MVUA YAUA WATATU, MMOJA ANING'INIA MTINI KWA SAA NNE
Na. Mwandishi wetu.
Akizungumza na vyombo mbalimbali vya habari ,Kamanda
wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Morogoro Shaban Marugujo amesema
aliyenusurika kifo ni Sengo Hamis(47) ambaye alipanda juu ya mti kwa zaidi ya
saa nne.
Amesema vifo vya watu hao vilitokea katika mtaa
wa Lukuyu kata ya Bigwa Manispaa ya Morogoro na kwamba tayari miili miwili
imeshaopolewa na jitihada za kuupata uliobaki zinaendelea
‘ni kweli watu watatu wamepoteza uhai na
wameshatambuliwa majina yao ni Asnath Thomas, Theresia Adolf(73) pamoja na Mwanahamis Issa(35) na taarifa ya hili tukio
tulichelewa kupata maana ilitufikia saa mbili asubuhi ya leo [Januari 11,2024]
na tukio lilitokea majira ya saa saba hivi usiku.”amesema na kuongeza
“Tunaona namna muda ulivyopotea bila taarifa
kutolewa, lakini taarifa ingetolewa mapema uwezekano wa kuwaokoa waliofariki
ingewezekana, sasa juhudi za kuutafuta
mwili wa Mwanahamisi zinaendelea,”ameongeza
Kamanda huyo pia ametahadharisha tabia ya baadhi
ya wananchi kupima maji kwa kuona ama kuweka mti huku akiwataka kusubiri maji
kupungua ama kuchuku tahadhari nyingine zaidi kabla ya kuamua kuyavuka.
Awali Mwenyekiti wa mtaa wa Bigwa standi Benjamin Suzee amesema siku hiyo ilinyesha mvua kubwa katika mtaa huo ambapo ilipelekea mto huo kujaa maji na kusababisha tukio hilo
Ameongeza kuwa majeruhi wa mafuriko hayo amelazwa katika hospitali ya rufaa mkoani humo na kwamba waliokumbwa na tukio hilo ni familia ya majeruhi huyo Sengo ambaye ndiye aliyetoa taarifa baada ya yeye kufanikiwa kupanda juu ya mti
‘nashauri kila mtu achukue tahadhari hasa kipindi hiki cha
mvua ambapo pamekuwa na matukio mbalimbali ya watu kusombwa na maji ama kuingiliwa
na maji kwenye makazi yao”amesema Benjamin
Comments
Post a Comment