na kwamba endapo atashinda nafasi hiyo utakuwa ushindi wa Wananchi wote.

Mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti Serikali ya Mtaa wa Mailimoja B Shauri Yombayomba akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe na viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) tawi la Yombayomba mara baada ya kuchukua fomu katika Ofisi ya Serikali ya Mtaa Mailimoja B leo Oktoba 28, 2024


"Leo nimekuja hapa katika ofisi zetu za Mtaa kwa ajili kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya kuwa mwenyekiti wa Mtaa huu, nimepata ridhaa ya Chama changu kwakuwa kimeniamini na mimi natumia nafasi hii kuomba ushirikiano ndani ya Chama changu na hata nje ya chama,"amesema Yombayomba 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM tawi la Yombayomba Amina Musa, amesema kuwa ndani ya Chama tayari wamepata mgombea lakini uchaguzi bado haujaisha hivyo amewaomba wanaCCM na wananchi wote kukiunga mkono CCM katika hatua zinazofuata.

Zoezi la kuchukua fomu kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa zimeanza leo Oktoba 28 hadi Novemba 1 huku uchaguzi wake ukitarajia kufanyika Novemba 27.


Club News Editor

Comments

  1. Hongera sana ujiona wengi wamesema jambo la wengi lifanyie kazi kiongozi mzuri ni yule mwenye hekima

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

RC PWANI AONGOZA WAKAZI PWANI KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA

BARAZA LA MADIWANI KIBAHA MJINI LAMPONGEZA MKURUGENZI WAKE KWA KAZI NZURI ANAYOIFANYA SAMBAMBA NA KUONGEZA MAPATO.

RAIS SAMIA ATANGAZA KIBAHA MJINI KUWA MANISAPAA,MBUNGE KOKA AFURAHIA ASEMA KIBAHA ITANG'AA