MAJALIWA AHITIMISHA TAMASHA LA BIBI TITI MOHAMED WILAYANI RUFIJI MKOANI PWANI



Na Gustafu Haule,Rufiji Pwani.

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa amempongeza waziri wa Tamisemi na Mbunge wa Jimbo la Rufiji Mohamed Mchengerwa kwa kazi kubwa aliyoifanya katika kipindi kifupi cha utekelezaji wa ilani katika Sekta ya Miundombinu. 

Majaliwa, amesema sekta ya miundombinu imepiga hatua kubwa kwa ujenzi wa barabara na madaraja makubwa yaliyokuwa na Changamoto kubwa kipindi cha misimu ya mvua. 

 


Ameyasema hayo katika kilele cha Miaka miwili ya kumbukizi ya Hayati Bibi Titi Mohamed Mwanasiasa Mwanamke wa kwanza Tanganyika kushiriki waziwazi katika juhudi za  kupigania uhuru wa Tanganyika  kipindi cha ukoloni.

 


Amesema hatua ya Jimbo la Rufiji kuwa na madaraja ya uhakika ni hatua nzuri hasa kwa mikoa ya kusini kuendeka bila changamoto yeyote. 

 

Pia ametoa salamu za Rais Dkt.Samia suluhu Hassan zenye lengo la  kuendelea kumkumbuka na kumuenzi Bibi Titi Mohamed kwa  kuthamini mchango wake katika harakati za uhuru wa Tanganyika. 

 


Amesema kauli mbiu ambayo italeta tija ya  kumkumbuka Bibi Titi Mohamed wakati wa sasa na baadaye ni kudumisha umoja, uzalendo na kuacha ujumbe kwa vizazi vijavyo. 

 

Waziri Majaliwa, amemuelezea Bibi Titi kuwa ni mwanamke jasiri, mkakamavu, na kujitoa kwake katika kuleta usawa wa kijinsia kwa wanawake na wanaume. 

 

Amesema kuendelea kumuenzi Bibi Titi ni kuendeleza usawa wa kijinsia kwa wanawake, na mchango wake katika kuleta maendeleo kuwa ni  shujaa, uhuru tulionao ni juhudi za Mashujaa waliopita. 

 

Ameeleza kuwa mawazo ya Bibi Titi ni mfano wa kuigwa kwa viongozi wanawake kama anavyofanya  Rais Samia.

 

Ameendelea kusema, kuwa maadhimisho hayo yawe chachu kupinga ukatili wa kijinsia na wanawake washiriki katika siasa na kufanya vizuri katika kuleta matokea chanya. 

 




Amesema Taifa lina kila sababu ya kukumbuka kazi nzuri na nguvu za  Rais Dkt.Samia kung'aa kimataifa kwa kuwa mwanadiplomasia namba moja kuimarisha uchumi, fursa za kibiashara, utalii na mageuzi makubwa ya uchumi.

 

Amesema  Rais Samia ameendelea kusimamia fursa za uchumi, elimu na diplomasia, siasa safi na ustaarabu.

 

Aidha ameimarisha sekta binafsi na kuendeleza mifumo ya sheria, na kuwezesha sekta binafsi kufanya kazi vizuri na kuhimiza ulipaji kodi. 

 

 Aisha,Majaliwa amesema kwa kipindi kifupi Dkt. Samia ameendelea kuhimiza utoaji wa elimu bure, kuongeza mikopo, maboresho mitaala ya elimu ili vijana wajiajiri, sekta ya afya hospital mpya 107 , huduma za kibingwa hadi ngazi za halmashauri. 

 

 Amesema  Rais Samia amehimarisha huduma za matibabu ya Moyo, ini, mifupa na uroto hii yote ni kuhakikisha anarudisha huduma ya afya karibu na wananchi. 

 

Waziri Mkuu amesema katika upande wa Siasa nafasi ya Mwanamke inazidi kuonekana kwa uwiano wa nafasi za teuzi kwa wanawake.

 

MWISHO.




Club News Editor

Comments

Popular posts from this blog

RC PWANI AONGOZA WAKAZI PWANI KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA

BARAZA LA MADIWANI KIBAHA MJINI LAMPONGEZA MKURUGENZI WAKE KWA KAZI NZURI ANAYOIFANYA SAMBAMBA NA KUONGEZA MAPATO.

RAIS SAMIA ATANGAZA KIBAHA MJINI KUWA MANISAPAA,MBUNGE KOKA AFURAHIA ASEMA KIBAHA ITANG'AA