SHIUMA KIBAHA WAPEWA MREJESHO NAMNA YA KUNUFAIKA NA MIKOPO KUTOKA SERIKALINI

Na. Mwandishi Wetu, Pwani

Shirikisho la Umoja wa Machinga (SHIUMA) Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani wamemshukuru Mheshimiwa Rais Daktari SAMIA SULUHU HASSAN Kwa kuona umuhimu wa kuwatambua kama Kundi la wafanyabiashara nao kuweza kukopesheka na kupata fursa mbalimbali na kufikia malengo Katika Biashara zao.

 

Akizungumza katika Mkutano wa Shirikisho hilo wakati wa kutoa mrejesho kwa wafanyabiashara hao Mwenyekiti wa Machinga Mkoa wa Pwani Ndugu FILEMON MALIGA, alieleza namna ambavyo wametengewa maeneo na kuwezeshwa Shilingi Milioni kumi Kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya Shirikisho hilo na alieleza kuwa watakaa mahali pamoja na kuweza kukopesheka 



Mwenyekiti wa Machinga Mkoa wa Pwani Ndugu FILEMON MALIGA        
         
                              

Katibu wa Mbunge Kibaha Mjini Ndugu Method Mselewa 
   

                  

Wajumbe wa Mkutano wa Shirikisho la Umoja wa Machinga (SHIUMA) wakifuatilia Mkutano


Aidha Shirikisho hilo wakiwa wamemwalika Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Mh. Silvester Koka ambaye amewakilishwa na Katibu wake Ndugu Method Mselewa wamemuomba ushirikiano katika kuhakikisha wanafanikiwa kujenga Ofisi yao Ili waweze kukaa Mahali pamoja.

Akizungumza na wafanyabiashara hao Katibu huyo wa Mbunge Ndugu Mselewa amesema Serikali inawathamini sana wafanyabiashara hivyo nao wathamini mikopo wanayopewa na waweze kurudisha Kwa wakati sambamba na kuwahakikishia ushirikiano kutoka Ofisi ya Mbunge.

Aidha kwa upande wao wafanyabiashara wamesema wanaishukuru Serikali kwa kutambua umuhimu wao kuwawezesha na kuwajengea soko.



Wafanyabiashara Wamachinga katika shughuli zao za biashara







 

 

Comments

Popular posts from this blog

RC PWANI AONGOZA WAKAZI PWANI KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA

BARAZA LA MADIWANI KIBAHA MJINI LAMPONGEZA MKURUGENZI WAKE KWA KAZI NZURI ANAYOIFANYA SAMBAMBA NA KUONGEZA MAPATO.

RAIS SAMIA ATANGAZA KIBAHA MJINI KUWA MANISAPAA,MBUNGE KOKA AFURAHIA ASEMA KIBAHA ITANG'AA