Posts

Showing posts from October, 2025

RC PWANI ATAKA MRADI WA IPOSA UTOE MATOKEO CHANYA KWA VIJANA

Image
Na Gustaphu Haule, Pwani  MKUU wa Mkoa wa Pwani  Abubakar Kunenge, ameielekeza Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima kuhakikisha programu ya Mpango wa IPOSA  inakuwa na matokeo chanya kwa kuwajengea vijana uwezo wa kujiajiri na kuajirika. IPOSA ni Mpango ulioandaliwa na Taasisi ya Elimu ya Watu wazima wa elimu changamani kwa Vijana walio nje ya Shule.  Kunenge ametoa maelekezo hayo wakati akifunga mafunzo ya walimu wa programu hiyo yaliyofanyika Oktoba 2,2025 katika  ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha. Mkuu wa mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge akizungumza na wasimamizi wa mradi wa IPOSA katika mkutano uliofanyika Oktoba 2,2025 katika ukumbi mdogo wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha. Alisema kuwa  elimu inayotolewa kupitia IPOSA haipaswi kubaki kwenye vyeti pekee, bali iwe chachu ya mabadiliko katika maisha ya vijana ambao wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya ajira. “Mradi huu wa IPOSA lazima uwe na matokeo ya kweli, vijana wanapaswa kufundish...

TISEZA YAKARIBISHA WAWEKEZAJI KWALA YATENGA EKARI 100 KWA AJILI YA UWEKEZAJI

Image
  Na Gustaphu Haule, Pwani  MAMLAKA ya Uwekezaji na Maeneo Maalumu ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) imesema imetenga ekari 100 katika eneo la Kwala katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani kwa ajili ya ujenzi wa viwanda. Kaimu Meneja Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma kutoka TISEZA Adelina Rushekya ametoa kauli hiyo Septemba 30,2025 wakati akizungumza na Waandishi wa habari katika mkutano maalum uliofanyika eneo la Kwala. Kaimu meneja Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma kutoka TISEZA Adelina Rushekya akizungumza na Waandishi wa habari katika eneo la Kwala. Rushekya amesema kuwa maeneo ya Kwala yana vivutio vinavyotakiwa kwa ajili ya uwekezaji huku akisema fursa za uwekezaji zipo vizuri katika kila sekta. Rushekya amesema mwekezaji atakayekuwa tayari kuwekeza katika eneo hilo atapatiwa ekari moja na pia anatakiwa kuwa na mtaji wa dola za Kimarekani milioni tano kwa wazawa na kwa raia wa kigeni anatakiwa kuwa na dola milion kumi. Aidha Rushekya amesema kuwa  mwekezaji at...