KIKWETE AFANYA MAZUNGUMZO NA SHIRIKA LA KIMATAIFA LA KAZI (ILO)




Na. Julieth Ngarabali, PWANI

Ridhiwani Kikwete, Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, amekutana na kufanya mazungumzo na Mwakilishi mkazi wa Kanda ya Afrika Mashariki wa Shirika la Kazi  (ILO) Bi. Caroline Mugalla na mratibu wa Mipango ya Kitaifa  wa shirika hilo Bw. Edmund Moshy mchana leo , ofisini kwake Dodoma. 




Katika mkutano huo , wamekubaliana kuendeleza mashirikiano baina yao na kuwahakikishia utayari wao kuendelea kufanyia kazi maamuzi makubwa  yaliyoingiwa na Nchi yetu katika kusimamia maslahi mapana ya Wafanyakazi katika kada zote. #KaziInaendelea



Club News Editor - Charles Kusaga

Comments

Popular posts from this blog

BARAZA LA MADIWANI KIBAHA MJINI LAMPONGEZA MKURUGENZI WAKE KWA KAZI NZURI ANAYOIFANYA SAMBAMBA NA KUONGEZA MAPATO.

RAIS SAMIA ATANGAZA KIBAHA MJINI KUWA MANISAPAA,MBUNGE KOKA AFURAHIA ASEMA KIBAHA ITANG'AA

RC PWANI AFURAHISHWA NA UTENDAJI KAZI WA MKURUGENZI WA KIBAHA MJINI DKT.ROGERS SHEMWELEKWA