CCM MKOA WA PWANI YASISITIZA UTULIVU KWA WAGOMBEA UBUNGE NA UDIWANI.

Na Gustaphu Haule,Pwani CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani kimewataka wagombea wa ubunge na udiwani walioongoza katika mchakato wa kura za maoni kuwa watulivu mpaka hapo utaratibu wa chama utakapokamilika. Aidha, kimewataka wagombea wa ubunge wa vitimaalum walioongoza kuacha kubweteka na badala yake wapite katika maeneo yao kwa ajili ya kumuombea kura mgombea wa Urais wa CCM Dkt . Samia Suluhu Hassan. Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi ( CCM) Mkoa wa Pwani David Mramba ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na Waandishi wa habari Agosti 14,2025 kwenye ofisi za CCM Mkoa zilizopo katika Manispaa ya Kibaha. Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM )Mkoa Pwani David Mramba akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu mchakato wa kujadili majina ya wagombea ubunge na udiwani wa Mkoa wa Pwani ,kikao hicho kimefanyika Agosti 14,2025 katika ofisi za CCM Mkoa zilizopo katika Manispaa ya Kibaha. Mramba, amesema kuongoza katika uchaguzi wa kura za...