LIGI YA MABINGWA AFRICA YAENDELEA
Na Gustafu Haule
LIGI ya Mabingwa
barani Afrika imeendelea leo Desemba 2, ambapo Klabu ya Yanga Sc imejikuta
ikiambulia sare ya kufungana 1-1 na mabingwa watetezi, Al Ahly katika
mchezo wa Kundi D uliochezwa Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es
Salaam.
Kipindi cha kwanza
timu zote mbili hakuna aliyeweza kuchungulia lango la mwenzake lakini kipindi
cha pili kilianza kwa kila mmoja kutumia mbinu mbadala ikiwemo kufanya
mabadiliko ya wachezaji wake.
Mabadiliko hayo
yalizaa matunda ambapo Mabingwa watetezi Al Ahly walipata bao dakika ya 86
kupitia Percy Tau ambapo Yanga waliweza kisawazisha mnamo dakika ya 90+1
kupitia kiungo mahiri kutoka Ivory Coast, PacĂ´me Zouzoua.
Kwa Matokeo hayo
Mechi inayofuata Yanga
SC itasafiri hadi nchini Ghana kucheza na Medeam Ijumaa ya Desemba 8,
wakati Al Ahly watawakaribisha CR Belouizdad Jijini Cairo.
MWISHO



Comments
Post a Comment