TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE YATEMBELEA BUNGE

Baadhi ya Viongozi wa Taasisi ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mkoni Pwani wakiwa kwenye Picha ya pamoja na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Pwani Subira Mgalu juzi walipotembelea Bunge kwa mualiko wa Mbunge huyo

Na. Yohana Msafiri Kibaha, Pwani.

Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani imetembelea Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Dodoma Februari 2, 2024 Kwa Mwaliko wa Mbunge wa viti maalumu Mkoa wa Pwani Bi. Subira Mgalu kwa lengo la  kujifunza Shughuli za Bungeni.

Viongozi wa Taasisi ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mkoni Pwani wakiwa Bungeni wakifuatilia mijadala ya Bunge inayoendelea.

Akizungumza na Mwàndishi wa habari hizi Katibu wa Taasisi hiyo Mkoani Pwani Omary Punzi amesema kuwa kitendo alichofanya Mbunge huyo kwa kuwakaribisha bungeni  kimewapa faraja kubwa kwani wameweza kujifunza mambo mengi ambayo yanahusisha maslahi ya nchi.

"Kwa niaba ya Taasisi ya Mwalimu Nyerere nampongeza Mbunge Mheshimiwa Subira Mgalu kwa namna alivyotujali na tumepata uelewa kwa kujifunza"amesema

 Pia alipongeza juhudi za Serikali ya awamu ya Sita ya Mh. Dk. Samia Suluhu Hassani kwa namna bunge lilivyokuwa linafanya kazi vizuri Kwa uchangamfu na kujibu hoja vizuri.

Mwisho




Charles Kusaga - Club News Editor

Comments

Popular posts from this blog

RC PWANI AONGOZA WAKAZI PWANI KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA

BARAZA LA MADIWANI KIBAHA MJINI LAMPONGEZA MKURUGENZI WAKE KWA KAZI NZURI ANAYOIFANYA SAMBAMBA NA KUONGEZA MAPATO.

RAIS SAMIA ATANGAZA KIBAHA MJINI KUWA MANISAPAA,MBUNGE KOKA AFURAHIA ASEMA KIBAHA ITANG'AA