Posts

CCM MKOA WA PWANI YASISITIZA UTULIVU KWA WAGOMBEA UBUNGE NA UDIWANI.

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani kimewataka wagombea wa ubunge na udiwani walioongoza katika mchakato wa kura za maoni kuwa watulivu mpaka hapo utaratibu wa chama utakapokamilika.  Aidha, kimewataka wagombea wa ubunge wa vitimaalum walioongoza kuacha kubweteka na badala yake wapite katika maeneo yao kwa ajili ya kumuombea kura mgombea wa Urais wa CCM Dkt . Samia Suluhu Hassan. Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi ( CCM) Mkoa wa Pwani David Mramba ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na Waandishi wa habari Agosti 14,2025 kwenye ofisi za CCM Mkoa zilizopo katika Manispaa ya Kibaha. Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM )Mkoa Pwani David Mramba akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu mchakato wa kujadili majina ya wagombea ubunge na udiwani wa Mkoa wa Pwani ,kikao hicho kimefanyika Agosti 14,2025 katika ofisi za CCM Mkoa zilizopo katika Manispaa ya Kibaha. Mramba, amesema kuongoza katika uchaguzi wa kura za...

WIZARA YA AFYA YASEMA:UGONJWA WA SIKOSELI SIO WA KUROGWA, YAHAMASISHA JAMII KWENDA KUPIMA VINASABA

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  WIZARA ya afya  Kitengo cha Sikoseli imesema kuwa ugonjwa wa Selimundu (Sickle Cell) sio ugonjwa wa kurogwa kama ambavyo jamii inachukulia lakini  ugonjwa huo ni wakurithi kutoka kwa mzazi mmoja kwenda kwa mzazi mwingine. Imesema ili kujiepusha na ugonjwa huo ni vyema kabla ya kuingia katika mahusiano jamii inapaswa kuchukua hatua ya kwenda kupima vinasaba vya ugonjwa na endapo watakuwa salama wanaweza kuoana na hatimaye kujenga familia salama isiyo na ugonjwa huo wa Selimundu (Sickle Cell). Daktari Bingwa wa magonjwa ya damu kutoka katika hospitali ya Amana iliyopo Jijini Dar es Salaam Jamila Makame, ametoa kauli hiyo katika semina ya siku moja kwa  baadhi ya Waandishi wa Mkoa wa Pwani iliyolenga masuala ya ugonjwa wa Selimundu Semina hiyo iliyofanyika Agosti 12, 2025 katika kituo cha afya Mkoani kilichopo Manispaa ya Kibaha iliwajumuisha baadhi ya Waandishi wa habari ambapo Dr.Makame amesema "Sickle Cell" ni ugonjwa wa kurithi ambao chanzo...

RAS PWANI KUANZA ZIARA MANISPAA YA KIBAHA AMSIFU DKT .ROGER'S SHEMWELEKWA KWA UKUSANYAJI MAPATO

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani  KATIBU Tawala wa Mkoa wa Pwani Pili Mnyema, ameanza ziara yake ya kikazi katika Halmashauri za Mkoa wa Pwani kwa kutembelea Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha. Katika ziara hiyo, Mnyema amesisitiza umuhimu wa ubunifu katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ili kuongeza mapato ya Halmashauri pamoja na Mkoa kwa ujumla. Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Pili Mnyema katika kikao na watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha alipofanya ziara ya kuzungumza na watumishi wa Manispaa hiyo Agosti 12, 2025 "Naomba tumuunge mkono mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kubuni vyanzo vipya vya mapato na hii ni miongoni mwa maagizo niliyopatiwa ili kusaidia kuongeza mapato ya Mkoa wetu," amesema  Mnyema. Aidha, amempongeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Kibaha Dkt.Rogers Shemwelekwa kwa kuendelea kubuni na kusimamia miradi mbalimbali yenye tija, ambayo imesababisha ongezeko la mapato ya Manispaa hiyo kila mwaka. ...

MWENEZI CCM PWANI AKOLEZA MOTO USIKU WA COREFA,ASIFU MAANDALIZI YAKE

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani CHAMA Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) kimetoa tuzo kwa wachezaji na wadau mbalimbali waliochangia kwa namna au nyingine katika kuendeleza mchezo wa mpira wa Miguu katika msimu wa mwaka 2024/2025. Hafla hiyo imefanyika Agosti 9, 2025 katika ukumbi wa Maisha Plus uliopo karibu na ofisi ya Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani ambapo mgeni rasmi katika hafla hiyo Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Pwani. Katibu Siasa , Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani David Mramba (Kulia)akitoa tuzo kwa mmoja wa wadau wa michezo waliofanya vizuri katika msimu wa mwaka 2023/2024. Katibu Siasa , Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani David Mramba (Kulia)akitoa tuzo kwa mmoja wa wadau wa michezo waliofanya vizuri katika msimu wa mwaka 2023/2024. Zaidi ya wadau 50 walishiriki hafla hiyo wakiwemo  waamuzi wa mpira wa miguu, wachezaji wa mpira wa miguu ,viongozi wa vyama vya miche...

