WAFANYABIASHARA SOKO LA LOLIONDO KIBAHA WAPATA VIONGOZI WAPYA, MNEMBWE AENDELEA KUSHIKA USUKANI.
Na Gustafu Haule,Pwani WAFANYABIASHARA wa Soko la Mnarani lililopo Loliondo Kata ya Tangini katika Halmashauri ya Mji Kibaha wamefanikiwa kupata viongozi wapya watakaoongoza Soko hilo kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo. Viongozi hao wamepatikana kufuatia uchaguzi uliofanyika Disemba 22 mwaka huu sokoni hapo ambapo hatahivyo nafasi ya mwenyekiti imekwenda kwa Mohamed Omari (Mnembwe). Mwenyekiti wa Soko la Mnarani Ndugu Mohamed Omari (Mnembwe) Mnembwe,ambaye alikuwa anatetea nafasi yake ameshinda kwa kishindo baada ya kumbwaga mpinzani wake Anthony Maganga ambaye alijikuta anapata kura 130 dhidi ya Mnembwe aliyepata kura 423. Pichani wapiga kura wakipiga kura kuchagua viongozi katika Soko hilo Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo msimamizi wa uchaguzi kutoka ofisi ya Mtendaji Kata ya Tangini Idd Hassan,amesema kuwa Mnembwe ameshinda nafasi hiyo baada ya kupata kura nyingi zaidi ya mwenzake . "Nafasi ya mwenyekiti ilikuwa na wago...