Posts

SHULE YA MSINGI MKOANI YADAI WAZAZI ZAIDI YA SH.MILIONI 168,

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani SHULE ya Msingi mkoani yenye mchepuo wa kiingereza iliyopo kata ya Tumbi katika  Manispaa ya Kibaha Mkoani Pwani ipo katika wakati mgumu wa  kutekeleza majukumu yake kutokana na baadhi ya  wazazi kushindwa kulipa ada kwa wakati. Shule hiyo ya serikali ilianzishwa mwaka 2018 ili kuwawezesha wanafunzi kupata masomo sawa na Shule za Kiingereza za binafsi ( Private) lakini changamoto iliyopo hivi sasa ni wazazi kushindwa kulipa ada ambayo ni Sh.400,000 kwa mwaka. Ada hiyo ni mgawanyo wa mihula miwili ambapo kila baada ya miezi Sita mzazi anatakiwa kulipa Sh.200,000 lakini bado wazazi wanashindwa kulipa jambo ambalo linapelekea uendeshaji wa Shule hiyo kuwa mgumu. Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Adelhelma Chawa akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake juzi amesema kuwa mpaka kufikia Julai 11,2025 shule hiyo inawadai Wazazi kiasi cha Sh.milioni 168,956,000. Mkuu wa Shule ya Msingi Mkoani iliyopo katika Manispaa ya Kibaha Adelhelma Chawa akizungumza na...

93 WAJITOKEZA KUCHUKUA FOMU ZA KUGOMBEA UBUNGE MKOA WA PWANI

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani  WANACHAMA 93 wa Chama Cha Mapinduzi ( CCM) kutoka Mkoani Pwani wamejitokeza  kuchukua fomu za  kuomba kuteuliwa na chama kwa ajili ya kugombea nafasi ya ubunge katika majimbo mbalimbali yaliyopo Mkoani Pwani. Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo wa Mkoa wa Pwani David Mramba ametoa taarifa hiyo Julai 2 ,2025 wakati akizungumza na Waandishi wa habari katika ofisi za CCM Mkoa wa Pwani zilizopo Mjini Kibaha . Mramba amesema kuwa Mkoa wa Pwani una majimbo tisa ambapo tangu dirisha la uchukuaji fomu za kuwania nafasi ya ubunge Mkoa wa Pwani umepata wagombea 93 na kati ya hao Wanaume ni 71 na Wanawake 22. "Mchakato wa uchukuaji fomu na kurudisha kwa ajili ya kuomba ridhaa ya kugombea ubunge katika majimbo ulianza Juni 28 na kumalizika Julai 2, 2025 na katika mchakato huo Pwani wamejitokeza wanaCCM 93 katika majimbo yote tisa",amesema Mramba Mramba ametaja majimbo hayo na idadi ya wagombea  kuwa ni Chalinze yenye wagombea (3) Wanaume akiwemo Ridhiwani...

MANISPAA YA KIBAHA YAFANYA KIKAO KAZI KUIMARISHA UWAJIBIKAJI

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani HALMASHAURI ya Manispaa ya Kibaha imefanya kikao kazi maalum kilichowakutanisha Maafisa Kilimo na Maafisa Maendeleo ya Jamii kwa lengo la kukumbushana wajibu wa kila siku katika kutekeleza majukumu yao ya kiutumishi. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Kibaha Julai 1, 2025 kikilenga kuimarisha utendaji kazi, uwajibikaji, ubunifu katika ukusanyaji wa mapato ya ndani pamoja na utoaji wa huduma bora kwa wananchi. Baadhi ya Watumishi wa Manispaa ya Kibaha wakiwa katika kikao kazi cha kujadili uwajibikaji kazini kilichofanyika jana. Akizungumza wakati wa kikao hicho, Mkurugenzi wa Manispaa ya Kibaha, Dkt. Rogers Shemwelekwa, amewataka watumishi wote kuongeza ubunifu katika kazi zao, kuachana na kufanya kazi kwa mazoea, na kuhakikisha mapato ya ndani yanakusanywa kikamilifu kwa maendeleo ya Halmashauri na wananchi wake. Mkurugenzi wa Manispaa ya Kibaha Dkt.Rogers Shemwelekwa akizungumza katika kikao kazi na watumishi wake kilichofanyika jana katika Uk...

ASASI ZA KIRAIA ZAOMBWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SERIKALI.