CCM PWANI YATANGAZA MATOKEO UBUNGE KURA ZA MAONI

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani  KATIBU wa Siasa ,Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM ) Mkoa wa Pwani David Mramba ametangaza matokeo ya uchaguzi wa kura za maoni uliofanyika Agosti 4, 2025. Mramba ametangaza matokeo hayo mbele ya Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali katika mkutano uliofanyika ofisi ya CCM Mkoa wa Pwani Agosti 5, 2025. Mramba ametangaza matokeo ya  Jimbo la Kibiti ambapo alisema  Jimbo hilo lilikuwa na wagombea watatu huku idadi ya wapiga kura ni 10,277 na kura zilizopigwa 7007, kura zilizoharibika 137 na kura. halali ni 6870 na  aliyeongoza ni  Amina Musa Mkumba aliyepata kura 4,712,Kharid Mtalazaki amepata kura 1102, na  Ally Seif Ungando 1068. Katika jimbo la Rufiji Mramba amesema kura zilizopigwa ni 8,534 ,zilizoharibika 1, na kura halali 8,533 ambapo Hamisi Kisoma amepata kura  nane,Salum Ponga amepata kura 34 , Selemani Muekela amepata kura 26, na Mohamed Mchengerwa ameongoza kwa kupata kura 8,465. Jimbo la Mafia amesema ku...

HAMOUD JUMAA AJIZOLEA KURA 3,247 AONGOZA UCHAGUZI KURA ZA MAONI

Image
Na Gustaphu Haule,Pwani MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Taifa kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Hamoud Jumaa (MNEC) amefanikiwa kumbwaga aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini Michael Mwakamo kwa kupata kura 3,247. Hamoud ameshinda katika uchaguzi wa kura za maoni wa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) uliofanyika Agosti 4, 2025 katika Jimbo la Kibaha Vijijini lililopo Mkoani Pwani. Mgombea aliyeshinda katika uchaguzi wa kura za maoni za Chama Cha Mapinduzi (CCM)katika Jimbo la Kibaha Vijijini Hamoud Jumaa.  Uchaguzi wa kura za maoni umefanyika kwa ajili ya kutoa nafasi kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa Jimbo la Kibaha Vijijini kwa ajili ya kumpata mwakilishi wa kugombea ubunge katika uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 29 mwaka huu. Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi ( CCM) Mkoa wa Pwani David Mramba ametoa taarifa hizo katika mkutano na Waandishi wa habari uliofanyika leo Agosti 5,2025 katika Ofisi za CCM Mkoa wa Pwani. Mramba ,amesema kuwa katika Jim...

KOKA ASHINDA UCHAGUZI KURA ZA MAONI CCM KIBAHA ANYAKUA KURA 2,824

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  Mbunge mstaafu wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka amefanikiwa kushinda katika uchaguzi wa kura za maoni kwa kupata kura 2,824 na kuwaacha mbali wengine watano waliokuwa wakipambania nafasi hiyo. Mbunge mstaafu wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka akipiga kura Katika uchaguzi wa kura za maoni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) uliofanyika Agosti 4 Kata ya Tumbi. Akitangaza matokeo hayo mara baada ya uchaguzi wa kura za maoni uliofanyika  Agosti 4, 2025 Katibu wa CCM Kibaha Mjini Isaack Kalleiya amemtangaza Koka kuwa ni mshindi aliyeongoza kwa kupata kura nyingi zaidi.  . Kalleiya,amesema Kibaha Mjini inakata 14 na jumla ya wajumbe 6300 walipaswa kupiga kura katika uchaguzi huo lakini kura zilizopigwa ni 5,743, zilizoharibika 53 na kura halali 5,682. Amesema katika matokeo hayo Koka ameongoza kwa kupata kura 2,824,akifuatia na Musa Mansour aliyepata kura (1,775), Abubakar Allawi aliyepata kura (727),Dkt.Charles Mwamwaja( 282), Magreth Mwihava (39...