Posts

Showing posts from May, 2024

Elimu ya tembo inavyoboresha maisha ya wanafunzi .

Image
Beatrice Lihaku ni mwalimu wa somo la mahusiano kati ya Tembo na wanafunzi shuleni Na Julieth Ngarabali.   Hana wasiwasi tena wa kutimiza ndoto yake ya kuelimika na kuwa kiongozi mwenye mafanikio katika jamii.  Uhakika huu umetokana na kikwazo cha kwenda shule kusoma kuondo lewa.  Huyu ni Joseph Sefu, mwanafunzi Shule ya Msingi Mlimani iliyopo Kata ya MangĂșla ‘B’ Halmashauri ya Mji wa Ifakara mkoani Morogoro.  Joseph Sefu, mwanafunzi Shule ya Msingi Mlimani akieleza namna yeye na familia yake walivyonufaika na somo laTembo shuleni. Wanafunzi wa shule tatu za msingi na awali za Mlimani, Kanyenja na Magombera akiwemo Joseph walikuwa wanakabiliwa na changamoto ya tembo kuvamia makazi ya watu katika Kata ya Mang’ula ‘B’.hivyo muda mwingi wakawa ni wenye hofu tu. Tembo hawa walikuwa wakifanya uharibifu wa makazi, mashamba, kujeruhi na hata kuondoa uhai wa watu matukio yaliyochangia hofu na wasiwasi mkubwa kwa watoto wakiwemo wale wa chini ya miaka nane. Hali hii iliwawek...

Mkaa mbadala ulivyosaidia kupunguza uharibifu ushoroba wa Nyerere Selous-Udzungwa

Image
Na. Monica Msomba.Kilombero Alikuwa ni miongoni mwa wanawake waliokuwa wakiamini kuwa kuni na mkaa ndio nishati pekee ya kutumia katika kupikia. Hata hivyo, alichokua anakiamini hakikuwa sahihi, mpaka alipokuja kugundua kuwa nishati ya kuni na mkaa ina madhara makubwa kiafya. Huyu ni Arafa Makeleketa, mkazi wa Mang’ula ‘B’ Halmashauri ya Mji wa Ifakara mkoani Morogoro ambaye ameachana na matumizi ya nishati hizo baada ya kupata elimu ya matumizi ya mkaa mbadala usio na madhara kiafya. Arafa Makeleketa ni mmoja wa waathirika wa matumizi ya mkaa na kuni katika kijiji cha Mang'ula B “Nimetumia mkaa na kuni kwa zaidi ya miaka 20 nikiwa napika maandazi na chapati vimenifanya  kupata ugonjwa wa kifua nakohoa mfululizo,” anasema Arafa, aliyewahi kuwa mama lishe maarufu Mang’ula B. Arafa ambaye yeye na wenzake walikuwa wakiingia ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Milima ya Udzungwa kuokota kuni anasema madhara aliyopata katika mfumo wa upumuaji hatamani tena mkaa na kuni. “Ninachowashauri mama l...

RC PWANI AGUSWA NA MCHANGO WA WAANDISHI WA HABARI MKOANI KWAKE, AJIPANGA KUWEKA MKAKATI WA KUWAINUA KIUCHUMI.

Image
Na Gustafu Haule,Pwani MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge, amesema anathamini michango ya waandishi wa habari waliopo katika Mkoa wake kwakuwa wanafanyakazi kubwa ya kuchochea maendeleo. Kunenge,ametoa kauli hiyo leo Mei 23 wakati akifungua mkutano wa maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari uliofanyika katika ofisi za  Mkoa huo  ukiwajumuisha Waandishi wa habari pamoja na wadau mbalimbali. Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge akizungumza katika ufunguzi wa maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yaliyofanyika leo Mjini Kibaha yakiandaliwa na Klabu ya Waandishi wa habari Mkoa wa Pwani (CRPC). Katika maadhimisho hayo yaliyoandaliwa na Klabu ya Waandishi Wa Habari Mkoa wa Pwani Kunenge amesema ,kazi wanazofanya Waandishi wa habari katika Mkoa wake zinaonekana na zimekuwa zikileta matokeo chanya huku akisema lazima wathaminiwa. Amesema , kutokana na mchango mkubwa unaotolewa na waandishi hao ,yeye yupo mstari wa mbele kutoa ushirikiano katika kuhakikisha...