MATUMIZI YA GESI YAZINGATIWE KUJIHADHARI NA MAJANGA YA MOTO




Na. Mwandishi wetu , Pwani

Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Pwani Jenifa Shirima amewasihi Wananchi hasa wanawake kuzingatia matumizi bora ya nishati safi ya Gesi kwani kufanya hivyo kutasaidia kujihadhari dhidi ya majanga ya moto. Amewataka wananchi kuhakikisha wanatoa taarifa mapema pindi yanapotokea majanga ya moto.







Amesema kuwa matumizi ya gesi ni moja ya vyanzo vya moto endapo haitatumika kwa usahihi. Amewasihi kinamama kuhakikisha wanapotumia mitungi ya gesi wanakuwa wanaifunga kwa usahihi baada ya kuitumia na kuiweka sehemu salama ambayo watoto hawawezi kuifikia na kisha kufungua na gesi kuvuja na kusababisha majanga hayo ya moto.


 hayo wakati wa Tamasha la Bibi Titi Mohammed, 2023 lililofanyika kwenye uwanja wa Ujamaa, Ikwirir Rufiji Mkoa wa Pwani.


-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------


Club News Editor

Comments

Popular posts from this blog

BARAZA LA MADIWANI KIBAHA MJINI LAMPONGEZA MKURUGENZI WAKE KWA KAZI NZURI ANAYOIFANYA SAMBAMBA NA KUONGEZA MAPATO.

RAIS SAMIA ATANGAZA KIBAHA MJINI KUWA MANISAPAA,MBUNGE KOKA AFURAHIA ASEMA KIBAHA ITANG'AA

RC PWANI AFURAHISHWA NA UTENDAJI KAZI WA MKURUGENZI WA KIBAHA MJINI DKT.ROGERS SHEMWELEKWA