Basi lapinduka likiwa safarini



Mwandishi wetu. 

Dodoma. Abiria  watatu wamejeruhiwa baada ya basi la kampuni ya Ally's waliokua wakisafiria  kutoka  Mkoani Shinyanga kwenda Dar es salaam  kupinduka  asubuhi ya leo katika eneo la Mnada mpya uliopo Mkoani Dodoma.

 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Martin Otieno amethibitisha kutokea ajali hiyo Januari 03, 2024 saa 12:15 asubuhi baada ya dereva wa basi hilo kushindwa kulithibiti na kupinduka.

" leo majira ya saa 12:15 asubuhi ndio hili tukio lilitokea  na ajali hii imesababisha  majeruhi watatu ambao majeraha yao ni ya kawaida na wanapatiwa matibabu hospitalini," amesema Otieno

Kamanda Otieno ametaja chanzo cha ajali ni dereva kushindwa kulithibiti kutokana na uchovu au matatizo ya kiafya hivyo kusababisha gari hilo kupinduka katika eneo hilo la mnada mpya jijini humo.

Ofisa habari wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma Jeneral, Renatha Mzanje ameongeza kuwa   majeruhi hao wote hali zao zinaendelea vema na bado wanaendelea na matibabu .




News Editor Julieth Ngarabali

Comments

Popular posts from this blog

BARAZA LA MADIWANI KIBAHA MJINI LAMPONGEZA MKURUGENZI WAKE KWA KAZI NZURI ANAYOIFANYA SAMBAMBA NA KUONGEZA MAPATO.

RAIS SAMIA ATANGAZA KIBAHA MJINI KUWA MANISAPAA,MBUNGE KOKA AFURAHIA ASEMA KIBAHA ITANG'AA

RC PWANI AFURAHISHWA NA UTENDAJI KAZI WA MKURUGENZI WA KIBAHA MJINI DKT.ROGERS SHEMWELEKWA