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani KAIMU Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Nsajigwa George, amezitaka asasi za kiraia na mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) kufanya kazi kwa kuzingatia sheria, kanuni, uwazi na uwajibikaji ili kuongeza tija katika utoaji wa huduma kwa jamii. Nsajigwa ametoa kauli hiyo Juni 26, 2025 wakati akifungua mkutano wa jukwaa la mashirika yasiyo ya kiserikali mkoa wa Pwani uliofanyika katika Ukumbi wa mdogo wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Pwani. Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani George Nsajigwa akizungumza katika kikao cha mashirika yasiyo ya kiserikali Juni 26,2025 Mjini Kibaha  Katika hotuba yake Nsajigwa amesisitiza umuhimu wa mashirika hayo kuzingatia taratibu za kisheria katika utekelezaji wa majukumu yao  hasa katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye mchakato wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025. “Mwaka 2025 ni mwaka wa uchaguzi, naomba niagize kuwa mashirika yote yafanye kazi kwa kuzingatia sheria na kanuni,msibadilike na kuwa sehemu ya migawanyiko ya kis...

DKT.CHARLES MWAMAJA AIPIGA TAFU KLABU YA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA PWANI.

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani MDAU wa maendeleo na mkazi wa Kibaha Mjini Mkoani Pwani Dkt.Charles Mwamaja ameipiga tafu Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Pwani kwa kuwapa samani za ofisi ikiwemo viti. Mwamaja, ambaye pia ni Kamishna kutoka Wizara ya fedha amekabidhi vifaa hivyo Juni 24, 2025 kupitia mwakilishi wake Philemon Maliga hafla ambayo imefanyika katika ofisi za Waandishi wa habari zilizopo Kibaha Mjini. Picha za makabidhiano ya samani za ofisi baina ya mdau wa maendeleo Dkt.Charles Mwamaja na Klabu ya Waandishi wa habari wa Mkoa wa Pwani. Awali, akizungumza kabla ya kukabidhi samani hizo  Maliga amesema kuwa  samani hizo ni sehemu ya kuonyesha ushirikiano kati ya Klabu ya waandishi wa habari na wadau wa maendeleo.  Maliga amesema  kuwa Waandishi wa Habari ni chombo ambacho kinachotumika kuelimisha jamii katika mambo mbalimbali hivyo wanatakiwa kupewa ushirikiano kutatua vikwazo vyao. Maliga, ameongeza kuwa msaada wa  samani hizo sio mwisho kwani ataendele...

MWENYEKITI KITONGOJI CHA KWAKIBOSHA MAPINGA AWAPIGA MSASA VIJANA 500 KULINDA AMANI YA TAIFA.

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani MWENYEKITI wa Kitongoji cha Kwakibosha kilichopo Kata ya Mapinga Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani Shaban Athumani amewataka vijana kuacha kutumika na watu wachache wenye nia ovyo ya kutaka  kuharibu amani na utulivu hapa nchini. Athumani ametoa wito huo katika mdahalo maalum wa kuwajengea uwezo vijana juu ya kukabiliana na vitendo viovu sambamba na kuwahamasisha vijana kulinda amani ya Taifa iliyoasisiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Mmoja wa Vijana wa Kitongoji cha Kwakibosha Mohamed Omary akichangia mada katika mdahalo huo Mdahalo huo umefanyika Juni 14, 2025  katika Kitongoji hicho na kuwashirikisha vijana zaidi ya 500 kutoka makundi mbalimbali wakiwemo bodaboda,mama lishe ,wapaka rangi na hata vijana kutoka UVCCM . Athumani, amesema kuwa mwaka 2025 ni mwaka wa uchaguzi mkuu unaokwenda kuwaweka madarakani viongozi akiwemo Rais, Wabunge na Madiwani na hiyo ndio fursa kwa vijana kuchagua viongozi wanaowataka. Mwenyekiti wa Kitongoji...

RC PWANI AFURAHISHWA NA UTENDAJI KAZI WA MKURUGENZI WA KIBAHA MJINI DKT.ROGERS SHEMWELEKWA

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani  MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge,amelipongeza Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Mji Kibaha kupitia mkurugenzi wake Dkt.Rogers Shemwelekwa kwa kazi nzuri ya kutekeleza miradi ya maendeleo iliyofanywa kwa kipindi cha mwaka 2020/2025. Aidha, Kunenge amesisitiza Baraza hilo kuwa katika kipindi cha mwaka 2025 /2030 wahakikishe wanapanga miradi yenye kipaumbele ili kuleta matokeo chanya katika jamii. Kunenge,ameyasema hayo Juni 16,2025 wakati akizungumza katika kikao maalum cha Baraza la Madiwani kwa ajili ya kujibu hoja za mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali (CAG)kikao ambacho kimefanyika katika Halmashauri ya Mji Kibaha. Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Musa Ndomba akizungumza katika kikao cha  Baraza maalum la kujibu hoja za mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) kilichofanyika Juni 16,2025  Amesema kuwa Kibaha Mjini imekuwa Halmashauri ya kuigwa kwakuwa katika kipindi kifupi tangu mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Dkt.Shemwelekwa kui...